UZUSHI UKIMWI hausababishwi na HIV, kwamba agenda nzima ni scam na kuwa hakuna kipimo cha kupima HIV bali vilivyopo hupima tu kushuka kwa kinga

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Peace be upon ya' all,

Hili swala limezua mjadala wa mda mrefu sana baina ya madaktari wao kwa wao wakivutana kwa hoja kuntu kabisa.

CC58F940-6D96-41BE-8159-AAC97B1C2286.jpeg


Je ni kweli UKIMWI hausababishwi na HIV kwamba agenda nzima ni scam na kuwa hakuna kipimo cha kupima HIV bali vilivyopo hupima tu kushuka kwa kinga?
 
Tunachokijua
HIV ama Human Immunodeficiency Virus ni kirusi kinachoshambulia mfumo wa kinga mwili, ambacho baada kuishi mwilini kwa kipindi fulani kinaweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini (UKIMWI)

Sio kila mwenye HIV hupata UKIMWI kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupata matibabu ya mapema. Pia, UKIMWI ni hatua ya mwisho kabisa anayopata mtu aliyeshambuliwa na HIV ambayo huonesha kuwa mfumo wa kinga umeshambuliwa vya kutosha, kiasi cha kuwa dhaifu na kuishiwa uwezo wa kutoa kinga kwa mwili.

Ili mtu mwenye HIV aweze kuchukuliwa kama tayari kapata UKIMWI anapaswa kuwa na nakala za seli hai nyeupe aina ya CD4 chini ya 200 kwa kila millimeter cubic ya damu (200 cells/mm3).

Pia, anaweza kuwa na hali hii ikiwa mwili wake tayari utaanza kushambuliwa na magonjwa mengine nyemelezi yanayoendana na maambukizi haya. Pamoja na machapisho mengine, Unaweza kutumia What Are HIV and AIDS? Kama rejea.

Hivyo, kujibu sehemu ya kwanza ya swali, JamiiForums inathibitisha kuwa ni kweli kuwa HIV husababisha UKIMWI. Tunapaswa kufahamu kuwa UKIMWI sio kitu cha ajabu, isipokuwa ni Upungufu wa Kinga Mwilini, jambo ambalo husababishwa na kudhoofika kwa mfumo wa kinga za mwili.

Sehemu ya pili ya swali inahoji juu ya uwepo wa kipimo kinachoweza kupima HIV, kuwa kwa sasa hakuna kipimo cha HIV, kinachopimwa ni uthabiti wa kinga pekee na siyo virusi wenyewe.

Ndugu msomaji, ni muhimu kukufahamisha kuwa hadi sasa kuna walau vipimo vitatu vya kuutambua ugonjwa huu.
  1. Antibody tests
  2. Antigen/antibody tests
  3. Nucleic acid tests (NAT)
Antibody ni kinga mwili zinazotengenezwa baada ya kushambuliwa na vimelea vya magonjwa ambavyo kwa hapa ni virusi, na antigen ndiyo kirusi chenyewe. Vipimo viwili vya mwanzo kwa kiasi kikubwa huchunguza kingamwili zilizozalishwa na virusi pamoja na antigen inayoitwa p24 ambayo huwepo mwilini ikiwa utakuwa na HIV.

Kipimo cha mwisho ambacho ni Nucleic Acid Test (NAT) huangalia na kuthibitisha uwepo wa HIV, pamoja na kubaini idadi ya nakala zake halisi kwenye damu. Unaweza kutumia CDC kama rejea.

JamiiForms imezungumza wa wataalam wa afya, na kwa kurejea taarifa hizi inasisitiza kuwa madai ya kutokuwepo kwa kipimo kinachoweza kugundua uwepo wa virusi kwenye damu pamoja na idadi ya nakala zake sio ya kweli.

Pia, sio sahihi kusema kuwa harakati zote zilizo nyuma ya gonjwa hili ni “Scam” kwa kuwa tunashuhudia watu wengi wakiugua na kupoteza maisha kila mwaka.
Peace be upon ya' all,

Hili swala limezua mjadala wa mda mrefu sana baina ya madaktari wao kwa wao wakivutana kwa hoja kuntu kabisa.

View attachment 2422564

Je ni kweli UKIMWI hausababishwi na HIV kwamba agenda nzima ni scam na kuwa hakuna kipimo cha kupima HIV bali vilivyopo hupima tu kushuka kwa kinga?
Kwani hao hao madaktari, haswa hao wa upasuaji na vidonda ikiwa ana mashaka na huduma aliyo toa kwa mteja, kuna dawa wanapewa za kujizuia na hilo jinamizi! Kama ni scam walikua wanazinywa na nini au hua zinawakinga na nini
 
Ni kweli UKIMWI husababishwa na HIV .

HIV inapoingia mwilini hupambana na CD4 yaani Kinga ya mwili.

Kinga ya mwili hutengengeneza antibody za HIV ambazo ndizo tunazopima ili kujua kama mteja yuko na maambukizi kwa kutumia kipimk cha SD BIOLINE.

kama kipimo kikisoma negative mtu anakuwa hana HIV,kikisoma positive tuna comfirm ķwa UNIGOLD ambayo husoma protein za HIV ikisoma positive maana yake mteja amepata maambukiźo.

Lakinj kadiri mteja anavyozidi kutumia dawa huwa kuna vipimo tunachukua ambavyo ni
1.HVL (Kuangalia wingi wa virusi)
2.CD4 count (kuangalia wingi wa kinga ya mwili).

Hivyo HIV/AIDS siyo scam lakini ni ugonjwa mpana unahitaji utulivu kuuelewa.

UKIMWI-upungufu wa kinga mwilini unapelekewa na HIV na ndiyo maana dawa zinatumika kufubaza ugali wa virusi,virusi wakufubaa kinga ya mwili hupanda na mtu kupata Ahueni.

Sijui kama Andiko limekusaidia.

UKIMWI upo na unawapata maelfu kila siku,vijana kuweni makini sana.
 
Habari ya asaivi,nilitaka kuuliza hivi mtu ambaye amefanya mapenzi na binti ambaye hamujui kuwa ana ukimwi au Hana akaja kushituka kuwa anaweza akawa ameambukizwa akaanza kutumia dawa za pep baada tasiku 6 hizo dawa zinaweza kumusaidia kwakiasi gani kukinga maambukizi ya VVU ?
 
Habari ya asaivi,nilitaka kuuliza hivi mtu ambaye amefanya mapenzi na binti ambaye hamujui kuwa ana ukimwi au Hana akaja kushituka kuwa anaweza akawa ameambukizwa akaanza kutumia dawa za pep baada tasiku 6 hizo dawa zinaweza kumusaidia kwakiasi gani kukinga maambukizi ya VVU ?

Ngoja tusubiri watalaamu waje, lakini kwa akili ya kawaida hili ni sawa na kufanya maombi ya kazi nje ya muda ulioruhusiwa.

Mwifwa
 
Habari ya asaivi,nilitaka kuuliza hivi mtu ambaye amefanya mapenzi na binti ambaye hamujui kuwa ana ukimwi au Hana akaja kushituka kuwa anaweza akawa ameambukizwa akaanza kutumia dawa za pep baada tasiku 6 hizo dawa zinaweza kumusaidia kwakiasi gani kukinga maambukizi ya VVU ?
PEP zitakusaidia ndani ya 72 hrs only otherwise sory
 
Habari ya asaivi,nilitaka kuuliza hivi mtu ambaye amefanya mapenzi na binti ambaye hamujui kuwa ana ukimwi au Hana akaja kushituka kuwa anaweza akawa ameambukizwa akaanza kutumia dawa za pep baada tasiku 6 hizo dawa zinaweza kumusaidia kwakiasi gani kukinga maambukizi ya VVU ?
kama binti huyo mwenye maambikizi ya VVU anatumia dawa kwa usahihi hawzi kuambukiza lakini pia ni vizuri ukatumia kinga pale unapokutana na mtu usiyemjua au ambaye hjafanya naye vipimo ili kujilinda dhidi ya jinamizi hili
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom