There you are Lizzy,
Naona some umelipata kweli kweli....
Ndiyo maana tumeimbishwa sana huko nyuma...Talk, talk, talk, talk, talk,talk, talk, talk, talk...........!!!
Hahahaha. ,Marudio ya theory au praktiko??
Babu wengine utasikia wanasema hata cha kuongelea hawana na bado wanajitambulisha kwamba wapo kwenye mahusiano. Sijui hapo hua wanategemea nini haswa!!
Hahahaha. ,
Ummmhh . . . theory na practical ndio nahangaika nayo sasa hivi. Ngoja tuone matokeo.
Halafu usije kujiingiza kwenye mtego wa kutunza vitu moyoni kama yule bibi wa Titanic!!
Sharing is not only caring but also healing!!
Ndiyo maana tumeamua kuweka kambi hapa MMU!!
Babu nakushukuru sana, ni kama umeletwa na mungu kwangu...nimejifunza sana kwa maana nami ndo nakoelekea..hii namba mbili hapo imenifungua macho...ni kama viconflict nilivyokuwa navyo moyoni vimepata majibuHeri ya mwaka mpya wapenzi wa jukwaa letu la MMU na pia natoa pole kwa wote ambao wana migogoro ya kiafya!!
Baada ya mijadala ambayo tumeifanya mwaka uliopita na ile ambayo tumefungia mwaka, baadhi ya wanadau ambao ni next generation ya wanandoa walihisi kwamba wametengwa. Kwa leo nimeona niwawekee maneno kidogo hapa, ili yawasidie wakati wanajiandaa kuingia kwenye hii taasis ambayo ni very simple but yet extremely complex, very sweet but also the hardest to swallow at times (hata quinine haifai) and very exciting but also boring!!
- Dont be naïve: Ni muhimu kufanya maandalizi ya ndoa kwa umakini wa hali ya juu na kuachana na utopia ambazo zinaweza kukusababishia matatizo. Haya mambo ya kudanganywa na maua, chocolate, sms za ajabu ajabu, simu za kila baada ya nusu saa (for girls) au ad libitum sex (kwa boys) visitumike kama vigezo vya kumpa mtu nafasi .Hakikisha unafanya home work yako (due diligence ya kutosha) vinginevyo utakumbana na mikataba kama ya Richmond; and that will be too late!!
- Hakuna sababu ya kuwa na huruma: Hakuna sababu ya kumwonea mtu huruma kwa sababu wewe siyo mama yake wala Yesu Masiha! .....Utasikia mtu anasema kuwa amekaa na GF au BF wake kwa muda mrefu kwa hiyo anaogopa kumuumiza Yes ataumia but that will be over after a very short time! Ila kama utajifanya Msamaria na kumkubali mtoto wa watu basi utakuwa umemharibia maisha yake yote Dhambi hiyo ni kubwa sana!!
- Unshakable criteria: Lazima mtu ujitambue wewe mwenyewe ili uweze kuwa na vigezo vya kumpimia mwenzio. Kama huwezi kufanya hiyo kazi, bora jikalie tu utange tange mitaani It will be very hard to work out your way kwenye ndoa kama hujui unachokitaka. Ni sawa na kwenda kuuza vitu sokoni ambavyo hata hujui bei yake katika masoko .Pia mwenzio akikugundua anaweza kukufanya msukule
- Dont compromise on important issue: Kwa mfano, kama unajua kuwa huwezi kulea mtoto wa kambo, basi usifanye urafiki na mtu mwenye mtoto (either sex). Pia usipende kufanya majaribio kwa kuwa na mahusiano na watu ambao wewe unajua kuwa hawana vigezo vyako muhimu (hii inawahusu sana boys ambao wanapenda kuchezea vitoto vya mitaani huku wakijidanganya kwamba wana pass time).
- Dont be a spectator: Ukishaamua kuwa na urafiki na mtu, hakikisha unashirikiana naye mambo yake ya muhimu. Kwa mfano, kuna vijana wengi (hata wanaume) wanakuwa na GF ila hawajui hata cycle zao zinaanza na kuisha lini. Matokea yake wanakuja kulalamika mara GF anaporipoti kuwa kapata mimba ................Ni muhimu kushea details na mwenzio ili kuondoa chances za kuwa surprised na mambo ambayo hukuyategemea kabisa na labda ungemsaidia kuya-avoid!
- Acha mizaha: Kuna watu wanafanya majaribio ya hatari katika mahusiano..Like kutumia ngono za mitandao isiyoruhusiwa. Pia kuna watu hawajali hata wakipata watoto kwenye mahusiano yasiyoeleweka. Please do whatever possible to avoid pregnancy if you cant be friends without sex!
- Expect the unexpected: Mahusiano yoyote kabla ya ndoa hayako binding Nawashauri vijana wajiandae kwa lolote But take precautions ili kupunguza maumivu. Kwa mfano, siyo fair kuwa kwenye relationship isiyoeleweka kwa miaka 2 au zaidi!!
Naamini wadau wataongeza au kuboresha ili hii dossier iwe ya manufaa kwa wadau na utukufu wa taasisi ya ndoa urudi mahali pake!!
Mungu awabariki nyote,
Babu DC (1947)
Hahahaha,
Babu bwana,
Ndio nimemaliza shule ya upili na kupata barua ya kujiunga chuo but nimejaza form ya kupostipondi kujiunga na chuo mpaka mwakani,
Ndio maana naona somo lako limekuja kwa wakati muafaka.
Babu nakushukuru sana, ni kama umeletwa na mungu kwangu...nimejifunza sana kwa maana nami ndo nakoelekea..hii namba mbili hapo imenifungua macho...ni kama viconflict nilivyokuwa navyo moyoni vimepata majibu
GBY (God Bless You)
Babu mbona hukuniambia kama umepost huku! Hii kitu inanihusu. Fafanua vizuri namba mbili na namba 7.
- Expect the unexpected: Mahusiano yoyote kabla ya ndoa hayako binding…Nawashauri vijana wajiandae kwa lolote…But take precautions ili kupunguza maumivu. Kwa mfano, siyo fair kuwa kwenye relationship isiyoeleweka kwa miaka 2 au zaidi!!
Happy new Year Hus,
Mbona unatoroka bila ruksa ya babu?? Ukishachakachuliwa utashitaki kwa nani??
Mie nilidhani iko clear sana ....
Hata hivyo niseme tu kuwa, kwa watu walio kwenye ndoa, kutoka ni jambo gumu na uzito. Ila kwa maoni yangu, linatakiwa kuwa jambo jepesi kumpiga chini BF au GF! Ukiona vigezo havijai chupa au akakuboa to death, unapiga chini na kusoga mbele...Hili litakuwa rahisi kama watu watakuwa wajanja kutotumia muda wao mwingi katika temporary relationships. Tena kama mwenzi mwenyewe haeleweki.
Tumeongea sana na akina Lizzy jinsi ya kumtambua mtu ambaye ameegesha kwako ili kupass time au kumsubiri Mr/Miss Right wake....!!
Hapo vipi??
Babu DC
Kumbeeeeeeeeeee,
You are almost getting there....You have my support and just knock on my door any time!!!
Bonne chance (good luck)!!!
ahsante babu, nisamehe kwa kuondoka bila kukuaga. Sasa hapo kwenye kupga chini asiefaa inabidi uandae darasa maana kuna vijana wake kwa waume ni ving'ang'anizi kama luba.
- Hakuna sababu ya kuwa na huruma: Hakuna sababu ya kumwonea mtu huruma kwa sababu wewe siyo mama yake wala Yesu Masiha! .....Utasikia mtu anasema kuwa amekaa na GF au BF wake kwa muda mrefu kwa hiyo anaogopa kumuumiza…Yes ataumia but that will be over after a very short time! Ila kama utajifanya Msamaria na kumkubali mtoto wa watu basi utakuwa umemharibia maisha yake yote…Dhambi hiyo ni kubwa sana!!
Halafu ni lazima tunapokuwa na wapenzi tujenge expectations za kuishi nao maisha ya ndoa? Je nikiamua kuwa na mtu sahivi halafu huko mbele nikatafuta ustaarabu mwingine hiyo hairuhusiwi?
Hivi king'ang'anizi anaweza akakufanya uendelee kuwa kwenye mahusiano usiyoyataka?ahsante babu, nisamehe kwa kuondoka bila kukuaga. Sasa hapo kwenye kupga chini asiefaa inabidi uandae darasa maana kuna vijana wake kwa waume ni ving'ang'anizi kama luba. Halafu ni lazima tunapokuwa na wapenzi tujenge expectations za kuishi nao maisha ya ndoa? Je nikiamua kuwa na mtu sahivi halafu huko mbele nikatafuta ustaarabu mwingine hiyo hairuhusiwi?
Babu nashukuru sn,ila safari inayonisuburi mwakan kwa miaka mitatu co rahic kuna sapu,cariova na diskolifikeshen so bado safari bado ndefu sn babu nikuomba mungu atufikishe salama.
Hivi king'ang'anizi anaweza akakufanya uendelee kuwa kwenye mahusiano usiyoyataka?
Kwangu huo ni udhaifu, inaonyesha kwamba hufanyi yale unayotaka/penda/hitaji wewe bali wanayotaka watu wengine (mf king'ang'anizi). Kama mtu humpendi/hutakia kuendelea na mahusiano nae unatakiwa ujiweke wewe kwanza ba sio yeye. Ukikueleza kwamba mahusiano yenu ndio basi tena uwe as straight as possible, usimung'unye maneno, usiyapake sukari na swala la huruma uliweke kando.
Babu wengi wanaoshindwana baadae hua wanaanza hivi. Mtu anaona kabisa aliyenae sie ama kamchoka alafu eti anakubali kubaki kisa katolewa machozi ama kang'ang'aniwa. Matokeo yake ni kupotezeana muda kuwa kwenye mahusiano ambayo yataanguka tu baadae.Poa sana Lizzy,
Inasikitisha kwamba kuna watu wanaweza kukubali kutumiwa (for whatever lame reasons) na kutafunwa tafunwa kama miwa ili utamu ukiisha watemwe njiani na kuwa msosi wa nyenyere!!
Very pathetic!!
Ngoja tumsikilize Hus, kama kweli anaweza kukubali kutumiwa namna hiyo!!
kwani kutooa ndio utoto babu?Kumbe na wewe bado upo upo, unashangaa shangaa????
Haki ya nani, lazima mwaka huu tuwatambue Boys na Girls wote ili tunapoongea mambo ya watu wazima tuwaombe watupishe kwanza!!!!
Babu DC!!