Ujumbe kwa wanandoa watarajiwa!



...kuna ule msemo watu wanasema huyu uliyemuoa wala sio type yako,....
hebu mtu mzima ichambue hii, naamini ushawahi isikia...!

Naweza na mie nikajaribu kujibu? Pleaaaaase. . . .!!

Nwy acha nijibu tu.

Wanaweza wakawa sahihi kwa maoni yao kwasababu wanaona zile tofauti. Wapo watu wanaotofautiana sana lakini tofauti zao ndio zikawafanya waelewane sana. Yani tofauti za mmoja zikiwekwa na za mwenzake zinatengeneza kitu kilichokamilika.

https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/164443-mimi-na-wewe.html#post2369774

Niliwahi kuanzisha mada inayosema sisi ni kama vipande vya puzzles, tulivyo, tabia zetu, muonekano, akili, fikra ndio hivyo vipande vya puzzles. Na tunapochagua wenzi tunatakiwa tuangalie ambae vipande vyetu vitaendana na vyao kutengeneza picha kamili.

Wengine, kutokana na walivyo inabidi wapate wanaofanana nao, wengine tofauti ndizo zitakazowaweka pamoja. Ukilazimisha kwa mtu unaefanana nae (kama hao walimwengu wanavyotaka) wakati kiukweli unahitaji wa tofauti ndipo matatizo huanza. Ndio maana mimi nadhani ni muhimu watu wakachagua wenyewe kuendana na mataka/mahitaji yao bila ya kujali walimwengu wanawaonaje pamoja.
 
Babu DC, asante kwa neno hili! Nimeona mtu amekuwa na BF kwa miaka 7, wanaishi mji mmoja lakini mdada hajui boifrendi anapoishi! Hii si kwa wanaume tu, hata wanawake! Kuna hajui BF anaishi wapi, anafanya kazi wapi, anafanya kazi gani, hajui marafiki zake wala ndugu zake! Kwanza inaonesha jinsi usivyomjali mwenzio!


[*]Don’t be a spectator: Ukishaamua kuwa na urafiki na mtu, hakikisha unashirikiana naye mambo yake ya muhimu. Kwa mfano, kuna vijana wengi (hata wanaume) wanakuwa na GF ila hawajui hata cycle zao zinaanza na kuisha lini. Matokea yake wanakuja kulalamika mara GF anaporipoti kuwa kapata mimba…................Ni muhimu kushea details na mwenzio ili kuondoa chances za kuwa surprised na mambo ambayo hukuyategemea kabisa na labda ungemsaidia kuya-avoid!


Mungu awabariki nyote,


Babu DC (1947)
 
Babu DC, asante kwa neno hili! Nimeona mtu amekuwa na BF kwa miaka 7, wanaishi mji mmoja lakini mdada hajui boifrendi anapoishi! Hii si kwa wanaume tu, hata wanawake! Kuna hajui BF anaishi wapi, anafanya kazi wapi, anafanya kazi gani, hajui marafiki zake wala ndugu zake! Kwanza inaonesha jinsi usivyomjali mwenzio!

Duh!!
Watu wanakutana kimjini mjini, wanamalizana kimjini mjini na kuagana kimjini mjini. Sasa huyo dada ni kwamba hajawahi kuuliza ama? Mimi hata rafiki ambae sijui anapoishi na hajawahi kunialika kwake(si lazima niende) siwezi kumwita rafiki wa karibu.
 


...kuna ule msemo watu wanasema huyu uliyemuoa wala sio type yako,....
hebu mtu mzima ichambue hii, naamini ushawahi isikia...!

Hiyo ni haki yao kwa sababu kila mtu yuko entitled kuwa na opions zake bila kuomba ruhusa ya mtu mwingine. Ila mhusika mwenyewe ndiye anayejua kwa nini ameamua kuwa na mwenzi wake aliyenaye....Hata hivyo kuna watu ama wanajikuta wametumbukia kwenye mahusiano kwa sababu ambazo hazikizi vigezo vyao vya msingi au pressure ya wanajamii na ndugu...Hilo kwa maoni yangu ni hatari kuliko ukoma!!

Ni vizuri mtu mwenyewe ajichagulie ili aweze kubeba dhamana ya matokeo ya uamuzi wake!! Na katika kufikia azma hii anaweza kusikiliza au kutosikilza maoni na ushauri wa mtu mwingine yeyote!! Na ingekuwa vizuri jamii ikapunguza tabia ya kuingilia mambo ya ndoa za wenzao!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Naweza na mie nikajaribu kujibu? Pleaaaaase. . . .!!

Nwy acha nijibu tu.

Wanaweza wakawa sahihi kwa maoni yao kwasababu wanaona zile tofauti. Wapo watu wanaotofautiana sana lakini tofauti zao ndio zikawafanya waelewane sana. Yani tofauti za mmoja zikiwekwa na za mwenzake zinatengeneza kitu kilichokamilika.

https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/164443-mimi-na-wewe.html#post2369774

Niliwahi kuanzisha mada inayosema sisi ni kama vipande vya puzzles, tulivyo, tabia zetu, muonekano, akili, fikra ndio hivyo vipande vya puzzles. Na tunapochagua wenzi tunatakiwa tuangalie ambae vipande vyetu vitaendana na vyao kutengeneza picha kamili.

Wengine, kutokana na walivyo inabidi wapate wanaofanana nao, wengine tofauti ndizo zitakazowaweka pamoja. Ukilazimisha kwa mtu unaefanana nae (kama hao walimwengu wanavyotaka) wakati kiukweli unahitaji wa tofauti ndipo matatizo huanza. Ndio maana mimi nadhani ni muhimu watu wakachagua wenyewe kuendana na mataka/mahitaji yao bila ya kujali walimwengu wanawaonaje pamoja.


Safi sana Lizzy,

Ndiyo maana juzi nilisema kwamba tayari wewe umehitimu...Tunasubiri kukupa cheti na kuona praktiko!!

Mungu atembee na wewe popote unapoenda,

Ni dua za,

Babu DC (1947)!!
 
Babu DC, asante kwa neno hili! Nimeona mtu amekuwa na BF kwa miaka 7, wanaishi mji mmoja lakini mdada hajui boifrendi anapoishi! Hii si kwa wanaume tu, hata wanawake! Kuna hajui BF anaishi wapi, anafanya kazi wapi, anafanya kazi gani, hajui marafiki zake wala ndugu zake! Kwanza inaonesha jinsi usivyomjali mwenzio!

Hii ni irresponsibility ya hali ya juu kabisa...

Hivi ukijikuta unadate serial killer aliyejaza vichwa vya watu kwenye freezer nyumbani utamlilia nani?

Kwanza vijana watambue kuwa mtu anayekupenda kweli atataka kukufahamu in and out na wewe pia kama unapenda uta-respond positively!!

Mtu wa namna hiyo anahitaji ama kucharazwa bakora au kupigiwa maombi ya mwezi mzima....He/she is a loser!!

Duh!!
Watu wanakutana kimjini mjini, wanamalizana kimjini mjini na kuagana kimjini mjini. Sasa huyo dada ni kwamba hajawahi kuuliza ama? Mimi hata rafiki ambae sijui anapoishi na hajawahi kunialika kwake(si lazima niende) siwezi kumwita rafiki wa karibu.

Mtu anayekuficha mambo yake ya msingi anawezaje kuwa rafiki??

Inabidi watu wajitahidi kufikiria kwa kutumia vichwa vyao halisi!!
 
Babu DC ujumbe mzuri sana huu naamini utawafaa na kuwaongoza sana wanandoa watarajiwa
 
Heri ya mwaka mpya wapenzi wa jukwaa letu la MMU na pia natoa pole kwa wote ambao wana migogoro ya kiafya!!


Baada ya mijadala ambayo tumeifanya mwaka uliopita na ile ambayo tumefungia mwaka, baadhi ya wanadau ambao ni next generation ya wanandoa walihisi kwamba wametengwa. Kwa leo nimeona niwawekee maneno kidogo hapa, ili yawasidie wakati wanajiandaa kuingia kwenye hii taasis ambayo ni very simple but yet extremely complex, very sweet but also the hardest to swallow at times (hata quinine haifai) and very exciting but also boring!!

  1. Don’t be naïve: Ni muhimu kufanya maandalizi ya ndoa kwa umakini wa hali ya juu na kuachana na utopia ambazo zinaweza kukusababishia matatizo. Haya mambo ya kudanganywa na maua, chocolate, sms za ajabu ajabu, simu za kila baada ya nusu saa (for girls) au ad libitum sex (kwa boys) visitumike kama vigezo vya kumpa mtu nafasi….Hakikisha unafanya home work yako (due diligence ya kutosha) vinginevyo utakumbana na mikataba kama ya Richmond; and that will be too late!!
  2. Hakuna sababu ya kuwa na huruma: Hakuna sababu ya kumwonea mtu huruma kwa sababu wewe siyo mama yake wala Yesu Masiha! .....Utasikia mtu anasema kuwa amekaa na GF au BF wake kwa muda mrefu kwa hiyo anaogopa kumuumiza…Yes ataumia but that will be over after a very short time! Ila kama utajifanya Msamaria na kumkubali mtoto wa watu basi utakuwa umemharibia maisha yake yote…Dhambi hiyo ni kubwa sana!!
  3. Unshakable criteria: Lazima mtu ujitambue wewe mwenyewe ili uweze kuwa na vigezo vya kumpimia mwenzio. Kama huwezi kufanya hiyo kazi, bora jikalie tu utange tange mitaani…It will be very hard to work out your way kwenye ndoa kama hujui unachokitaka. Ni sawa na kwenda kuuza vitu sokoni ambavyo hata hujui bei yake katika masoko….Pia mwenzio akikugundua anaweza kukufanya msukule
  4. Don’t compromise on important issue: Kwa mfano, kama unajua kuwa huwezi kulea mtoto wa kambo, basi usifanye urafiki na mtu mwenye mtoto (either sex). Pia usipende kufanya majaribio kwa kuwa na mahusiano na watu ambao wewe unajua kuwa hawana vigezo vyako muhimu (hii inawahusu sana boys ambao wanapenda kuchezea vitoto vya mitaani huku wakijidanganya kwamba wana pass time).
  5. Don’t be a spectator: Ukishaamua kuwa na urafiki na mtu, hakikisha unashirikiana naye mambo yake ya muhimu. Kwa mfano, kuna vijana wengi (hata wanaume) wanakuwa na GF ila hawajui hata cycle zao zinaanza na kuisha lini. Matokea yake wanakuja kulalamika mara GF anaporipoti kuwa kapata mimba…................Ni muhimu kushea details na mwenzio ili kuondoa chances za kuwa surprised na mambo ambayo hukuyategemea kabisa na labda ungemsaidia kuya-avoid!
  6. Acha mizaha: Kuna watu wanafanya majaribio ya hatari katika mahusiano..Like kutumia ngono za mitandao isiyoruhusiwa. Pia kuna watu hawajali hata wakipata watoto kwenye mahusiano yasiyoeleweka. Please do whatever possible to avoid pregnancy if you can’t be friends without sex!
  7. Expect the unexpected: Mahusiano yoyote kabla ya ndoa hayako binding…Nawashauri vijana wajiandae kwa lolote…But take precautions ili kupunguza maumivu. Kwa mfano, siyo fair kuwa kwenye relationship isiyoeleweka kwa miaka 2 au zaidi!!

Naamini wadau wataongeza au kuboresha ili hii dossier iwe ya manufaa kwa wadau na utukufu wa taasisi ya ndoa urudi mahali pake!!


Mungu awabariki nyote,


Babu DC (1947)
no 7 maximum iwe three month
 
Hiyo point kwamba usimhurumie mtu mpige chini tu ni muhimu sana kuizingatia hahaha ahsante kama binti huna mpango nae usikae nae sana lala mbele fasta.
 
Babu DC ujumbe mzuri sana huu naamini utawafaa na kuwaongoza sana wanandoa watarajiwa


Hahahahahahah,

Hujambo dogo? Heri ya mwaka mpya!!

Wewe ni wa pili after Lizzy, kuwapasia wengine mpira badala ya kuucheza!!

Vyovyote vile, naamini umeambulia kitu cha kukufaa kama silaha muhimu mbele ya safari inayokukabili!!

Usisahau kula na wenzio akina Hus!!

Babu DC!!
 
Ujumbe ni mzuri sana babu DC.
mm binafsi nimechukua ki2 hapa.
asante sana dark city.

Poa ndugu yangu,

Hebu basi na wewe ongezea kidogo ili wenzio wafaidi uzoefu wako.

Kwa mfano, unalionaje suala la kutegesheana mimba ili kulazimisha ndoa??

Babu DC!!
 
no 7 maximum iwe three month

Poa tu kama wadau watakubaliana na wewe.....!!!

Unaweza kushauri nini kifanyike na kipi kisifanyike ndani ya hiyo miezi 3???

Mfano, ni fair kupeana tunda katika huo muda mfupi??

Babu DC!!
 
Hiyo point kwamba usimhurumie mtu mpige chini tu ni muhimu sana kuizingatia hahaha ahsante kama binti huna mpango nae usikae nae sana lala mbele fasta.


Kaka usiwe mbinafsi,

Hata wadada wanatakiwa kuwapiga chini watoto wa mama wanaokuja kwa GFs wao na kuanza kulilia kama midoli inayotumia betri za Tiger!!

Babu DC!!
 
Asante sana Babu huu uzi utakuwa na manufaa sana kwangu...

Kumbe na wewe bado upo upo, unashangaa shangaa????

Haki ya nani, lazima mwaka huu tuwatambue Boys na Girls wote ili tunapoongea mambo ya watu wazima tuwaombe watupishe kwanza!!!!

Babu DC!!
 
Hapo kwa mwaka utakuwa na relationship ngapi??

Kwani maximum unatakiwa kuwanazo ngapi ndugu??

Kama hamtangulizi tamaa ya kubanjuana, nadhani ni strategy nzuri ili kuwajua waegeshaji!! Ila kama mtatanguliza libeneke basi hapo lazima wototo watachakaa kabla ya umri wao!!

Babu DC
 
Kuna falsafa moja inasema;Uongo uliwahi kuwa ukweli wakati fulani,lakini pia ukweli jambo ambalo halijapata jambo lingine la "kupruvu" otherwise.Yaani ukweli ni uongo mtarajiwa!
 
Asante sana babu nimepata somo,limeniingia sawia...na nitalizingatia.:poa
Mungu akubariki sana...Happy new year to u!!
 
Back
Top Bottom