Ukijiamini haupati Maradhi

Ukijiamini haupati Maradhi

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,543
Reaction score
21,551
Hiyo ilikuwa ni kauli ya mwamba mmoja ambaye nimekutana nae asubuhi hii Kwa mama lishe.

Kwa kawaida mwandishi yoyote Yule huwa anaandika kutokana na mambo anayokutana nayo kila siku, mwengine huandika kutokana na uzoefu wa Maisha yake na mwengine huandika story za kutunga kama hadthi, Ila Mimi mara nyingi huandika kutokana na matukio ambayo huwa nakutana nayo katika Maisha.

Sasa Leo asubuhi nikiwa napata chai Kwa mama lishe, mara paap kuna mwamba akaja kukaa katika meza niliyo kaa Mimi, baada ya kuagiza chai yake na chapati kama tano na maharage, akaambiwa na mama lishe maji ya kunawa yapo pale, mwamba akasema haina haja ya kunawa kwani anajiamini yupo Safi.

Ndio nami ikabidi nishiriki Yale mazungumzo, nikamwambia mwamba " lakini unajua kunawa ni muhimu Sana kwani mikono yetu inashika mambo mengi Sana" mwamba akasema "ukijiamini haupati Maradhi"

Nikiwa katika Hali ya kupatwa na mshangao juu ya kauli ya jamaa, ikabidi nimuulize tena Yule mwamba "ulipokuja hapa vipi umepanda daladala?" Akajibu ndio, nikaendelea kumwambia mkuu umeshika viti na bomba katika daladala kila mtu anashika pale uwezekano WA kuacha bacteria wanao sababisha maradhi mbali mbali ni Mkubwa mno hivyo kunawa ni Jambo la msingi Sana.

Mwamba huku akianza kukuta chapati yake Bila kunawa akasisitiza kwakusema Sisi ngozi nyeusi tupo imara Sana ni wazungu Tu wanatudanganya na Mimi najiamini Sana na unajua ukijiamini haupati Maradhi kabisa.

Huyu mwamba nilimkubali Kwa kujiamini na kusimamia misimamo yake ingawa Kwa upande mwengine sikumkubali Kwa kulichukulia Jambo la afya kimchezo mchezo, sijui alipata wapi hiyo elimu ya afya ambayo inamwambia akijiamini basi hapati maradhi.

Je, ni huenda kwa kuwa na watu kama hawa ndio kumefanya COVID 19 isituchape Sana wabongo coz ilijua hatuiogopi hivyo ikaamua kupunguza makali yake? Au ni kweli Sisi waafrika tuna ngozi ngumu?

Baada ya kumaliza kifungua kinywa changu nikaondoka na kumwacha Yule mcuba akiendelea kupata chai yake taratibu Bila wasi wasi wowote ule.

Ni hayo Tu!
 
Sometimes yes sometimes no. Vuta picha maisha ya bush hawana maji kule maji ni hanasa wanakula bila kunawa wala kuoga maji ya kunywa ya mtoni machafu n mtoto ana immunity balaa azingui magonjwa sasa ww wa mjini gusa km wao uone, lifestyle la mtu inategemea na antibodies antigens high immunity mtu wa Afya atajazia kwa undani zaidi
 
BECOMING SUPERNATURAL, soma hiko kitabu kuna full madini....humo unaweza kujiponya maradhi ya kila namna, kupunguza uzee na kuondoa kabisa tatizo la nguvu za kiume nk
 
Sometimes yes sometimes no vuta picha maisha ya bush hawana maji kule maji ni hanasa wanakula bila kunawa wala kuoga maji ya kunywa ya mtoni machafu n mtoto ana immunity balaa azingui magonjwa sasa ww wa mjini gusa km wao uone, lifestyle la mtu inategemea na antibodies antigens high immunity mtu wa Afya atajazia kwa undani zaidi
Nakubalia na wewe mkuu

Na jamaa kiasi Fulani yupo sahihi,Kwa mfano kijijini utakuta wanakunywa maji ambayo na ng'ombe wanakunywa pale pale na freesh Tu wapo vizuri Ila Mimi na wewe tunakuwa na Shaka na maji Yale,na kweli tukinywa Tu yanaamka mambo mengine kabisa

Hatar Sana!
 
BECOMING SUPERNATURAL, soma hiko kitabu kuna full madini....humo unaweza kujiponya maradhi ya kila namna, kupunguza uzee na kuondoa kabisa tatizo la nguvu za kiume nk
Uishi Maisha marefu mkuu

Maoni yako yatazingatiwa!
 
Hiyo ilikuwa ni kauli ya mwamba mmoja ambaye nimekutana nae asubuhi hii Kwa mama lishe.

Kwa kawaida mwandishi yoyote Yule huwa anaandika kutokana na mambo anayokutana nayo kila siku, mwengine huandika kutokana na uzoefu wa Maisha yake na mwengine huandika story za kutunga kama hadthi, Ila Mimi mara nyingi huandika kutokana na matukio ambayo huwa nakutana nayo katika Maisha.

Sasa Leo asubuhi nikiwa napata chai Kwa mama lishe, mara paap kuna mwamba akaja kukaa katika meza niliyo kaa Mimi, baada ya kuagiza chai yake na chapati kama tano na maharage, akaambiwa na mama lishe maji ya kunawa yapo pale, mwamba akasema haina haja ya kunawa kwani anajiamini yupo Safi.

Ndio nami ikabidi nishiriki Yale mazungumzo, nikamwambia mwamba " lakini unajua kunawa ni muhimu Sana kwani mikono yetu inashika mambo mengi Sana" mwamba akasema "ukijiamini haupati Maradhi"

Nikiwa katika Hali ya kupatwa na mshangao juu ya kauli ya jamaa, ikabidi nimuulize tena Yule mwamba "ulipokuja hapa vipi umepanda daladala?" Akajibu ndio, nikaendelea kumwambia mkuu umeshika viti na bomba katika daladala kila mtu anashika pale uwezekano WA kuacha bacteria wanao sababisha maradhi mbali mbali ni Mkubwa mno hivyo kunawa ni Jambo la msingi Sana.

Mwamba huku akianza kukuta chapati yake Bila kunawa akasisitiza kwakusema Sisi ngozi nyeusi tupo imara Sana ni wazungu Tu wanatudanganya na Mimi najiamini Sana na unajua ukijiamini haupati Maradhi kabisa.

Huyu mwamba nilimkubali Kwa kujiamini na kusimamia misimamo yake ingawa Kwa upande mwengine sikumkubali Kwa kulichukulia Jambo la afya kimchezo mchezo, sijui alipata wapi hiyo elimu ya afya ambayo inamwambia akijiamini basi hapati maradhi.

Je, ni huenda kwa kuwa na watu kama hawa ndio kumefanya COVID 19 isituchape Sana wabongo coz ilijua hatuigopi hivyo ikaamua kupunguza makali yake? Au ni kweli Sisi waafrika tuna ngozi ngumu?

Baada ya kumaliza kifungua kinywa changu nikaondoka na kumwacha Yule mcuba akiendelea kupata chai yake taratibu Bila wasi wasi wowote ule.

Ni hayo Tu!
😁😁😁😁 oi ungempiga ofa ya chapati mbili nyingine kwa masharti anawe mikono alafu ungetazma mtazamo wake ukoje baada ya ofa
 
Mkuu
Kuna mazingira ambayo kuwa msafi sana kwa muda mrefu ni hatari. Mwili hauwezi tengeneza kinga halisi kama haushambuliwi.
Mkuu kauli yako kama inaingia halafu inakataa

Tafadhali tufungulie code kidogo

Wanakati unafikilia uwezekano WA kufungua au laa!

Kuna tafiti moja inasema kuoga kila siku sio lazima,,hatar Sana!
 
😁😁😁😁 oi ungempiga ofa ya chapati mbili nyingine kwa masharti anawe mikono alafu ungetazma mtazamo wake ukoje baada ya ofa
Mkuu

Yule mwamba yupo serious Sana,hawakawii kunivunjia heshima hahaha
 
kile unachokiwaza ndio kinachokutokea ukiwaza kuumwa utaumwa ukiwaza kuwa na afya nzuri hautaumwa Cha kushangaza unakuta mtu kaandaa budget ya mambo yake mbalimbali alafu ameweka na budget ya kuumwa akiwa na Maana ni kitu Cha kawaida lazima aumwe unajichuliaa na utaumwa tu ni sàwa na kuchimba kabuli alafu uliache wazi umechimba la nini sasa?
 
Mkuu
Mkuu kauli yako kama inaingia halafu inakataa

Tafadhali tufungulie code kidogo

Wanakati unafikilia uwezekano WA kufungua au laa!

Kuna tafiti moja inasema kuoga kila siku sio lazima,,hatar Sana!
Kuna tafiti moja inasema kuoga kila siku sio lazima,,hatar Sana!

nimewahi kuweka uzi humu kuhusu kuoga, sio lazima kuoga kila siku nilishambuliwa balaa!
 
Mzee wa Mbususu Mzabzab ataunga mkono hyo sentensi ya huyo jamaa

Kuna watu ni wazinzi hatari na kuna muda huwa hawatumii ndomu lakin hawana ngoma huwa nashangaa sjui inawezekanaje

Kwa africa bacteria ni wengi sana kula bila kunawa ni hatari sana bora kwa wenzetu huko bacteria sio sana huko hata ukila bila kunawa ni fresh tu
 
Back
Top Bottom