Ujenzi wa Subway Trains jijini Dar

Ujenzi wa Subway Trains jijini Dar

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
40,801
Reaction score
46,925
Nilikuwa naomba kuuliza,

Hivi kati ya BRT na underground (subway) trains, mradi upi ungeweza kuleta matokeo makubwa na ya haraka?

Foleni za Dar usipokuwa na roho ngumu unaweza ukadondosha chozi barabarani kama mtoto mdogo, especially kama unawahi appointment muhimu.

Pia tufahamishane; mradi wa BRT una bajeti ya kiasi gani? Na je, pesa hizo zingetosha kutekeleza mradi wa ujenzi wa subway hapa Dar?

Pia tufahamishane, ni nini kimesababisha miaka yote hii ya uhuru? Tumeshindwaje kuwa na ka-flyover walau hata kamoja tu hapa Dar despite the incredible necessity na hasara yote hii tunayopata kutokana na foleni?

DON FRANCIS
 
Don, kuna kitu kinaitwa "opportunity cost"
 
Shanghai_metro_line_2_people's_square_station.jpg CHINA SUBWAY1.jpg CHINA SUBWAY2.jpg

Kama hivi?
 
Nilikuwa naomba kuuliza,

Hivi kati ya BRT na underground (subway) trains, mradi upi ungeweza kuleta matokeo makubwa na ya haraka?

Foleni za Dar usipokuwa na roho ngumu unaweza ukadondosha chozi barabarani kama mtoto mdogo, especially kama unawahi appointment muhimu.

Pia tufahamishane; mradi wa BRT una bajeti ya kiasi gani? Na je, pesa hizo zingetosha kutekeleza mradi wa ujenzi wa subway hapa Dar?

Pia tufahamishane, ni nini kimesababisha miaka yote hii ya uhuru? Tumeshindwaje kuwa na ka-flyover walau hata kamoja tu hapa Dar despite the incredible necessity na hasara yote hii tunayopata kutokana na foleni?

DON FRANCIS

Definitely underground rail system ingeleta matokeo ya haraka sana. Lakini hatuwezi, na kama sikosei Africa nzima hakuna underground trains. Angalia hii; Mradi wote wa BRT, 21km, gharama yake ni USD 290m.

Source; http://www.worldbank.org/en/news/pr...em-benefit-300000-commuters-create-80000-jobs.

Wakati ujenzi wa ungerground rail system, Kilometre 1 tu inagharimu around USD 200m!!!

Source; http://railway-technical.com/finance.shtml
Kwa maneno mengine, ujenzi wote huu wa BRT tunaoufanya tungeweza kujenga kama kilometre moja tu ya underground rail network.
 
Obama wa Bongo
Hapana,tena hapana,napenda wote waone waseme hapana. Mwezi uliopita nilikuwa China Mji mmoja mdogo kabisa jimbo la Si chuan, haya mambo ya kawaida kabisa kwao, tena ni treni za chini ya ardhi kutoka say Mbezi hadi Posta,ni kama 25km urefu.

Treni inakimbia 260km/hr.kwasababu kuna vituo kama 8 kutoka kituo cha kwanza hadi cha mwisho speed inafikia say 140km inakuwa tayari imeshafika kituo kingine.

Haya yanawezekana kabisa,Au waweke fly over za j uu,mji huo huo kuna TWO WAY 20km Fly over,ni cement na Nondo tuu, ndo zimetumika. Tena so simple unaanza na nguzo tuu, wao walitumia 3years kukamilisha hizo 20km za juu.

Hapa issu ni NIA TUUU.
 
Last edited by a moderator:
FRANCIS DA DON
Kutokuwa na miundombinu bora imetokana na akili chache na pia umaskini uliokithiri hasa siku zilizopita. Unajua flyover sio kitu ambacho hakipo kabisa na pia utakubali kwamba flyover zilizopo zipo nje ya Dar ambapo pana mahitaji makubwa

Kwa mfano pale karibu na Kibaha kuna flyover ya treni, ukiwa maeneo ya Same Kili kuna flyover ya treni na huko porini kuelekea Ifakara pia ipo.

Yote yalifanywa na wazungu miaka ile ya nineteen kweusi, sasa alipokuja mswahili hakuona kwanini afanye zaidi ya hayo.

Unajua kwamba miji kama Tanga, dar, Moshi, Arusha na kadhalika ilikuwa mizuri zaidi ilivyo sasa kwa miundombinu yake enzi za mzungu miaka ya 1930!?

Tutafika tu ila yahitaji muda kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Chini ya CCM, hakitowezekana chochote. Kama hata kujenga vyoo wanategemea wafadhili, wataweza kujenga fly over hao au CCM? Hiyo nchi ni unique hiyo! U can't find anywhere under the sun nchi yenye mipango bogus kama hiyo.
 
Umeme shida, pia planning nayo tatizo.

Hakuna political will and comitment.
 
TRL inatushinda. Je haya mambo makubwa? Enzi za TRC route zilikuwa kibao. Utendaji wa sasa ni kurudisha nyuma mipango.
 
Back
Top Bottom