UKAWA sasa IKAWA?

UKAWA sasa IKAWA?

Hivi huyu ni Mwanakijiji yule yule ninayemfahamu au account yake imeingiliwa? Siamini kwani kwa sasa amekuwa mtu wa siasa nyepesi nyepesi sana. Hivi ni kweli Mwanakijiji hafahamu kilichopo nyuma ya hao viongozi wa NCCR?

Swali la msingi la kujiuliza ni hili, makubaliano ya mgawanyo wa majimbo haukufanyika leo, siku zote hao viongozi walikuwa wapi kupinga au kutoa maoni yao kuboresha makubaliano yaliyofikiwa na m/kiti na katibu wao mkuu?

Majimbo yamegawanywa kabla ya muda wa kurudisha form NEC tarehe 22/09/2015, watu wamechukua form zikajazwa na kurudishwa. Kampeni zinaelekea kumaliza mwezi sasa leo wao ndio watoke waseme kuwa hawaridhishwi na mgawanyo wa majimbo? Mtu mzima mwenye akili timamu unayekubaliana na mitazamo ya hovyo kama hii tukuelewe vipi?
 
Too low Mwanakijiji, kwani pilipili usioila yakuwashia nini?

Kura yangu ni mabadiliko.

mkuu ni kumbushe hivi mbatia ni msemaji wa chadema au ni mwanachama wa chama gani.
 
Mzee Mwanakijiji, kwa sasa habari ni moja tu kwanza. Kuing'oa CCM madarakani, jambo amblo limekuwa humu kwa miongo kadhaa.

Iking'oka badi hayo mengine yatakuwa mepesi kabisa. Kumbuka yalisemwa mengi kwamba wasingeweza kufika hapa waliko leo lakini ona wamefika.

Ikasemwa akiondoka fulani na fulani itakuwa na negative impact na UKAWA kusambaratika na wafuasi wake kugawanyika kwa kiasi kikubwa. Lakini ina wameonfoka wale lakini no one cares!

Maelezo yako hayatii watu moyo wakati wanakaribia au wanaelekea kupata ushindi bali yanavunja nguvu jambo ambalo linakuweka katika kundi la maadui.
 
Mafanikio ya CCM si kubadilisha maisha ya watanzania,ila kuvuruga muungano wa watanzania ili iwe rahisi kuwatawala...safari hii watashindwa tu...to hell CCM!
 
Ngamia anapokaribia kufa, huwa anarusha mateke ya hatari san. Hakuna cha ajabu sasa kuwaona hata ''makamanda'' wakisalimu amri. Too late though.
 
Sio muungano wa Kilaghai tuliutarajia wengi, sio muungano wa kusigina Democrasia, kwa hali ilivyo sasa utaita muungano au "Genge" no planning, no strategy, no leadership..no reasoning, no motive, no ambitions, no mission, no vision ni uhuni na utapeli wa hali ya Juu, Chadema ikishinda uchaguzi Tz itakua ni Nchi inayoongozwa na Majuha Duniani elewa katiba iliyopp niya 1977 hebu nipangieni Baraza la Mawaziri la hawa matapeli usinitajie Mnyika,Sugu, Nyerere, Mbowe,Msigwa, Lema etc hawana sifa zote za kua viongozi.

Zee lingine hili apa.
 
Hao wasomi wako wamesaidia nini for the past 54 years?
Wasomi style ya akina Kapuya, Kawambwa, Tibaijuka and the likes?
Hao uliowataja ni viongozi tena wanajitosheleza kabisa...na kama wakihitaji technical advice, wapo wasomi wanaojielewa kama akina Prof Baregu watasaidia kama wanavyosaidia sasa.

Nilikata tamaa Mbatia aliposema mnao wazoefu akawataja kina Mungai, Mgana, Masha, Mahanga na mimi nakuongezea Sumaye na Lowasa walioshiriki kwa takribani miaka 40 kati ya hiyo 54 ya uhuru.
 
Sio muungano wa Kilaghai tuliutarajia wengi, sio muungano wa kusigina Democrasia, kwa hali ilivyo sasa utaita muungano au "Genge" no planning, no strategy, no leadership..no reasoning, no motive, no ambitions, no mission, no vision ni uhuni na utapeli wa hali ya Juu, Chadema ikishinda uchaguzi Tz itakua ni Nchi inayoongozwa na Majuha Duniani elewa katiba iliyopp niya 1977 hebu nipangieni Baraza la Mawaziri la hawa matapeli usinitajie Mnyika,Sugu, Nyerere, Mbowe,Msigwa, Lema etc hawana sifa zote za kua viongozi.

Ww sifa unayo!
 
Wewe babu unahangaika tokea Eddo atue Chadema badala ya kujishughulisha na shughuli zako za kukosha vikongwe huko ugaibuni unafikiri utabadilisha watu kwa vithread vyako? endelea kutunga riwaya za mapenzi uwauzie na wakina babu slaa wajifunze kuishi na wake vizuri badala ya kutawaliwa

Kinachowaponza hamtaki kuelezwa ukweli.subiri baada ya oktoba utamwelewa mwanakijiji ambaye baadhi yenu mnasema anaishi ughaibuni wakati tuko nae huku uswahili.shame on you
 
Wewe babu unahangaika tokea Eddo atue Chadema badala ya kujishughulisha na shughuli zako za kukosha vikongwe huko ugaibuni unafikiri utabadilisha watu kwa vithread vyako? endelea kutunga riwaya za mapenzi uwauzie na wakina babu slaa wajifunze kuishi na wake vizuri badala ya kutawaliwa

Huyu jamaa anayejiita mwanakijiji hata sura yake hajawahi kuionyesha asituhangaishe .
 
Hahaha...huyu MM wa 2005, 2010 na 2015... kweli binadamu hasa sisi wa Afrika hata uishi Marekani miaka 50 bado tu utabaki kuwa na ubongo wa KIafrika.

unachosahau MM ni kwamba kwa sasa UKAWA hawana mamlaka au hawajashikilia gia ya mabadiliko, wanaohitaji mabadiliko haya ya kidemokrasia tena bila vurugu ni WaTanzania masikini wanaopata shida za CCM directly, ni Vijana wa Taifa hili ambao kwa sasa wamejua umasikini hausababishwi na Mungu bali sera mbovu na wezi wa serikalini, na wanamjua adui yao ni CCM maana ndie anaekua responsible...

Hata LOWASA akishindwa uchaguzi huu, bado haitaondoa idea ya kuhitaji mabadiliko vichwani mwetu...na wewe utakua sehemu ya Political Dinosaur ambao wamepoteza influence na heshima... unajificha kwenye kivuli cha "Taasisi" hata kufikia kusema wewe ni Institution mate wa Nyerere? haya ni matusi na sijui ni Nyerere yupi unamzungumzia.

Zile zama za 2005 ulipokua unaiunga mkono CCM na Kikwete tulikuwepo, na hata ulipoiunga mkono CHADEMA na UKAWA tulikuwepo, na hata sasa unapoiita DUBWASHA bado tupo...hii inaakisi wewe ni mtu wa namna gani, unayejificha katika vichaka na vivuli vinavyowaka moto...

Kile kidogo ulichobaki nacho hifadhi, kwa maana si muda utakua sawa na Lizaboni
 
Last edited by a moderator:
UKAWA.jpg


Dubwasha hili linaundwa na vyama vinne; vitatu kati ya hivyo ni vikubwa na vina historia ndefu tu ya upinzani Tanzania. Nimeliita "dubwasha" siyo kama kejeli bali ni kitu ambacho huwezi kukielezea kikaeleweka. SIyo chama, siyo muungano, siyo umoja ni ushirikiano tu fulani hivi ambao unataka kutuaminisha kuwa unataka kuja kuongoza Taifa. Kwa muda mrefu wapo watu ambao wameushabikia sana kiasi kwamba wanafikiria UKAWA ni kama chama cha siasa fulani hivi au kina mgombea au wagombea katika Uchaguzi. Kumbe UKAWA siyo chama cha siasa na hakina wala hakiwezi kuwa na Ilani, Sera, wagombea n.k.

Lakini ambacho kimethibitika mapema sasa na wengine tumeonya tangu kuundwa kwa hili dubwasha ni kuwa UKAWA unajiandaa kutuletea matatizo; tayari mengine tumeyaona na mengine yameashiriwa tu. Baada ya uongozi wa NCCR-Mageuzi nao kuja na kulalamikia dubwasha hili nimejikuta nikisema kuwa hili sasa siyo tena UKAWA bali ni IKAWA

UKAWA sasa imekuwa ni IKAWA! Vyama vitatu vinavyounda ushirikiano huu wenye mashaka tayari vimekuwa na matatizo na viongozi wao wajuu kisa UKAWA. Imekuwa hivyo kwa CHADEMA - na kuondoka kwa Dr. Slaa - Katibu Mkuu, CUF - kwa Prof. Lipumba (Mwenyekiti) na sasa NCCR-Mageuzi na malalamiko ya Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu kuhusiana na dubwasha hili.

Kimsingi sasa UKAWA imekuwa IKAWA kwani itakuwa ni shida nyingine ambayo hata hatujaifikiria sana; kwamba tayari vyama hivi vina migogoro ya ndani kuhusiana na ushiriki wao kwenye UKAWA na wengine kwa maamuzi ya kusimamisha wagombea mbalimbali. Ngoma yote itakuwa chungu pale baada ya Uchaguzi vyovyote itakavyokuwa - wakishinda CHADEMA na wagombea wake au wakishindwa kutakuwa na matokeo kwenye vyama hivi vikuu.

Fikiria kwa mbali tu ije itokee wajaribu kuunda Baraza la Mawaziri...!!!

Wanachama wa vyama hivi huko waliko nina uhakika wanaangalia kwa makini yanayoendelea kwenye vyama vyao; ukimya wao sidhani kama ni woga...

Na Itakuwa IKAWA kweli kweli...

NLD peke yao inaonekana ndio wamenufaika zaidi na dubwasha hili!

MMM

TOO LATE, TOO DESPERATE ! Bahati mbaya unadhani hatukuewi..... Ulituaminisha CCJ is the best party - hata kabla haijapata usajili. Ulitumia vigezo gani? Unachohofia UKAWA hakipo CCM? CCM leo hii raisi akichagua kiongozi yeyote wa ngazi lazima aangalie dini na kabila. Akichagua Muislamu, basi makamu mkristo, akichagua mkristo, makamu muislamu..hii ndo dubwasha unalolipenda. Mzee Mwanakijiji, tuambie lini CCM imegeuka nzuri na isiyo na mifarakano? Leo hii Waziri Mkuu kanuna, Makamu wa Raisi kanuna, Mshauri mkuu wa raisi kanuna...bado unataka kutuaminisha CCM wana umoja? We vipi Mkuu, au umefikia umri wa Mkapa kutojua nini uongee mbele ya kadamnasi? Spare UKAWA man, talk a balanced talk. Mbona huisemi CCM, umeng'atwa na kunguni nini?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom