Ujumbe kwa wanaume

Mkuu sijakupa andiko hilo tu nimekupa hadi hilo linalosema aziniye na mwanamke hana akili hilo nalo linamlenga mwanamke peke yake eti? Hahahaha yaani maandiko yanayomkataza mwanamke kuzini ndo sahihi ila yanayomkataza mwanaume kuzini ni ya kihuni?

Aisee kwenye biblia wanaume hmachomoki kwa sababu bado sijaona wala kusikia andiko linalomruhusu narudia tena linalomruhusu mwanaume kuzini wala kuoa mke zaidi ya mmoja bishana na maandiko siyo mimi tena
 
Daaaah....umesema ukweli...ila walahi mke mmoja hatoshi......yaan uwiiiiii.....hatoshi tena narudia
Duuh yaani hadi wewe mwanaume unayetumia neno 'uwiiiiii' unasema mwanamke mmoja hakutoshi? Halafu hii siyo post yako ya kwanza kuona umetumia hili neno ila mwanzo nilidhani umeliweka bahati mbaya tu ila kumbe ni makusudi kabisa basi nimeamini kweli wanaume kuchepuka mnajiendekeza tu
 
Basi huyo alikuwa hampendi mkewe
Mambo haya yanataka hekima, ukijua mmeo anachepuka
dawa siyo kususa ni kusimama kidete kuidhibiti hiyo hali
siyo kuzira,ukifanya hivyo unawapa nafasi wakati wewe ndo
mwenye mali.Mmeo akichepuka cha kwanza jihoji binafsi ni kwa nini then chukua hatua.
 
Mambo haya yanataka hekima, ukijua mmeo anachepuka
dawa siyo kususa ni kusimama kidete kuidhibiti hiyo hali
siyo kuzira,ukifanya hivyo unawapa nafasi wakati wewe ndo
mwenye mali.Mmeo akichepuka cha kwanza jihoji binafsi ni kwa nini then chukua hatua.
Kuna wanaume ambao wanapata kila kitu kutoka kwa wake zao ila wanachepuka ili tu kubadilisha ladha sasa hapo napo mke ajichunguze kitu gani? Wanaume kubalini tu kwamba mnafanya makusudi kuchepuka ila mnatumia mapungufu ya wake zenu kama ndo sababu za kuhalalisha huo umalaya
 
Hahahahahaaaa,siku hizi MTU akishindwa kukushinda kwa hoja atatafuta udhaifu mdogo wakipuuzi ilimradi tu aonekane bora kuliko wewe....in fact,one woman is not enough for me,whether u like or dislike it.....find another shit to squirt....
 
Ni vigumu kupingana na uumbaji
 
Hahahahahaaaa,siku hizi MTU akishindwa kukushinda kwa hoja atatafuta udhaifu mdogo wakipuuzi ilimradi tu aonekane bora kuliko wewe....in fact,one woman is not enough for me,whether u like or dislike it.....find another shit to squirt....
Mimi au nyie wenyewe wanaume mnaodhani kila kitu ni umama? Hayo ya kusema kwamba kuna kauli fulani mwanaume haimpendezi kuzitumia mmeanzisha wenyewe wengine tunaendeleza tu by the way kama mwanamke mmoja hakutoshi who cares?

Raha ya mwanaume kuchepuka mkeo akijua aone wivu ila ukiona anajua halafu anakupotezea jua kashakuona fala kashakudharau na hajali anakuwa yuko tayari kwa lolote wewe endelea na umalaya wako tu baba no one cares wala usijishitukie tuna mambo mengi ya kufanya siku hizi kuliko kuhangaika na wanaume kama nyie
 
Ni vigumu kupingana na uumbaji
Uumbaji upi? Kwani uumbaji si unaonyesha kwamba binadamu wa kwanza walikuwa ni mwanaume mmoja na mwanamke mmoja au?

Na Mungu si alisema mwanamume atamuacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe nao watakuwa mwili mmoja nasisitiza mkewe siyo wakeze na kumbuka ubavu wa Adam ulitumika kumuumba mwanamke mmoja tu na siyo zaidi kwahiyo wewe ubavu wako ni mwanamke mmoja tu

Yaani kwa kifupi ukishakuwa na mke mmoja huyo ndo anayehesabika hao wengine utakaowaongeza unajidanganya wewe na unawadanganya wao kwahiyo ni kama unazini nao tu hakuna cha baadhi ya dini kuruhusu wala sijui wanaume mmeumbwa na tamaa hamtosheki na mwanamke mmoja

Na usiwatolee mifano hao mitume na manabii wa zamani waliokuwa na wake wengi hao nao hiyo waliyoifanya ilikuwa ni dhambi na ndo maana walipozeeka walitubu wakasamehewa ila siyo wanaume wa siku hizi badala ya kukubali kuwa hilo ni kosa bado mnatafuta sababu za kuhalalisha halafu mnasema Mungu ndo karuhusu sijui uumbaji ndo umeruhusu uumbaji upi huo?
 
ngoja uolewe, halafu upate uzoefu ndo maada itakua nzuri sasa hivi unaongea nadharia tu
 
ha ha ha ha umenishinda kwa hoja
 
Mimi nawashangaa mnavyotafuta visingizio wakati maandiko yako wazi kabisa na hizo dini nyingine sijui zinamuabudu mungu yupi aliyewaruhusu kuoa wake wengi shauri yenu
ha ha ha ha umenishinda kwa hoja
 
Mimi nawashangaa mnavyotafuta visingizio wakati maandiko yako wazi kabisa na hizo dini nyingine sijui zinamuabudu mungu yupi aliyewaruhusu kuoa wake wengi shauri yenu
ha ha ha ha
 
Mkuu uzinzi unaosemwa hapo juu ya mwanaume ni ule wa kutoka na mke wa mtu. Lkn Biblia haijatuzuia sisi hata kama tumeoa kujihusisha na mchepuko ambaye siyo mke wa mtu. Biblia imemzuia mwanamke kujihusisha na mwanaume mwingine akiolewa bila kujali atakayejihusisha naye ameoa au hajaoa! Mwanamke akiolewa anakuwa amefungwa na sheria hadi mumewe afe. Lkn mwanaume anakatazwa tu kujihusisha na mke wa mtu. Lkn kwa mfano mimi nikikulana na wewe ambaye huna mume hiyo inaruhusiwa.
 
Dada nimefatilia comments zako umejitahidi kuwaelewesha hao viumbe wachepukaji ila nasikitika hawatakuelewa ndoa kwao ni fashion waonekane wameoa.
 
Hahahaha duuh waalimu wana kazi aisee mkuu hebu rudia hii sentensi "aziniye na mwanamke hana akili" hivi ambaye hajaolewa siyo mwanamke? Hapo maana yake ukishaoa hautakiwi kutoka nje ya ndoa

Sababu ukifanya na mwanamke asiye wako tayari umeshazini haijalishi huyo hawara kaolewa au hajaolewa halafu kuna andiko linasema "lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe" hilo linadhihirisha kwamba ndoa ni ya mume mmoja na mke mmoja

Haya nikakupa andiko jingine linasema "ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi wazinzi na waasherati Mungu atawahukumia adhabu" haya hilo hapo limekataza hadi uasherati maana naona wewe umeshikilia hapo kwenye uzinzi tu

Halafu hilo andiko unalosema tumeruhusiwa kuachana kwa sababu ya uzinzi limeruhusiwa kwa wote wala siyo kwa wanaume tu hebu katafute mtu ambaye haijui biblia vizuri ndo umdanganye hapa umekosea njia
 
Dada nimefatilia comments zako umejitahidi kuwaelewesha hao viumbe wachepukaji ila nasikitika hawatakuelewa ndoa kwao ni fashion waonekane wameoa.
Yaani acha tu najua kabisa kwamba hawawezi kunielewa wala hawawezi kuacha ila nataka wajue kuwa wanapochepuka ni juu yao wenyewe hakuna maandiko yanayoruhusu maana wanajitetea eti maandiko yamewaruhusu sasa ndo nimewaambia wanionyeshe maandiko yaliyoruhusu wanambwelambwela tu
 
Hahahahaahahahahah!

Hongera mkuu, mimi nlishawaambia family yangu kabisa. Ikitokea siku nimemuacha wife basi wanikamate, wanifunge kamba waniwahishe hospital maana itakuwa sio akili zangu
 
Mimi nafikiri hii inatokana na ile nature ya mwanamme aloumbwa nayo.
Mitara.

Kupambana na nature ni kazi,ila mabadiliko ya kimazingira,kibaiolojia na kiuchumi yanasaidia baadhi kubadilika.

Zamani hakukuwa na mayai ya kisasa.
Hivi wewe unaamini kwenye mitala sincerely??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…