Maana ya ukawa ni nini? Ni umoja wa katiba ya wananchi. Sasa umoja huu utasambaratika vipi kwa masuala ambayo yanaingizwa kwenye katiba kinyemela na CCM bila kushirikisha wananchi? CCM Ndio itasambaratika kwanza kwani wananchi wanajua Kwamba nchi yetu ilikuwa ni secular kwa miaka 50, kwa maana ya Kwamba haikuwa ikiongozwa kwa itikadi yoyote ya kidini. Cha kushangaza ni Kwamba baada ya CCM Kujenga sana hoja Kwamba kuna vyama vinajenga udini, hatimaye CCM imeamua kusimika suala Hilo Rasmi Liwe kwa Mujibu wa katiba. Hii itakuwa ni moja ya sababu kubwa ya katiba mpya kufeli kwenye kura ya maoni, hivyo to mark the beginning of the end of ccm's dynasty.
Sent from my iPhone using JamiiForums