BABA TUPAC
JF-Expert Member
- Sep 30, 2015
- 1,533
- 3,837
Hakuna adhabu kubwa duniani kama pale umemfanyia mtu kosa na yeye anajua kuwa umemfanyia kosa lakini anakaa kimya hakuulizi wala halalamiki, ki ukweli inaogopesha sana. Lowassa anaaminika nchini kwakuwa mtu asiyeongea sana lakini huwa anakuwa na mikakati mikubwa sana, sisi wana CCM tunamfahamu fika kwakuwa tumekaa nae miaka mingi sana na alikuwa akishiriki katika mikakati mikubwa sana ndani ya chama.
Sasa tokea matokeo yametoka huyu mtu amekuwa kimya anafanya lumumba hapakaliki kabisa, hatujui ni kitu anaenda kukifanya. Mashushu wezi wa taarifa wamekwamba kabisa kuja na taarifa inaonekana jambo analotaka kulifanya linapangwa kwa usiri mkubwa ili kuepusha taarifa kuvuja. Lowassa tunakushauri, rudi CCM tukae meza moja tuangalie ni wapi tulipotofautiana kisha tusawazishe maisha yaendelee.
Hata raisi mteule nina imani atakuwa hana amani kabisa anahofu isiyoelezeka. Lowassa, CCM ni nyumbani kwako. Uwe huru kurudi muda wowote ule ukijisikia, usimdharau mama yako aliyekuzaa sababu ya mwanamke changudoa uliyekutana nae barabarani. Pamoja na tofauti zilizojitokeza hapo nyuma ukweli ni kwamba wana CCM wengi tunakupenda na tunakuhitaji.
Tafadhali lowassa usikae kimya, unatuogopesha wana CCM.
Sasa tokea matokeo yametoka huyu mtu amekuwa kimya anafanya lumumba hapakaliki kabisa, hatujui ni kitu anaenda kukifanya. Mashushu wezi wa taarifa wamekwamba kabisa kuja na taarifa inaonekana jambo analotaka kulifanya linapangwa kwa usiri mkubwa ili kuepusha taarifa kuvuja. Lowassa tunakushauri, rudi CCM tukae meza moja tuangalie ni wapi tulipotofautiana kisha tusawazishe maisha yaendelee.
Hata raisi mteule nina imani atakuwa hana amani kabisa anahofu isiyoelezeka. Lowassa, CCM ni nyumbani kwako. Uwe huru kurudi muda wowote ule ukijisikia, usimdharau mama yako aliyekuzaa sababu ya mwanamke changudoa uliyekutana nae barabarani. Pamoja na tofauti zilizojitokeza hapo nyuma ukweli ni kwamba wana CCM wengi tunakupenda na tunakuhitaji.
Tafadhali lowassa usikae kimya, unatuogopesha wana CCM.