Hii mbona ipo chini ya kiwango,utalipwa book 7 kweli?
wameamua lini? we akili yako kweli mbaya. kama unampenda wewe el mkaribishe nyumbani kwako akuongoze sisi oct 25 tunamchagua magufuli.Hata akibakia lowassa peke yake watz washaamua rais ni lowassa full stop.
Washapigwa asubuhi kama wataendelea na migogoro yao. Tatizo ni tamaa ndo inayowasumbua hawa viongozi, wanachama nao ndo fuata upepo, mbaya zaidi ukiwauliza kwa nini mzee hakuna jibu la msingi zaidi ya kutamka mabadiliko.
Samahani! hivi wewe ndio msemaji wa UKAWA!!??Kufuatia hali kuwa tete ndani ya kambi ya UKAWA, viongozi wa vyama vinavyounda umoja huo wanatarajia kukutana kwa dharura kesho kujadili mwenendo wa umoja wao.
Taarifa za ndani ya UKAWA zinasema Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ambaye yupo nchini Marekani atalazimika kurudi haraka nchini na inaelezwa huenda akaingia usiku huu au mapema kesho kwaajili ya kikao hicho cha dharura ambacho kitaamua hatma ya umoja huo.
Mbali na Mbowe, timu yote ya kampeni za mgombea urais na mgombea mwenyewe pamoja na mgombea mwenza wanatarajia kusitisha kampeni na kurudi Dar es Salaam kwa siku ya kesho hadi watakapopata mwafaka wa masuala yanayobishaniwa ndani ya umoja huo.
Taarifa zinasema, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa viongozi wa CUF kulalamikia kutotimizwa kwa makubaliano yaliyofikiwa wakati wanaungana na kupjnga jinsi Chadema wanavyoendesha umoja huo hadi kufikia hatua ya mgombea mwenza wa Chadema Juma Duni kutangaza kujitoa kwenye chama hicho na inaelezwa kikao hicho kitatumika kumuomba asijitoe.
CUF wanalalamikia UKAWA kuendeshwa na mtu mmoja ambaye ni Mbowe badala ya kuendeshwa kama taasisi na amekuwa akichukua maamuzi bila kushirikisha wengine.
"UKAWA ni Mbowe na yeye ndo anaendesha mambo anavyotaka kwa maslahi yake na mkwewe mzee Mtei. Huu ni uhuni ambao tulikuwa tunausikia tu ila leo tunajionea baada ya kuingia ndani" alisema kiongozi mmoja wa CUF ambaye alisisitiza kama Mbowe lengo lake lilikuwa ni kuua CUF amefanikiwa ila dhambi hiyo itamtafuna na watahakikisha Chadema haibaki salama.
Hivi ukawa niambieni hasa, kinachowaaminisha kuwa mshachukua nchi ni nini?
UKAWA KUWA NA KIKAO CHA DHARURA
Kufuatia hali kuwa tete ndani ya kambi ya UKAWA, viongozi wa vyama vinavyounda umoja huo wanatarajia kukutana kwa dharura kesho kujadili mwenendo wa umoja wao.
Taarifa za ndani ya UKAWA zinasema Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ambaye yupo nchini Marekani atalazimika kurudi haraka nchini na inaelezwa huenda akaingia usiku huu au mapema kesho kwaajili ya kikao hicho cha dharura ambacho kitaamua hatma ya umoja huo.
Mbali na Mbowe, timu yote ya kampeni za mgombea urais na mgombea mwenyewe pamoja na mgombea mwenza wanatarajia kusitisha kampeni na kurudi Dar es Salaam kwa siku ya kesho hadi watakapopata mwafaka wa masuala yanayobishaniwa ndani ya umoja huo.
Taarifa zinasema, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa viongozi wa CUF kulalamikia kutotimizwa kwa makubaliano yaliyofikiwa wakati wanaungana na kupjnga jinsi Chadema wanavyoendesha umoja huo hadi kufikia hatua ya mgombea mwenza wa Chadema Juma Duni kutangaza kujitoa kwenye chama hicho na inaelezwa kikao hicho kitatumika kumuomba asijitoe.
CUF wanalalamikia UKAWA kuendeshwa na mtu mmoja ambaye ni Mbowe badala ya kuendeshwa kama taasisi na amekuwa akichukua maamuzi bila kushirikisha wengine.
"UKAWA ni Mbowe na yeye ndo anaendesha mambo anavyotaka kwa maslahi yake na mkwewe mzee Mtei. Huu ni uhuni ambao tulikuwa tunausikia tu ila leo tunajionea baada ya kuingia ndani" alisema kiongozi mmoja wa CUF ambaye alisisitiza kama Mbowe lengo lake lilikuwa ni kuua CUF amefanikiwa ila dhambi hiyo itamtafuna na watahakikisha Chadema haibaki salama
Mbona makamanda viongozi wetu wanatuchanganya hivo, tuchukueni maamuzi magumunkama ni hivo, hawa jamaa wanataka kutubuluza.
Kila kona tunaambiwa migogoro, hali ni mbaya sana huku mitaani, wenzetu wanatucheka na kufurahia hii migogoro maana wanainchi hawatuamini tena.
Nilikwishasema kitambo sana, Ukawa ni mwamvuli unaowakilisha kampuni yenye maslahi kwa Chadema tu na vyama vingine vinasindikiza tu juhudi za Chadema kuingia Ikulu. Watu wameanza kushtuka. Hamjiulizi atakaemwongoza Lowassa ni nani.
Bahati nzuri, hilo linaeleweka na sisi tunaoona mbali.
Mnaanzisha uzi mnachangia wenyewe poleni eeeh