Hussein Massanza
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 1,016
- 2,195
Nilisikiliza neno kwa neno hotuba ya Rais JPM huko Ukerewe.
Pamoja na mambo mengi aliyoyahutubia, naona habari ya mjini ni ishu ya kusema alimchagua Waziri Mpina kwa sababu naye ni kichaa kichaa kama yeye.
Kwanza, kiu ya siasa nchini ni dhahiri ipo juu sana. Watu wanatamani kufanya siasa za kejeli na propaganda kwa namna ile ile iliyozoeleka miaka ya nyuma. Hii kiu haitaisha, mpaka pale Rais atakapoamua kuruhusu mikutano ya kisiasa iendelee kwa mtindo uliozoeleka.
Pili, kauli ya ukichaa imechukuliwa out of context. Na ndivyo propaganda zilivyo. Kwa ambaye hakutazama hotuba nzima, ni rahisi kuchotwa na maneno yanayoendelea mtandaoni kwamba Rais 'amekiri' kuwa yeye ni kichaa na anaowateua nao ni vichaa.
Hata hivyo, Usahihi upo kwenye context, kwamba Rais alizungumzia ukichaa kumaanisha kiongozi mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi mapana ya taifa, akirejea uamuzi wake wa kukamata meli yenye samaki waliovuliwa kiharamu kipindi akiwa waziri wa Uvuvi.
Kama watu wanafanya utani, sawa. Lakini kama kuna wanaoipa uzito hiyo propaganda kwa kuiamini, nayo ni sawa tu. La muhimu, ieleweke kuwa ni propaganda.
Naamini Rais hawezi kupaniki kwenye hilo!
Pamoja na mambo mengi aliyoyahutubia, naona habari ya mjini ni ishu ya kusema alimchagua Waziri Mpina kwa sababu naye ni kichaa kichaa kama yeye.
Kwanza, kiu ya siasa nchini ni dhahiri ipo juu sana. Watu wanatamani kufanya siasa za kejeli na propaganda kwa namna ile ile iliyozoeleka miaka ya nyuma. Hii kiu haitaisha, mpaka pale Rais atakapoamua kuruhusu mikutano ya kisiasa iendelee kwa mtindo uliozoeleka.
Pili, kauli ya ukichaa imechukuliwa out of context. Na ndivyo propaganda zilivyo. Kwa ambaye hakutazama hotuba nzima, ni rahisi kuchotwa na maneno yanayoendelea mtandaoni kwamba Rais 'amekiri' kuwa yeye ni kichaa na anaowateua nao ni vichaa.
Hata hivyo, Usahihi upo kwenye context, kwamba Rais alizungumzia ukichaa kumaanisha kiongozi mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi mapana ya taifa, akirejea uamuzi wake wa kukamata meli yenye samaki waliovuliwa kiharamu kipindi akiwa waziri wa Uvuvi.
Kama watu wanafanya utani, sawa. Lakini kama kuna wanaoipa uzito hiyo propaganda kwa kuiamini, nayo ni sawa tu. La muhimu, ieleweke kuwa ni propaganda.
Naamini Rais hawezi kupaniki kwenye hilo!