Ukiijua hii Saikolojia na tabia ya Askari Polisi, hawatakusumbua sana

Sema askari Wetu wanavyo penda kujaribu nguvu zao kwa raia ni noma yaani unaweza ukawa mpole nabado ukala kipondo
 
Inaonekana huyu anayewakojolea hawamuoni kwa sababu ya hizo ngao


Wakimtia mbaroni lazima tu atajinyea
 
walimdandia kijana wangu nilimuagiza sehemu ni mizigo haikua na risit lilikua bonge la furushi ila in real life thaman yake ilikua haifik 50k majamaa yakajua apa ulaji dogo akanipigia simu nikaomba kuongea na afande mmoja nilimkoromea akawa mdogo mixa kumuuliza jina lake na number yake nilivoenda sasa kuonana nao nikakuta mnyama kawaalika wenzie waje wampige tough maana ule mkwara ulikua beyond his level walivoniona tu wakaanza kucheka yaan uyu chalii ndio kutia jamba jamba nikatumia mbinu tajwa hapo juu maana jamaa walikua na SMG bullet proofs helmets mabut ma kinga ugoko nikajidai pimbi miksa kucheka cheka kuapologize kila kitu kuwaita bro wakaniachia kiroho safi miksa kuuliza wakitaji hayo mazaga ninayo suply watapataje majamaa yanapenda ukuu
 
Jamaa wakipiga kinga ugoko ujue hali si shwari kabisa
 
Kweli inasaidia, lakini kwa Mwanaume kama wao kidogo ni mtihani kuweza kujishusha kiasi hicho.Na hasa ukiwa na akina Mama
ndani ya gari lako.
Pia hii tabia siyo dunia nzima.Kweli nchi kama Marekani mtizamo wako ni sahihi.Lakini mahali kama Uingereza tofauti sana.
 
Hii ni nzuri sana kama wewe ni mtu wa kujishusha, me sio mtu wa aina hiyo ila kuna siku nikiwa na gari ya kuazima natoka Mwanza naenda Igunga pale Usagara mbele kidogo nikasimamishwa na traffic mrembo wa kike, neno la kwanza kuongea " Habari dada mrembo, moyo wangu umepiga paah!
nikidhani nimekutana na malaika kumbe binadamu kama malaika pia wapo' hata leseni sikuombwa. Nilifanya hivyo sababu alikua mwanamke.
 
Yaani hawa jamaa ukikutana nao wewe kuwa Fala tu basi. Nishakutana na ngese zaidi ya 10 lakini jamaa hawachukui hata senti tano.
Kuwa humble, obey their orders jivishe sura ya upole uliopitiliza ==> ufala
Utasikia hebu ondoka !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe utakuwa askari na unatafuta nguvu...ASKARI WANA INFERIORITY COMPLEX na ndo maana unapowajibu au waelimisha wanakuja juu na kuona umewadharau.hivyo wanataka kutumia nguvu na vitisho. Askari kiakili ni weupe sana. Hawana SUPERIORITY COMPLEX YOYOTE NI SO WEAK AND INFERIOR NDO MAANA INABIDI WAWE WAKALI.
 
kuna mmoja tupo nae mtaani yupo poa sana hana mambo ya kipuuzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilishawahi kukamatwa askari nikiwa chuo huko DSM (nilikuwa na vijana wenzangu pale mtaani, kama watano hivi)
Walikuwa askari kama wanne wa kawaida, FFU wawili wakiwa full covered pamoja na mabaunsa watatu.

Hiyo siku, majira ya saa 3 asubuhi baada ya kupata chai, nikaamua kwenda kucheza pool table aisee!

Basi, game ya kwanza, ya pili, tatu... Muda unaenda tu, sasa nikawa nahisi kuna communication kichwani ikiniasa kuondoka eneo lile (hapa wakuu huwa nashindwa kujitambua nina kitu gani kichwani, hatari nyingi zinazonitokea huwa kuna nguvu inayonipa habari mda mchache kabla, nyingi huwa napuuzia, nyingine chache naziitikia na kujiokoa) lakini nikapuuzia!

Sasa ghafla aisee, nikajikuta naning'ining'ia juu pasipo kujielewa, kutazama nakutana na jitu refu sana lenye mwili uliojengeka haswa, mweusi ti!

Kuja kutahamaki najikuta ndani ya defender....Dah! Stori ndefu nisiwachoshe!

Baada ya kuswekwa humo na wenzangu, mimi nilijua hapa nikijifanya najua, mara.naongea sana, ntakufa kwa vipigo! Nikawa kiiimya, sikutaka hata kuwaangalia usoni wale jamaa!

Wale wenzangu wakaanza ubabe wa kiaina kama mnavyowajua wagogo na visu vyao! Aisee walikutana na kipondo kikali sana huku nashuhudia! Nikazidi kuwa mpole!

Askari mmoja akanigusa begani
"We dogo, mbona umejikunja hapo, huongei, unaumwa"?

...siumwi afande

" kwanini unacheza pool siku ya kazi"?

...afande Jmosi ni siku yetu ya kuwa free

(Afande akakaa kimya) hapo gari.lishaanza mwendo kuelekea kituoni, shekilango! Kichwani nikiwa nachakata mipango ya kujinasua na hili tatizo! Dah hatari sana

Tukafika Shekilango, nikaruka na.kuwa wa kwanza kutoka, nikasoma mazingira chap chap mle na kuona kuna selo 2. Moja ina watu kama 30, wako gizani hatari, kelele sana halafu vifua wazi! Nikaona humo ntakufa!

Ya pili iko na mzee mmoja, kijana mwingine halafu dirisha kubwa tu inaangalia barabarani.. Nikajisemea.hapa ndo naingia!!

(Nitarudi kumalizia)
Askari ni ndugu yako akiwa kitaa, akifika kituoni anakupita na kukuacha kwa wenzie wakuangamize
 
Mkuu msemee na hao wanawake uliokataa kumsemea ili tumpe marks zake.

Maana kimoja ulichokitaja katika mtungo wa 3w's na kugoma kutaja hicho kingine muhimu, unamkosesha marks za majaji wadau.

Maana hilo moja tu ulilolitaja halimuondoi kwenye sifa zao hizo za jadi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba unijibu.

Unaweza jua wanawake anaotembea nao baba yako?
 
mkuu tuwekee na audio mm nimejitahidi but nimeshindwa kabisa kumalizia kusoma, hakuna vituo kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…