pepsin
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 3,486
- 6,172
Serikali ipo mbioni kujenga chanzo kikubwa cha kuzalisha umeme ndani ya Hifadhi ya Seleou.Ni kwamba 1/3 ya eneo lote litatumika.Naunga mkono serikali kujiamulia namna nzuri ya kujiletea maendeleo kwa kutumia rasilimali zake bila kuingiliwa na wazungu.Tanzania ya "viwanda" bila shaka inahitaji umeme zaidi.Hofu yangu ni;
1.Environmental Impact Assessment ilifanyika siku nyingi,1980's.Hatujambiwa kama kuna ecological na economical divergences zilizotokea kwa kipindi hichi kirefu.
2.Tuliaminishwa kuwa ungunduzi wa gasi asilia ungetatua matatizo yote ya umeme nchini na tungeuza ziada nje.Sijui nini kimetokea mpaka tuanze kutaka kutafuta reserve zingine ambazo labda zina athari za ki ecologia na kimazingira.
3.Tuliambiwa nchi ina mkondo wa upepo huko Singida ambao ungeweza kuzalisha umeme mwingi,na kazi ni kuweka tu mitambo ya kubadilisha nishati moja kwenda nyingine.Hatuambiwi huu upepo unaleta faida gani kiasi kwamba tuendelee "kuufuga" bila kuutumia.
4.Jua linawaka sana Tanzania,kwanini hatulitumii kutengenezea umeme mpaka tuharibu vyanzo vyetu vingine vya kiuchumi kwa kujenga hilo Stigler's gorge? Huwa inaniumiza sana kuona backup ya umeme kwenye taasisi nyingi ni majenereta yanayotumia mafuta mengi badala ya kuweka solar pannels.
Naishauri serikali iangalie potentiality ya fursa zote za kuzalisha umeme kabla ya kuanza kuchimba huko Seleou.
Kama umeme wa gesi tulioaminishwa tutauza nje haujatosheleza ndani,je,tuamini wa Stigler's gorge utatosheleza au ni kudanganyana tu!
1.Environmental Impact Assessment ilifanyika siku nyingi,1980's.Hatujambiwa kama kuna ecological na economical divergences zilizotokea kwa kipindi hichi kirefu.
2.Tuliaminishwa kuwa ungunduzi wa gasi asilia ungetatua matatizo yote ya umeme nchini na tungeuza ziada nje.Sijui nini kimetokea mpaka tuanze kutaka kutafuta reserve zingine ambazo labda zina athari za ki ecologia na kimazingira.
3.Tuliambiwa nchi ina mkondo wa upepo huko Singida ambao ungeweza kuzalisha umeme mwingi,na kazi ni kuweka tu mitambo ya kubadilisha nishati moja kwenda nyingine.Hatuambiwi huu upepo unaleta faida gani kiasi kwamba tuendelee "kuufuga" bila kuutumia.
4.Jua linawaka sana Tanzania,kwanini hatulitumii kutengenezea umeme mpaka tuharibu vyanzo vyetu vingine vya kiuchumi kwa kujenga hilo Stigler's gorge? Huwa inaniumiza sana kuona backup ya umeme kwenye taasisi nyingi ni majenereta yanayotumia mafuta mengi badala ya kuweka solar pannels.
Naishauri serikali iangalie potentiality ya fursa zote za kuzalisha umeme kabla ya kuanza kuchimba huko Seleou.
Kama umeme wa gesi tulioaminishwa tutauza nje haujatosheleza ndani,je,tuamini wa Stigler's gorge utatosheleza au ni kudanganyana tu!