Ukaguzi wa vyeti feki Serikalini umeanza rasmi, waanza na Walimu

Kwa taarifa yako kwenye sekta binafsi watu hawajali vyeti wanajali uwajibikaji. Nadhani unaona tija katika taasisi binafsi kulinganisha na serekali. Huko kwenye sekta binafsi uwe na cheti usiwe na chetim, kinacholinda ajira yako ni kufikia lengo la muajiri basi.

Taasisi binafsi kabala ya cheti unatakiwa upige kaz waione. Unaweza ukawa na chet kaz hujui.
 
Hili ni jambo jema maana tumechoka kuwa na Vihiyo wengi maeneo ya kazi.Hata hivyo nashauri waanze na wakubwa kwanza halafu ndiyo wateremke hadi kwa wadogo.Nashauri hivi kwa sababu kuna jamaa mmoja nadhani anaitwa Kainerugaba Msemakweli ambaye aliwahi kuandika kitabu kilichoelezea Mafisadi wa Elimu Tanzania lakini hakuna hatua zilizochukuliwa kuthibitisha kama kilichoandikwa ni kweli au uongo.Kwa nyongeza ni kuwa Kihiyo mkubwa ana madhara makubwa zaidi kwa jamii ukilinganisha na Kihiyo mdogo.

Mkuu huyu si ndio alitoa Kitabu kabisa kikiwa na Orodha ya vigogo kadhaa Serikalini wenye PhD. feki?

Asilimia kubwa ya vigogo hao walitishia kua watamshtaki lakini hatukuona kesi yoyote iliyofunguliwa mpaka leo hii.

Mi naona huyo Bwana atafutwe yeye pamoja na Kitabu chake kiwe ndio muongozo wa kuwabaini hao Vigogo waljofoji Vyeti.
 
Jamani mie cha kwangu cha fm 4 kilipotea katika mazingira ya utata sana na sijui itakuwaje siku nikamkamata anayekitumia kwasababu naamini yupo tu.

Ulifuata taratibu za kupata Cheti kingine?
Isije kua ulikifanyia biashara Mkuu.
 
Mbona vyeti hukaguliwa kwanza ndo unathibitishwa kazin,labda upolis,jeshin,magereza na umuu wa mkoa au wilaya ndo nikirahis kufoji vyeti
 
mkuu watanzania ni wasahaulifu sana. wamesahau kuwa haya yote Kikwete alijaribu baadaye tukaona imepotezewa tu. nimeshangaa kuna baadhi yenu angalau mnaangalia nyuma. anyway, tusubiri.

JK alijaribu na alianzia polisi na jeshi nadhani, alichokiona huko nadhani ndio maana lilisitishwa ghafla. Kama kweli ni serious basi masharti ya vibali vya kazikwa wageni inabidi yalegezwe!
 
Huu uzi unafanana na uzi uliokanushw wa kutoa taswira mbaya ya taaluma za watu,mbona huu haukanushwi? By the way walimu hukaguliwa vyeti mara kwa mara na hasa unapooenda kufanya mtihani hadi kazini,ni zoezi ambalo lipo kila mara.Sasa hii habari ni mpya?
 
ndio maana posho walimu hatupati kisa kuna watu walitumia madirisha kutokea, duuu! kaza kabisa tena anzia KASULU.
 
Katika kuhakikisha wafanyakazi wa Serikali ni wale wenye sifa stahiki, Serikali imeanza ukaguzi wa vyeti ili kuhakiki kama ni vyeti ambavyo sio feki.

Baadhi ya mikoa walimu wametakiwa kuwasilisha vyeti vyao kwa uhakiki.

Baada ya walimu wataofuata ni Halmashauri zote nchini kwa kuwa fedha nyingi za maendeleo hupelekwa huko.

Connect Dots fedha za Elimu kupelekwa moja kwa moja kwa wakuu wa shule.
Tegemeeni watu wengi kupoteza uhai kwa kiharusi. Tena nawashauri wahakiki vyeti vyote kuanzia sekondari yaani form four hadi vyuo. Tunaweza kushangaa asilimia 75 wana vya magumashi.
 
bahati mbaya vyuo vyetu huwa havitunzi kumbukumbu za wahitimu wao,nina ushahidi wa hilo,jaribu kwenda hapo udsm uombe rekodi za mwanafunzi aliemaliza chuo 2005 uone kama watakupa.me binafsi nilimaliza pale 2013,bahati mbaya transcript yangu ililowana na mvua ikaharibka,mwaka huu nimeenda kuomba nyingne,cha ajabu wanasema nlishafutwa kwenye database ya chuo hvyo record zangu hazipo tena,sasa hyo ni udsm tu,bado sijajua hvi vyuo vidogo vinavyochipukia vyenyewe viko vipi.ndo maana nakuambia kwa necta watawakamata ila kwa vyuo vikuu sidhani.

Mkuu unazungumzia transcript ambayo kisheria ina expiry mara tu vyeti vinavyokuwa tayari. Transcript inakubalika kutumika kwa muda tu ambao unajulikana itakuwa vyeti habijatolewa kwa wahitimu ambapo haiwezi kuwa zaidi ya mwaka.

Record za masomo ni za kudumu kama ilivyo cheti chako cha kuzaliwa labda iwe ni chuo cha kichochoroni. Vyuo vyote kisheria inatakiwa iweke records za vyeti vya wanafunzi wao kwa miaka hata 70. Ukipoteza cheti original hupati chengine lakini muajiri au tassisi ikitaka matokeo yako wanaweza wakaandika barua au wewe ukaandika barua wakapelekewa directly na sio kupewa wewe mkononi.
 
Back
Top Bottom