Ukimpata mke wa aina hii utafanyaje

Ukimpata mke wa aina hii utafanyaje

Mung Chris

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2017
Posts
3,473
Reaction score
4,007
Wana Jamvi,

Mfao umempata mke umeoa hajawahi kwambia kuwa huwa hali KUKU, MAHARAGE, SAMAKI, DAGAA NA NYANYA CHUNGU. anasema akila anawashwa mwili mzima na kutapika hapo hapo hata harufu ya hivyo akiisikia tu anaanza kusikia kichefuchefu. utafanyaje ukizingatia ndio mmeshafunga ndoa. hii inamaana kuwa hawezi kupika vyakula hivyo akikupikia basi ile harufu tu inamdhuru.

unafanyaje hapo (ulimpeleka hospitali imeshindikana, wamempa dawa za allergy bado tatizo liko palepale).

chicken.jpg
beans2.jpg
dagaa.jpg
fish.jpg
 
Inawezekana vipi?. Yaani mmeanza date, mmeingia kwenye uhusiano then uchumba finally ndoa kitu kidogo hivyo unashindwa nini kujua?
Unataka kusema kwamba mlikuwa hamtoani out? Hamtembeleani?
Au umeandikaje andikaje?
 
Inawezekana vipi?. Yaani mmeanza date, mmeingia kwenye uhusiano then uchumba finally ndoa kitu kidogo hivyo unashindwa nini kujua?
Unataka kusema kwamba mlikuwa hamtoani out? Hamtembeleani?
Au umeandikaje andikaje?
Anaficha yote usiyajue mkitoka out anaagiza keki soda au wali nyama ukimwambia kuku hataki anasema wanakula sana kwao si unajua tena maana anahisi ni kigezo kinaweza kukatisha tamaa usimchukue, basi yakawa hivyo
 
Depal kwani mdada akikwambia hamna kugegedana mpaka muoane ndio utamjua mwanaume si huwa ni mvumilivu siku ya siku unaingia kwa mara ya kwanza unakutana na usichokipenda unafanyaje mfano ndio kama hivi
 
Kwani yale maneno ya kasisi.... 'katika taabu na raha, magonjwa na afya.....umeshayasahau?
ndio yapo na kila mtu anayajua maisha yako ni kwamba hutaendelea kula vyakula hivyo maana utamuudhi sana mkeo
 
Wana Jamvi,

Mfao umempata mke umeoa hajawahi kwambia kuwa huwa hali KUKU, MAHARAGE, SAMAKI, DAGAA NA NYANYA CHUNGU. anasema akila anawashwa mwili mzima na kutapika hapo hapo hata harufu ya hivyo akiisikia tu anaanza kusikia kichefuchefu. utafanyaje ukizingatia ndio mmeshafunga ndoa. hii inamaana kuwa hawezi kupika vyakula hivyo akikupikia basi ile harufu tu inamdhuru.

unafanyaje hapo (ulimpeleka hospitali imeshindikana, wamempa dawa za allergy bado tatizo liko palepale).

Mpe 7800 achape lapa, yaani nikutane na kuku hotelini!!!! No, ili kuepusha migoro ambayo itanipa stress baadae, tuachane tu
 
Mpe 7800 achape lapa, yaani nikutane na kuku hotelini!!!! No, ili kuepusha migoro ambayo itanipa stress baadae, tuachane tu
Ni chakula kipi hapo au vingapi kama hali utavumilia kutotumia au kupikiwa nyumbani maisha
 
Kiafrika unaoa mwingine wanakuwa wawili..
huyo anakuwa kama mke mgonjwa...
Na akiwa hazai au kabahatika kumzaa mtoto mmoja tu unafanyaje unamkataa unamtafuta anayezaa sio kuvumiliana eti
 
Mkuu amka ..toka ndotoni. Utakua unaota.
 
Chunguzaneni kabla ya tendo takatifu la ndoa..
 
Na akiwa hazai au kabahatika kumzaa mtoto mmoja tu unafanyaje unamkataa unamtafuta anayezaa sio kuvumiliana eti

Wewe ukiwa husimamishi yeye atakuvumilia? ndugu zake watamshauri akuvumilie?
 
Marehemu Rais wa Zimbabwe alipokutana na Sally ambaye ni mke wa kwanza walizaa mtoto mmoja, mtoto huyo akafa badae alishindwa kuzaa kutokana na tatizo la Ini,lilimsumbua sana, Mugabe akasema Mama yangu mzazi ananisumbua sana anahitaji kuona wajukuu anasema hataki kufa kabla hajaona wajukuu, ndugu zake vile vile walimsema sana ndio ikabidi aanzishe mahusiano na aliye kuwa naye wakazaa watoto je unafikiri maamuzi hayo yalikuwa sahihi kusikiliza upande wa pili na kuutekeleza. mkeo anaweza akaenda ukweli kwake akaambiwa aandae chakula kama hicho ikawa ngumu unadhani wakwe zake watasemaje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom