UKAWA kutoingia bungeni-siri yafichuka

UKAWA kutoingia bungeni-siri yafichuka

Unajua historia ya ccm kuanzia TAA ilifanya mabadiliko mangapi hadi sasa? Mbona hata kama umesoma shule ya kata, hata macho huna? Kila kukicha serikali inatangaza mabadiliko. Kila leo ccm inatangaza mabadililko. Ni taasisi gani unayoijua isiyofanya mabadiliko?

Mabadiliko kama lengo lake ni kuboresha mifumo yanaubaya gani?

Kwa nini leo kikwete aliamua kuanzisha mchakato wa katiba mpya? Kwa nini katiba ibadilishwe?

Katiba iliyopo imefanyiwa mabadiliko kibao hadi imejaa viraka. Unadhani mabadiliko hayo yalifanyika kwa sababu walioona haja hiyo ni wajinga kuliko wewe?

Bunge hata sasa, linabadilisha kanuni kila kukicha, kwa mtazamo wako, huoni mantiki?

Sera za taifa na vipaumbele vinafanyiwa mabadiliko mara kwa mara na mipango ya maendeleo ya muda mrefu na muda mfupi inarekebishwa wewe kwa akili yako huoni hilo?

ccm imebadilisha kanuni zake mara ngapi? kushika hatamu, kujikosoa, kukorimba, kubambikiza, kujisafisha, ku Limboka, vifungo vya akina bibi titi, mohamed babu, vizuizi vya akina maalimu sharif hamad, kuua na kuchinja wapinzani, yote haya ni mabadiliko ya mikakati. Haijalishi walikuomba ruhusa wewe ama walikupa taaarifa. Haijalishi kama yanaathari chanya kwa kila mtu ama la. Lakini siku zote mabadiliko yapo.

Kwa nini hutaki CHADEMA wafanye mabadiliko? Unataka watu wote wawe na akili mgando kama wewe? Kwamba ukisikia kijiweni mwehu anasema chadema kila siku wanabadilisha mambo, unakariri na kupata hoja ya kutembelea? Angalau basi upelek vijiweni hoja hizo siyo hapa.

Unaelewa madhumuni ya kuwa na monitoring and evaluation entities kwenye programs?

Monitoring ina umuhimu gani kama kufanya marekebisho katika safari ni uovu?

Ukikaa kimya, hata kama ni m'p'mbavu------, utaonekana una hekima!. Ni afadhali kunyamaza kuliko kujidhalilisha kwako unakojianika hadharani. Wewe ulishahudhuria vikao vya CHADEMA ukaona unaburuzwa? Una ushauri gani wewe mbadala wenye tija na hadhi kuliko CHADEMA?

Kama umeshindwa hata kuona maana ya kuwa na katiba ya wananchi, ninachelea kusema, hufai kwa mijadala ya maendeleo ya taifa. Nyamaza ujifunze, au usubiri kufa, lakini huwezi kujiweka kuwa kigezo wote wakufuate wakati huna unalojua na una akili mgando na uelewa wa jalalani kuliko msukule.

Mi nalipwa na nani! tatizo lenu mnaburuzwa na Mbowe na mawazo ya wake zake. We kiongozi gani kila akiamka asubuhi anafanya amendment za kanuni za chama bila mkutano wowote! mara anabadili baraza kivuli! mara anashirikiana na huyu, mara yule simtaki! Vikao hivyo vya yeye kulala na kuota na hatimaye asubuhi (baada ya kushauriwa na madem wake) anakurupuka na kutoa maamuzi!
 
Wewe ulioleta thread unafikiria kwa kutumia ------ sio bure,yaani unalopokolopoka tu...kumbuka sio wote tuliopo humu ni kizazi cha mulugo na sera yake ya BRN,Kwa hiyo unapoleta maada lete na reference sio unaparamia tuu na kuandika kama mwendawazimu.......
 
Mi nalipwa na nani! tatizo lenu mnaburuzwa na Mbowe na mawazo ya wake zake. We kiongozi gani kila akiamka asubuhi anafanya amendment za kanuni za chama bila mkutano wowote! mara anabadili baraza kivuli! mara anashirikiana na huyu, mara yule simtaki! Vikao hivyo vya yeye kulala na kuota na hatimaye asubuhi (baada ya kushauriwa na madem wake) anakurupuka na kutoa maamuzi!

Kama vile mnavyoburuzwa na buku 7 za Nape hapo lumumba na matamko ya kuvua magamba, mawaziri mizigo halafu JK wenu anawapotezea
 
Kuna mropokaji mmoja aitwa Makondo jana kwenye kipindi cha Star Tv alisema huu upuuzi. Nilimwangalia nikamsikiliza sana nikajua CCM ni majuha kupindukia. Makondo ni Makondo tuu, hopeless creature.
 
Huu mtafaruku ni wa kutengeneza ,kuna engine wananufaika kwa namna moja ama nyingine
 
Kumbe kwa siku moja wasipoingia wanalipwa 450,000/= kudadadeki!

Nchi hii kumbe inaelekea kwenye shimo. Mtu wa aina hii hakustahili hata kujua kutumia kompyuta, sijui imekuwaje, lakini naamini ni wale waliopewa B+ za form iv hii ya div. 5.

Hebu angalia profile yake mtu huyu;

Join Date : 6th July 2014
Posts : 330
Rep Power : 370
Likes Received:53
Likes Given:0

Kwa siku 24 tangu kujiunga ameandika wastani wa meseji 13 kwa siku! NI kama kapewa ajila. Badala ya kujisomea arudie mitihani aliyofeli yeye ameona ni vizuri kushinda JF!
 
hujaweza kushawishi jukwaa kwa maneno yatima yasiyojulikana mama yake nani! jipange upya mheshmiwa
 
Madaraka mazuri. Wanaogopa kutupwa nje na kufa kifo cha mende, miguu juu.

Tatizo ninaloona mie ni pale chama tawala kinatafuta sababu za kitoto kuwalaghai wananchi. Hi shule wamesoma kweli. Walianza na udini, wakaja na ukanda sasa "wanapoke". Mwisho wa longolongo umewadia
 
Mbona hamsemi kalipwa na nani na kuweka ushahidi? Kusema sio kutuaminisha. Acheni cheap politics za kitoto.

walipaji wako wengi kwa masilahi tofauti tofauti wako wanje na ndani hivi wale wanaochukua laki tatu wanalipwa na nani? vile
 
Back
Top Bottom