Wana MMU,
Nimekuwa nikichangia mada za wengine ila leo yamenikuta. Mahali ninapoishi kuna nyumba tano ambazo ni za mtu mmoja, zimezungushiwa ukuta na wote kwa pamoja. Tupo familia tano kama idadi ya nyumba zilizopo. Binafsi mi ni wa mwisho kuhamia hapa, hizi familia nyingine zipo kwa muda sasa.
Moja kati ya familia hizi nilibahatika kujenga nao urafiki kwa kuwa baba wa familia tunatoka mkoa mmoja, yeye ni mtu mzima kiasi ana mke na pia anaishi na mdogo wake, yeye pamoja na mkewe ni wafanyakazi katika ofisi tofauti, mdogo wake yeye ni mwanachuo. Jamaa ana gari ambalo hulitumia kumpeleka mkewe kazini na kumpitisha mdogo wake chuoni asubuhi.
Baada ya mimi kuhamia hapa nikawa nawapa lift mke na mdogo wake na huyu jamaa kwa kuwa kibaruani kwangu ni uelekeo mmoja na anapofanya kazi mke wa jamaa na anaposoma mdogo wake. Hili halikuwa tatizo kwangu kwa kuwa ni kawaida yangu kuishi vizuri na jirani zangu.
Hali imeendelea hivi kwa miezi mitatu sasa lakini jana jamaa akaja kunisalimu usiku wa saa mbili na kuniambia kuwa kuanzia kesho (leo) atakuwa anawapeleka mke na mdogo wake mwenyewe ofisini na chuoni japo kwa kufanya hivi atakuwa anazunguka maana ofisini kwake ni uelekeo mwingine.
Ilinishtua lakini nikaona nisiulize chochote nikamwambia sawa,jamaa akaaga.Nilitafakari na nikataka kujua kwanini jamaa amebadili maamuzi, nikahisi labda jamaa anahisi namtaka mdogo wake?! Sikupata jibu, leo mchana mdogo wake akanitumiasms " mambo, bro amemind wifi kukuzungumzia kila mara.."Nikachoka kabisa, ila nimejifunza kitu unaweza kuhisiwa vibaya bila kufanya ubaya. Tuwe makini na wake za watu.
Note: Sikuwahi kumtamani mke wa jamaa wala mdogo wake.