UKAWA haikujiandaa kwa mafuriko haya

UKAWA haikujiandaa kwa mafuriko haya

Lengo lako ni nini na huu uzi wako!? Unawataka UKAWA wasipokee wageni kama Dr. Slaa alivyofanya. Ubinafsi ni maradhi makubwa sana,hongera sana Mbowe.

Soma vizuri hiyo thread ww,sio unakurupuka tu,kwani nani kasema kumpokea mtu ni kosa,shida ni nyazifa wanazopewa hawa wageni ktk chama .
 
Kupokea wageni rukha, tatizo ni pale tayari una wageni kwako. Wengine hawajui wamefikaje ila nao wanahitaji nafasi. Ukawa imejipangaje kupanga na kupangua bila madhara mengine?

Mkuu tunayoyaona ya hovyo yanayofanyika nchini ni kutokana na udhaifu wa chama cha mapinduzi. Hapo namaanisha vyombo vyake vya maamuzi, Kamati kuu na Halmashauri kuu.
Hao wangekuwa makini wangeweza kuisimamia serikali katika day to day activities.
Chadema hata impokee nani, madamu vyombo vyake vya maamuzi bado viko makini wataweza kuwadhibiti watendaji wabovu na hawawezi kuleta zile tabia walizokuwa nazo kabla.
Jana nimemsikia Lowasa Mwanza akisema mtu yeyote anapovurunda ni kuondoa mara moja bila kusita. Nadhani hiyo njia ndio sahihi. Unajua hata hawa watendaji waliokuwa ndani ya CCM sio wabaya kabisa bali ni mfumo waliokuwa nao ndio uliokuwa unawasukuma kujikuta wanafanya mambo ya hovyo kabisa.
Nchi hii itajengwa na Watanzania hawa hawa tulionao ni swala la kurekebishana tuu.
 
Mbowe ni Genius wa siasa,sijui kwa nini Dr.Slaa hakutaka kuelewa the motive behind

Mkuu hata Mwenyezi Mungu huwa anawaumba wengine kuandaa mapito tuu kisha wajibu wao ukitimia anawaweka pembeni. Musa alipewa jukumu la kuwaondoa utumwani wana wa Israel lakini hakuingia nchi ya ahadi na hakulalamika.
Mzee wetu atulie tuu maana mbona tunaiheshimu kazi aliyoifanya na tutamuenzi tuu.
 
Ni jambo jema chadema kupata wageni wengi kiasi hicho, ila pia na wao wajitafakari sana ujio wa wageni hao, na wengi wao ni wale wanaoshindwa kwenye kura za maoni. na hao wageni wengi wanaingia chadema si NCCR wala CUF au NLD, hao wageni wengi wao wanataka nafasi za uongozi kwenye hicho chama, hasa ubunge na hatimaye waweze pata uwaziri wenye uzoefu wa kazi, kwani UKAWA ndo kuna nafasi nyingi za kugombea, Mbowe alisema kwamba kutatokea mabadiliko kwenye nafasi za ubunge, maana yake kuna nafasi walizochaguliwa za ubunge kubadilishwa kwa kiasi kikubwa, wataanza kuchomoa wa zamani na kuweka wapya wa mzee Lowasa,

Lakini nimeona baadhi ya vijana leo wanasema Dr. Slaa ana uroho wa madaraka, wamekwishasahau mroo wa madaraka, je ni sahihi kusema maneno hayo? vijana wanatumika vibaya sana, haya mageuzi yote yameletwa na akina Dr, na pia inatakiwa wafurahie matunda yao, ss kama ndo tunafanya hivo si jambo jema sana.

Angalizo langu, kama UKAWA wakishindwa uchaguzi huu, basi ni wazi kwamba upinzani utashuka sana sana, na itawachukua tena muda mrefu kuaminiwa na wanachi, je ni nani atayekubali kuimalisha chama alafu kikipendeza watu wanazamia? siku zote unapotafuta faida ujue pia na hasara ipo. Hao wazee kukaa pembeni iko siku watajua nn kiliwafanya wakae pembeni.
 
Sio kila mhamiaji atakuwa kiongozi. Ukawa hatugawi madaraka bali majukumu.

Kila mmoja atagombea kufuatana na utaratibu wa chama. Vyama vyote vitabaki na utawala wao bali taifa litaongoza na wote kulingana na kura au wabunge waliopata
 
Ccm tayari ina chuki na lowassa na hata wale watu waliokuwa karibu na lowassa wakati wakiwa ccm...ccm inaiendeleza chuki kwao kwa kuwaona kama wanafki ndani ya chama...wanawakata makusudi ili waonekane hawana mvuto kwa jamii na sisi tunawapokea bila wasi maana nia ni kuitoa ccm madarakani kwanza..
 
jamani kwa sasa ukisema mfumo wa vyama vingi unaeleweka maana tulitawakiwa na chama kimoja tuuu
Now tuone ukawa wataleta maendeleo gani ya tofauti
 
Ccm tayari ina chuki na lowassa na hata wale watu waliokuwa karibu na lowassa wakati wakiwa ccm...ccm inaiendeleza chuki kwao kwa kuwaona kama wanafki ndani ya chama...wanawakata makusudi ili waonekane hawana mvuto kwa jamii na sisi tunawapokea bila wasi maana nia ni kuitoa ccm madarakani kwanza..

Mimi naona kama tunawasingizia maCCM. Hapa mwenye chuki zilizopitiliza ni JK mwenyewe. Na kwa tabia za kisultani anazoziendeleza ni wimbi tu la miCCM kujenga chuki isiyo na mbele wala nyuma.

Lowassa anachukiwa na JK siyo na wanaCCM. Waliokuwa wanaambatana na Luwassa wanaipata fresh ya chuki za mkwere.

Kisultani hakuna utaratibu kuna umwinyi tu. Na ndicho kinachoitafuna CCM KWA USIMAMIZI WA MKWERE
 
Mbowe ni mwenye Upendo, na aliye na upendo ni; Mtulivu, hana hasira , pia huwatumikia wenzake. Ahsante sana Mbowe.
 
Hata tsunami hutulia yenyewe haihitaji mtu kuizuwia.

Binadam anaefata mafuriko huyo hajielewi, anakwenda na maji.

polee dada faiza. Najua position yako ndio inayokunyanyasa ila wewe ni mtu mzuri tu.
 
Wengi wanaoshindwa kwenye kura za maoni majimbon mwao, ndio wanaohamia Ukawa.. Wakijua kbsa Ukawa inaweza ikashinda na wenyew hawataachwa.. Hasara watapata pale Ukawa itaposhindwa, cjui wataelekea wap tn! maana wanahama kwa mbwembwe hao, kurud kwao itakuwa aibu kubwa..

yoyote yule anaeogopa changamoto kamwe hawezi kufanikiwa maishani mwake. katika vitu vinavyo sababisha kudumaa kwa vyama vya upinzani ni pamoja na mawazo kama haya yako.
 
Ukawa wataji adjust tu kuendana na ujio huu wa wanachama wapya,
Chama ili kikue kinahitaji wanachama, na hao wanachama hawatoki mbinguni ila ni wale wale wakutoka chama kimoja kwenda kingine,wanachama wapya kwa maana ya kutowahi kuwa na vyama kabisa before kujiunga na ukawa ni wachache sana.
 
Mkuu hata Mwenyezi Mungu huwa anawaumba wengine kuandaa mapito tuu kisha wajibu wao ukitimia anawaweka pembeni. Musa alipewa jukumu la kuwaondoa utumwani wana wa Israel lakini hakuingia nchi ya ahadi na hakulalamika.
Mzee wetu atulie tuu maana mbona tunaiheshimu kazi aliyoifanya na tutamuenzi tuu.


Kwel kabisa mkuuu
 
Back
Top Bottom