Ukicheleweshwa mahali...umewahishwa mahali

Ukicheleweshwa mahali...umewahishwa mahali

kwakweli nimejifunza kitu kizuri sana afu kama umetugusa wengine hapa
asante mpenzi kiwatengu ni fundisho zuri kwetu pia
tutafika tu
 
Last edited by a moderator:
^^
Shukrani Ablessed nilijifunza mengi..kukubaliana na kuumana mioyo ni silaha njema katika maisha.
^^
Mungu awasaidie wale wote ambao bado hawajayaanza maisha ya ndoa wapate wenza bora. Na wale walio kwenye ndoa ngumu Mungu awape wepesi ili nao siku moja washuhudie kuwa kwenye ndoa ipo raha na wenye ndoa njema basi wamshukuru Mungu na wajue kuthamini walicho nacho.
 
Mungu aliamua kuwafuta machozi wote wawili, as mdau mmoja kasema the woman took a HUGE risk na nina imani alikuwa anaisikiliza sauti ya Mungu ndani yake na nina imani walimshirikisha Mungu katika kila hatua maana kwa vikwazo walivyopitia iliwalazimu kumlilia Mungu kwa maombi na hiyo ndio ilikuwa salama yao.

Wangekuwa watu wa kujirusha tu na starehe za duniani, shetani angetumia starehe hizo hizo (drinking, partying) kuwaseparate.

I love the couple, ila l have to admit kwamba sidhani mimi kaunga ningeweza kufanya kama huyo mama kwa nguvu zangu na ufahamu wangu bila msaada wa Roho Mtakatifu.
 
Mungu aliamua kuwafuta machozi wote wawili, as mdau mmoja kasema the woman took a HUGE risk na nina imani alikuwa anaisikiliza sauti ya Mungu ndani yake na nina imani walimshirikisha Mungu katika kila hatua maana kwa vikwazo walivyopitia iliwalazimu kumlilia Mungu kwa maombi na hiyo ndio ilikuwa salama yao.

Wangekuwa watu wa kujirusha tu na starehe za duniani, shetani angetumia starehe hizo hizo (drinking, partying) kuwaseparate.

I love the couple, ila l have to admit kwamba sidhani mimi kaunga ningeweza kufanya kama huyo mama kwa nguvu zangu na ufahamu wangu bila msaada wa Roho Mtakatifu.

Hivi umeokoka lini?....lol!
 
Tatizo letu wengi huwa tunatambua uwepo wa mungu pale tunapofanikiwa na tunaamini kuwa tusipofanikiwa kwa yale tunayoyapenda basi Mungu hayuko nasi, au kuna mkono wa mtu n.k. ukweli ni kuwa Mungu ni mwema na mwenye upendo na hivyo tunapokosa yale tuliyomuomba basi atakuwa anatafuta namna nzuri ya au kitu kizuri kisichokuwa na madhara nasi. Stay blessed.
 
^^
Nilialikwa kwenye tafrija fupi ya kuwapongeza wanandoa wawili.Wanandoa waliotimiza miaka 25 katika ndoa.Nilifika mapema sana,tafrijailikuwa inaanza saa 12,sitaki kutaja chakula,burudani na manjonjo yaliyokuwepo maana ntachokoza njaa za watu bure.
...
Kilichonipendeza ni namna wanandoa hawa walivyokuwa wamejawa tabasamu,faraja,na wakiwa wana matumaini mapya utadhani ndio kwanza wamefunga ndoa leo.
Lakini maneno yao machache juu ya simulizi zao yalijengwa juu ya neno moja 'haikuwa rahisi' Hilo halikunivutia kwani kila aliyekuwa ukumbini bila shaka alijua haikuwa rahisi.Kilichonivutia ni hichi
...
Namna walivyoingia katika ndoa.Mume alieleza namna alivyokutana na mkewe,alikuwa darasa la saba kamaliza,na mkewe alikuwa Mganga Mkuu wa wilaya.Binti ambae wakati huo anasema,alikwisha poteza tumaini la kuolewa.Alishazomewa akafika hatua akazoea,alishasimangwa akafika mahali akaona maneno ya watu hayaui.Walitueleza namna ndugu na jamaa walivyopinga uhusiano huu,walivyotengwa,na kwenda kuombewa kwa viongozi wa dini kuwa wamechanganyikiwa na walivyotishiwa radhi.Lakini kadri walivyopitia magumu ndivyo walivyopendana zaidi kiasi kuwa mke alimsomesha mume,hadi akawa Daktari kama yeye,wana watoto,majumba na kila ndugu akifika kwao hataki kurudi alikotoka
...
Nilijifunza mengi,lakini kubwa ni kuwa UKICHELEWESHWA MAHALI..UMEFIKISHWA MAHALI Mke alicheleweshwa ndoa lakini alifikishwa kwa mtu aliyemsitahili.Mume alicheleweshwa elimu lakini alifikishwa katika hekima na utaratibu
...
Kuna watu wamechelewa kupata wenza wao,lakini wamefikishwa katika darasa la subira,Kuna watu wamecheleweshwa kupata watoto lakini wamefikishwa katika somo la kuomba,Kuna watu wamecheleweshwa katika uchumba lakini wamefikishwa katika kujifunza ili wakimpata wajue thamani yake,Kuna watu wamecheleweshwa na mitazamo yao lakini wamefikishwa katika mitazamo.
...
Maisha yetu yote yana desturi ya kutuchelewesha Lakini tukikagua vizuri kuna mahali yametufikisha.
Hicho ndicho nilichojifunza.Waswahili wanasema Kizuri kula na umpendae.
Nimewaletea niwapendao MMU.
...
CC:
Queen Kan mimi49 Mentor Heaven on earth Mashaxizo Toria Lady doctor Munkari Nivea data lara 1 mwekundu Ablessed @FixedPoint Kaunga kiwatengu Mtambuzi UNDENIABLE Shine Swts Blue G GRAffan1

Soo touchıng!!! Yaan Mungu hua hachelewı wala hawaı, He ıs always ontıme!
 
Last edited by a moderator:
Tatizo letu wengi huwa tunatambua uwepo wa mungu pale tunapofanikiwa na tunaamini kuwa tusipofanikiwa kwa yale tunayoyapenda basi Mungu hayuko nasi, au kuna mkono wa mtu n.k. ukweli ni kuwa Mungu ni mwema na mwenye upendo na hivyo tunapokosa yale tuliyomuomba basi atakuwa anatafuta namna nzuri ya au kitu kizuri kisichokuwa na madhara nasi. Stay blessed.

^^
mwathu
Nimeipenda pia,be blessed too
cc: mito
^^
 
Last edited by a moderator:
Himidini this is soo touching,hope imebeba ujumbe mkubwa sana ambao kwa kweli utatusaidia katika maisha yetu ya kila siku yaliyojaa kila aina ya misukosuko na vivunja moyo,always tukumbuke huwezi kuwa na furaha sikuzote na wala huwezi kuwa na huzuni wakati wote tu Mungu yupo na kila mmoja wetu.asante mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom