change junior
Member
- Aug 11, 2014
- 42
- 7
Naona toka maandamano yatangazwe raia hawana mbwembwe kitaa.......wameshawazoea hamuwasumbui tena RAIA........
Ndugu, Unaemuona mfuasi kidampa lazima uelewe kuwa kwa CCM ana kura iliyosawa na wale ambao unawaona siyo wafuasi kidampa.Mkuu nchi nyingi zilizoishia kwenye machafuko ni kwa watawala kuupuuza umma. Ona nchi kama Siera Leon, Liberia na hata Kenya mambo yalikuwaje? Tatizo la hapa kwetu, viongozi wa chama Tawala kama wakina Nape wakiingia mitandaoni na kuona maoni ya wafuasi wao vidampa kama waliochangia hapa wanaona ni haki yao kuendelea na wakifanyacho. Wanasahau kwamba iwapo nchi itavurugika na kutokea machafuko wao viongozi ndio watakaowajibika kwenye mahakama za uhalifu wa kivita sio hawa wapiga debe wa JF na mitandao mingine.
Maridhiano ni jambo la muhimu sana kwani wote ni Watanzania kwa nini tufikie kugombana? Utakuta mume ni CUF au Chadema na mke ni CCM jee ni haki kweli kwa kuwa itikadi za kisiasa ni tofauti basi tutwangane?
Hebu watumie akili watuepushe na hizo dhahama pia waangalie nao wasiishie pabaya.
Sent from my iPad using JamiiForums
Ndugu, Unaemuona mfuasi kidampa lazima uelewe kuwa kwa CCM ana kura iliyosawa na wale ambao unawaona siyo wafuasi kidampa.
Maridhiano kuhusu Rasimu ya Katiba hayapatikani barabarani. Maridhiano kuhusu Rasimu ya Katiba yanapatikana ndani ya Bunge la Katiba.
Ukikimbia bunge, ina maana hata maridhiano utakuwa umeyakimbia.
Amani ya Tanzania inalindwa kama mboni ya jicho na serikali ya CCM, ndiyo maana taifa letu bado ni mfano wa kuigwa na nchi zingine Africa. Tutaendelea kuwa ni mfano wa kuigwa chini ya serikali ya CCM.
Tunawatakia kila la heri kitu cha maana ni ujumbe maalum katika mikutano si kutukana au kumwaga kashfa.Ningependa mikutano hiyo ilenge kuwajenga na kuwafunza waTanzania uchafu unaofanywa na bunge la posho huko mjini Dodoma.
Maandamano mpaka ikulu....mkuu, cybercrime kasema kweli, hivi unafikiri maandamano ya UKAWA yakiisha wataenda wapi tena?
Inakuwaje mnaandamana na watu wenye uhakika wa kula milo mitatu?
CHANZO: Mwananchi
NB Ikumbukwe JINI likitoka kwenye CHUPA huwa halirudi ndani ya CHUPA serikali 3 ni lazima sio ombi tena.
Tunayasubili maandamano kwa hama sana,ila tunawaomba viongozi wetu wa ukawa mtoe elimu zaidi kama walivyo fanya wajumbe wa iliyokuwa tume ya mabadiko ya katiba,maana kuna wengine hawakubatika kuona mdahalo ule.