Ukimya wenu unatia mashaka uumini wenu kwa Mungu mnayemtumikia wakati kondoo wanahitaji kauli yenu. Tutawasikia siku ikitangazwa kuwa Tanzania ni nchi ya kiislamu, au inajiunga OIC, hapo maaskofu mtalipuka , maana linahusu maslahi yenu. Hivyo hivyo Masheikh ikisemwa sheria ya ndoa ni mke mmoja mtalipuka kwa vile imegusa imani yenu.
Nyote Kuminywa kwa democrasia hakuwahusu, mko kimya
==============================
Nyote Kuminywa kwa democrasia hakuwahusu, mko kimya
==============================
Hapa tupate majibu. Baraza LA maaskofu (TEC) na Jumuia ya Kikristo (CCT) ni makundi yanayoheshimika sana.
Kwenye mitandao kumekuwa na tuhuma kuwa pamoja na utawala wa awamu ya tano kuja na speed kubwa ya kusigina katiba na sheria kiasi cha kuhatarisha amani ya nchi kuliko kipindi chochote toka uhuru hawaja kemea hali hiyo kwa vile muhusika ni muumini wao tofauti na JK ambaye walikuwa wanamkomalia hata masuala madogo madogo.
Taarifa hizo binafsi zimenifedhehesha na kujiuliza jee kuna ukweli? Kama ni hivyo hamuoni mna tuondolea imani tuliyokuwa nayo na taasisi hizo?