Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Yanayojilia hoja za UK kupunguza mkopo tuliozoeshwa kuita msaada wa bajeti kwa Tanzania si ushoga, bali ni ubakaji wa demokrasia nchini. Viongozi waandamizi wa serikali wamekomalia kuongelea ushoga ili kutuyumbisha ukweli wenyewe. Na hata Cameroon ametumia neno la jumla zaidi katika haki za binadamu, na haki za binadamu ni mambo mengi ingawa ushoga laweza kuwa mojawapo. Ukweli kama alivyosema balozi wa UK ukweli wa jambo lenyewe limepotoshwa na wanasiasa kupata mahali pa kusimamia utetezi wa maovu wayafanyayo.