Ukiona Redflags hizi, usioe

Ukiona Redflags hizi, usioe

No 90 izingatiwe zaidi

Mambo ya Sikupi mpaka ufanye hiki au sikupi mpaka unioe, ukiikubali utateseka huko ndoani
Mkuu, sidhani kwa namna ulivyoifafanua wewe ndiyo muktadha halisi wa mwandishi!

Ukiomba ukapewa kabla ya ndoa, ni kitu gani utachokuwa umebakiza kwake cha kukufanya usilale ukimuwaza yeye na kuharakisha kumuoa?

Hili sikuungi mkono.
 
UKIONA REDFLAGS HIZI USIOE 🚩

Sio kila anayekupenda anafaa kuwa mke wako, Wengine ni majaribu ya maisha.

Kabla hujaoa, fungua macho yako vizuri 👇

1. Hana tabia ya kukubali makosa
Kila kitu ni kulaumu wengine(sababu kibao)… hana “samahani” ya kweli.

2. Anatafuta attention kwa wanaume wengine
Akikosa validation, anahangaika… huyu hataridhika kirahisi.

3. Ana historia ya mahusiano mengi yaliyoshindikana
Sio bahati mbaya… ni pattern. ukijitia mjuaji utakasikia

4. Hana heshima kwa wanaume
Leo anawadharau wengine, kesho ni zamu yako.

5. Ana mood swings za kupindukia
Leo anakupenda, kesho anakuchukia… ndoa itakuwa vita ya hisia.

6. Hana self-control
Anaishi kwa tamaa na hisia, sio akili.

7. Hana mwelekeo wa maisha
Hajui anataka nini… na wewe utapotea naye.

8. Maisha yake ni drama kila siku
Kila mtu ana tatizo naye… utakuwa next.

9. Anatumia mapenzi kama silaha
Anakupa au anakunyima ili akudhibiti. Atakuendesha

10. Hana misingi ya maadili
Anafuata utandawazi, sio principles.


Kama hakuheshimu… hata kama anakupenda, ONDOKA.


Upendo unaweza kukuingiza kwenye ndoa…
Lakini tabia ndio itaamua kama utaishi kwa amani au mateso.

Chagua kwa akili, sio hisia.


✍️Abuuabdillah
Umepiga pale pale kwenye mshono. Miaka ya nyuma niliamua kuishi na mwanamke mmoja ambaye alikuwa karibu na hizi red flags zote ulizoziorodhesha..... hali ilikuwa mbaya. Utaomba dunia ikumeze. Yaani hizi dalili kila kijana wa kiume anatakiwa azijue na ahakikishe amezichunguza zote.
 
Vp ikiwa tayar ushazaa naye ila hujaoa ndo unagundua hizi tabia mbovu....
Hee... kwani hujui ukikutana na mnyama simba unafanya nini? Miguu ina kazi gani? Ndiyo... watoto wanaweza kuwa kikwazo ila njia nzuri sana ni kuwachukuwa wewe uishi nao. Ukimwachia watoto wanawake wa aina hiyo watakunyoosha.
 
Hee... kwani hujui ukikutana na mnyama simba unafanya nini? Miguu ina kazi gani? Ndiyo... watoto wanaweza kuwa kikwazo ila njia nzuri sana ni kuwachukuwa wewe uishi nao. Ukimwachia watoto wanawake wa aina hiyo watakunyoosha.
Ndo maana watu wanashauri kuwa makini sana na mtu kuzaa naye na hii ni kote kote mwanaume au mwanamke
 
Ndo maana watu wanashauri kuwa makini sana na mtu kuzaa naye na hii ni kote kote mwanaume au mwanamke
Swala la mahusiano tena kufikia hatua ya kupata mtoto pamoja inatakiwa umakini coz unaweza kuzaa na shetani ukaishia kujuta maisha yako yote

Mi nasema ndoa sio ya kila mtu
Ukiona kabisa mahusiano yanakugalagaza Kifo cha mende ndoa ya nini sasa?
 
Back
Top Bottom