UKAWA imeivuruga ACT - Mwigamba

UKAWA imeivuruga ACT - Mwigamba

Katibu Mkuu wa ACT Samson Mwigamba amekiri ujio wa Muungano wa UKAWA umevuruga malengo ya chama chake.

Mwigamba amesema lengo kubwa la chama chake ni kuwaunganisha wananchi na kuwaeleza ubovu wa chama kikuu cha upinzani nchini Chadema.

Mwigamba amesema hata hivyo kwa sasa Chadema iko katika ushirika na vyama vya CUF na NCCR chini ya mwamvuli wa UKAWA.Ameendelea kudai kwamba imekuwa vigumu kueleza uovu wa Chadema wananchi wakaulewa kwa sababu imetokea wananchi wanaiamini UKAWA na hawataki useme chochote kuhusu mshirika wa umoja huo.

Mwigamba hata hivyo amesema anaamini UKAWA utasambaratika kabla ya 2015.Na baada ya hapo ndipo wananchi wataelewa kuhusu vita ya ACT na Chadema.

Source:Sauti Huru.

Naomba muniambie Maana ya -------- na mjinga ili nijue lipi Nitumie hapa all together if the will meet my taget
 
Hiki ni chama cha madalali wa. Kisiasa kama vile vyama ambavyo dakika za mwisho nyakati za chaguzi wagombea wao wa urais utangaza kuiunga mkono ccm.

Hiki chama ni kagenge ka watu kwenda kufichia aibu zao za matakwa yao oVu ya kisiasa kushindwa.

Mwigamba anatutia aibu sana watu wa mkoa wa mara.
 
Haya pambana! Ila mwisho wa ubaya.....

Toa uchuro wako hapa,act imekufa kabla hata kipenga hakijapulizwa. Watz si wajinga kiasi hicho waunge mkono chama kilichoanzishwa kwa ufadhiri wa ccm! Kweli dhambi ya usaliti mbaya hadi Mwigamba anajisahau na kusema hadharani kuwa malengo ya act si kupambana na ccm ili ichukue dola bali kupambana na CDM kana kwamba Ndiyo yenye dola!
 
bora mwigamba angehamia tu ccm, huko anapoteza muda wake, hivi huwa hakumbuki CCK.CCJ walikujaje? sasa wapo wapi.
 
Huyu Mwigamba kachanganyikiwa, kinachowaumiza wananchi leo ni sera zinazo tutawala, sasa hao cdm ubaya wao utasaidia nini kwa wananchi wakati migodi inauzwa kodi haikusanywi, dhahabu inasafirishwa kwa matani lakini hakuna kodi zaidi ya peanut, ubaya wananchi wanaotaka kusikia ni jinsi nchi inavyoendeshwa kwa zengwe sio vita ya madaraka ndani ya vyama.
 
mimi naitetea haki kokote ninakoiona.Wewe je!
mnafki tu wewe,act wanapambana na cdm tu,hiyo unaona ni sawa?vyama vya upinzani lengo lao ni kukitoa chama tawala madarakani,sasa hawa wasaliti wanataka kupambana na cdm kwa faida ya ccm!and you think it's fine!tunajua mwigamba na kundi lake la wasaliti wanafadhiliwa na ccm from day one but that ain't gonna work.By the way,the last i checked you were a strong supporter of ccm and all of a sudden you join cdm/opposition just like mrema and cheyo did!!!
 
Mchumia tumbo huyo hakuna kitu hapo Chadema ndio habari yamjini yeye aseme ndoa yake na ccm ndio ipo mashakani
 
Kweli pesa ni balaa, ni mwigamba huyu huyu au kuna mtu ame hack kichwa chake? Nikizikumbukaga makala zake za kwenye ukurasa wa kalam ya Mwigamba na anavyofanya sasa, hakika nachanganyikiwa aise!
 
CHADEMA wanapambana na CCM ili kuiondoa CCM.ACT wanapambana na CHADEMA ili wapate nafasi ya CHADEMA itakapokuwa madarakani sijui CCM watakubali kuwaachia nafasi hiyo ya kambi ya upinzani.
 
ACT sera yenu kuu ni CDM kwa kauli hiyo utawakomoa wananchi maana kesho CUF au chama kingine kikikosea kama CDM nao utaanza mgogoro nao sasa sera yako itakuwa ipi
 
Katibu Mkuu wa ACT Samson Mwigamba amekiri ujio wa Muungano wa UKAWA umevuruga malengo ya chama chake.

Mwigamba amesema lengo kubwa la chama chake ni kuwaunganisha wananchi na kuwaeleza ubovu wa chama kikuu cha upinzani nchini Chadema.

Mwigamba amesema hata hivyo kwa sasa Chadema iko katika ushirika na vyama vya CUF na NCCR chini ya mwamvuli wa UKAWA.Ameendelea kudai kwamba imekuwa vigumu kueleza uovu wa Chadema wananchi wakaulewa kwa sababu imetokea wananchi wanaiamini UKAWA na hawataki useme chochote kuhusu mshirika wa umoja huo.

Mwigamba hata hivyo amesema anaamini UKAWA utasambaratika kabla ya 2015.Na baada ya hapo ndipo wananchi wataelewa kuhusu vita ya ACT na Chadema.

Source:Sauti Huru.

Hivi huyo Judeas Iskariot huwa yupogo? Nilidhani DEAD PEOPLE DO NOT COUNT!!
 
Back
Top Bottom