UKAWA tuache Kuzomea Wavaa Nguo za CCM

UKAWA tuache Kuzomea Wavaa Nguo za CCM

Pinda alisema sisi tupigwe je na sie tunaozomea ni nani mstaarabu hapo?
 
Inauma sana, eti nakula kiroba wakati me najigongea zangu bierre!!! kwa nini wasizomewe???
 
Wengi wao wanafanana na zomea zomea maana wengine wahuni na walevi ndo wanaona mahala pao ni huko,kuna haja ya kubadilika maana hiyo pia ni uchanga wa siasa na uelewa mdogo,mbona utawala wa siasa,mbona chama tawala sasa hakizomei ukawa,si ustaraab
 
Simnatuita Wanywa Viroba! Zomea Haooo Majiziiii Oooooooooo!

Wakikuzomea pia utakasirika.
Na hapo ndio mwanzo wa uvunjifu wa amani.

Sio lazima wote wawe na itikadi sawa na yako.

Jambo hili likiachiwa litaenea pia katika tofauti za kidini na kabila.
Katiba inazuia mtu yeyote kutukanwa, kudharauliwa au kubaguliwa kutokana na jinsi yake, dini, kabila au itikadi.

Huu ni ubaguzi mbaya unapaswa upingwe na wote katika CCM na UKAWA. Unarudisha nyuma dhana ya kuwa na vyama vingi vya siasa, uhuru wa kujumuika na kushusha hadhi ya utu.
 
Hatuwezi kuacha kuwazomea wanyonyajo na waji.nga wasiotaka mabadiliko..... Na tutandelea kuwazomea kwa sana
 
aisee minaona hakuna namna nyingine we umeambiwa ccm wamechoka unakaidi unavaa nguo zao hakuna jins uzomewe tuuuu!!!!
 
Wakikuzomea pia utakasirika.
Na hapo ndio mwanzo wa uvunjifu wa amani.

Sio lazima wote wawe na itikadi sawa na yako.

Jambo hili likiachiwa litaenea pia katika tofauti za kidini na kabila.
Katiba inazuia mtu yeyote kutukanwa, kudharauliwa au kubaguliwa kutokana na jinsi yake, dini, kabila au itikadi.

Huu ni ubaguzi mbaya unapaswa upingwe na wote katika CCM na UKAWA. Unarudisha nyuma dhana ya kuwa na vyama vingi vya siasa, uhuru wa kujumuika na kushusha hadhi ya utu.

nguo za ccm hazitakiwiiiii
 
My take: jambo muhimu na la msingi zaidi ya kuzomea ni kupiga kura kuondoa ccm madarakani 25/10/2015. Haya mengine ni sahihi ila si kila sahihi inafaa. Vyote ni vizuri ila si vyote vifaavyo. Tabia nzuri ni kutumia kura yako kwa uadilifu kuondoa ma ccm madarakani
 
Ccm Haikubaliki Hata Kwa Mungu
Unapozomea Ndiyo Wanajua Madhara Ya Ccm
 
Kwani Kuzomea Ni Kosa? Kuzomea Ni Kinyume Cha Kushangilia Je? Iweje Mtu Ufulahie Kushangiliwa Tu Inapogeuka Upande Wa Pili Uchukie?
 
Kwa kweli watu wanaozomea awatoi ujumbe wowote wa maana. Wanapozomea husikii neno lolote linalosemwa. Unapotaka kutoa ujumbe ni lazima uwasihi wazomeaji wanyamaze ili kupisha maneno ya busaa kutoka kwa wenye busara. Huwezi kuwakuta watu wastaarabu, kwenye mkutano wowote wa watu wastaraabu, au kanisani au hata jeshini wakizomea. Ukiwakuta genge la watu wanazomea au wanazomeana utajua kuwa genge hilo ni la wahuni.
CHADEMA kilioonekana na kukubalika kuwa chama cha upinzani makini na cha watu makini kwa sababu wamekuwa wakitoa hoja Bungeni na kwenye mikutano ya siasa. Sasa tabia ya zomea zomea inaletwa na kuenezwa na watu ambao pengine hata siyo wanachama wa CHADEMA. Zomea zomea ya mitaani itawafanya watu wengine makini waliokuwa wakikipenda chama hiki waamini kuwa ni cha cha wahuni hivyo kubadili maamuzi yao ya kutaka kujiunga nacho. Chama kiathriwa na tabia ya zomea zomea inayofanywa na wahuni ambao hata hawajajiandikisha na sio wanachama wa CHADEMA. Siku kura zisipotosha chama kitaamini kimeibiwa kura kumbe walidanganyika na watu wasiokuwa hata wanachama
 
hii inatufanya kutokua na imani kabsa na ukawa.jamaa hawa ni wahuni xana. cwez kutoa kura kwA watu wanaodhalilisha mama na dada zetu.
 
Jioni hii majira kama saa 12 hivi nimekaa nje ya nyumba napunga upepo, ghafla nikasikia mayowe, zomea zomea na makelele ya mwizi! Mwizi! mwizi! Mwizi huyo, huyooo. Nikaingia ndani na kujiandaa fasta kwa zama za maangamizi.
Kuja kutoka nakuta anayezomewa na kukimbizwa ni kada wa SISIEM limevaa kijani linatokea huko Diamond Jublee kumsikiliza Makufuli.
 
Na vyama vingine na wap wanapanga safu us zomeazomea,kitajachofuata ni Mapiganoooooooooo.
 
Back
Top Bottom