Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,344
- 9,845
Wadau tukubali tu kwamba katika Mambo mageni tuliyoona kwenye wakati huu ni nguvu na ukubwa wa sauti ya Ukimya wa Lowasa.
Nimejaribu kupitia mabandiko mengi hapa JF na ninaona mengi ni malalamiko au matokeo ya wasiwasi wa ukimya wa Lowasa.
Magufuli ameanza kwa kasi ya ajabu bila kujali uelekeo ili kujaribu kuzima makali ya sauti ya ukimya wa Lowassa.Anatamaani sana Lowasa asahaulike mapema ili apate nafasi ya kujenga jina lake na labda umaarufu wake mwenyewe.
Kwa bahati mbaya kila anachofanya kinaongeza kumbukumbu na ukubwa wa sauti ya Ukimya wa Lowasa.
Wamejitokeza wana CCM humu wanaomshambulia Mbowe,wanamshambulia Mbatia,wanakishambulia CHADEMA na vyama vya ukawa,wanachokoa kwa kijiti wapate majibu.Watu kama Juliana Shonza na Faiza walioumizwa na Ukimya wa Lowasa.
Ni dhahiri sasa taifa limetega sikio,liko makini kiasi kwamba hata sindano ikianguka linasikia,lina kiu na sauti ya mtu mmoja tu, Linateseka kwa ukimya wake,linataka kumsikia Ndugu Edward Ngoyae Lowasa.
Mihemko ya kisiasa inayoongelewa na vyombo vya usalama ni mawimbi tu ya Ukubwa wa sauti ya ukimya, intelijensia inaumizwa na ukimya.Naanza kuipenda falsafa hii ya ukimya.
Ila kama mdau tu wa UKAWA na mwanachama wa kawaida kwenye chama changu nitumie fursa hii kumuomba Ndugu Edward Ngoyae Lowassa aongee kitu, Taifa linaumia.
Nimejaribu kupitia mabandiko mengi hapa JF na ninaona mengi ni malalamiko au matokeo ya wasiwasi wa ukimya wa Lowasa.
Magufuli ameanza kwa kasi ya ajabu bila kujali uelekeo ili kujaribu kuzima makali ya sauti ya ukimya wa Lowassa.Anatamaani sana Lowasa asahaulike mapema ili apate nafasi ya kujenga jina lake na labda umaarufu wake mwenyewe.
Kwa bahati mbaya kila anachofanya kinaongeza kumbukumbu na ukubwa wa sauti ya Ukimya wa Lowasa.
Wamejitokeza wana CCM humu wanaomshambulia Mbowe,wanamshambulia Mbatia,wanakishambulia CHADEMA na vyama vya ukawa,wanachokoa kwa kijiti wapate majibu.Watu kama Juliana Shonza na Faiza walioumizwa na Ukimya wa Lowasa.
Ni dhahiri sasa taifa limetega sikio,liko makini kiasi kwamba hata sindano ikianguka linasikia,lina kiu na sauti ya mtu mmoja tu, Linateseka kwa ukimya wake,linataka kumsikia Ndugu Edward Ngoyae Lowasa.
Mihemko ya kisiasa inayoongelewa na vyombo vya usalama ni mawimbi tu ya Ukubwa wa sauti ya ukimya, intelijensia inaumizwa na ukimya.Naanza kuipenda falsafa hii ya ukimya.
Ila kama mdau tu wa UKAWA na mwanachama wa kawaida kwenye chama changu nitumie fursa hii kumuomba Ndugu Edward Ngoyae Lowassa aongee kitu, Taifa linaumia.