Ujumbe kwa wenye mamlaka ya kuajiri

Newbies

JF-Expert Member
Jul 13, 2018
1,492
2,164
Mdau anasema, tafadhali Sana usialike watafutaji wa kazi kwenye usaili Kama ulipanga kuitoa nafasi hiyo ya kazi kwa ndugu jamaa au marafiki. Wapo wanaokuja katika usaili kwa Nauli za kuazima Tena kwa umbali mrefu😭 imenihuzunisha Sana.

Screenshot_2024-03-15-22-20-43-00.jpg
 
Sasa watapata wapi ushahidi kuwa huyo ndugu yao amepata ajira kupitia interview.?
Nafasi moja mtu anaita Watahiniwa 100? Hizi ni akili kweli?

Ukiwa na nafasi 4 ita inteview watu 20 tu.

Binadamu wa kiafrika hawajali namna watu wengine wanavyo athirika na kupata hasara.

Kwenye Mashirika ya Wazungu kama kun anafasi tatu basi interview ataita Watu 10 tu.

Hapa bongo nafasi moja tu anataka kuchukulia na sifa humo humo anasumbua watu 100
 
Hapa bongo nafasi moja tu anataka kuchukulia na sifa humo humo anasumbua watu 100
100?

Mpaka 100,000 alafu mwenyewe mwenye nafasi yake tayari yupo ndani kashapewa ajira, watu wanaitwa kukamilisha ratiba tu ionekane watu waliitwa interview
 
Ndio maana watu wanatuma maombi ili wao wafanya kazi ya kuchuja wapatikane wachache
Mfano kwenye zile ajira za utumishi,

wakasema tunataka waliopata GPA kuanzia 4
Au
tunataka mtu ambaye amepitia A level na sio umemaliza O level ukaenda chuo moja kwa moja
Au
Tunamtaka mwandishi wa habari ila pia awe anajua kutumia maybe camera, sound equipments etc.
Au
Tunamtaka mhasibu ila lazima ajue kuendesha gari n.k

Yn kwa ufupi, tangazo lianze kukukataa hata kabla wahusika hawajakukataa.
 
Back
Top Bottom