Kukaa tu hata ukiweka mti unakaa tatizo mzigo unaokuja juu naona hatutaelewana Mimi ni mjenzi mtaalamu ninafahamu ninachosema bahati mbaya sifanyi kazi za nondo mbili nitakutupia kazi yakoMbili zinakaa fresh tu acha ubishi.
Kikanuni kabisa inatakiwa 4.
Ila kiuchumi ndio mtu inabidi ubane tu matumizi.
Sasa asiposuka zitakaaje ∆ ?Nondo 3 zinafaa kabisa, lakini ziwe za mm 12, asije kukushauri uweke mm 10 hazitafaa. Hizo za mm 12 azisuke katika umbo la pembe 3 (yaani mbili chini kwenye base ya linter na moja juu, yaani ikae umbo la pyramid) lengo hapa ni kupata balance), fundi anaweza akazisuka na binding wire au anaweza asisuke pia; inategemea na ustadi wake katika kuzipanga inavyotakiwa. Mimi nimejenga nyumba yangu kubwa tu ya room 3, sebule kubwa tu, dining, jiko na store; na linter yake nimetumia nondo 3 za mm 12, juu ya linter nimeweka tofali za course 3, so naelezea kitu nnachokifahamu.
Sasa asiposuka zitakaaje ∆ ?
Ndio.umeona nondo ni urembo katika nyumba
Sasa unabishana na mimi niliyeshuhudia!? Ninakisema nimekishuhudia sikurupuki.Acheni uongo nondo mbili zinawezaje kugawanya mgandamizo na kustahimili kani ya nguvu ya mzigo?
Haya umeshindaSasa unabishana na mimi niliyeshuhudia!? Ninakisema nimekishuhudia sikurupuki.
Huko kweru ni moja tu mkuuHabari wakuu,katika kubana matumizi fundi kaniambia ujenzi wa lenta kwa kusuka nondo 3 unafaa,naomba ushauri wananzengo
Spring nzuri na imara hivyo??? Kuna jamaa aliwaachia mafundi hela kumbe badala ya nondo wameweka mirunda............ALIJUAJE????....siku moja ameita mafundi waongeze rumu kwa nje kwa kuattach kwenye main house .....jamaa wamefikia usawa was lenta wanatindua ili waunganishe nondo....wanakutana na mirunda!!!!!!!!Wewe utakufa kwa kuangukiwa na paa ukiwa umelala
Kachukue kijana mwenye diploma tu atakuchorea nyumba na kukuwekea gharama za ujenzi kwa bei nafuu
Kwa njaa yake huyo fundi kuna siku atakuambia mtumie springi za malori badala ya nondo
Msingi wa mawe unagharama kubwa ukilinganisha na msingi wa matofali gharama za msingi wa mawe huwa kwenye saruji, na gharama za ujenz kwa fund, ila ni imara zaid kama mawe yamepangwa vizur na fundi mzur. Msing wa matofali hauna gharama zaid ila ni hafifu sana ukilinganisha na wamaweHivi sehemu iliyo tambarare kati ya kuweka msingi Wa mawe na Matofali upi bora? Na upi unaokoa gharama?
Ukizifunga kwa mtindo wa pembe tatu sawa pande zote...bado symmetry haipatikani?Kitaalamu haufai kabisa.
Kwa sababu hiyo lenta(linta) ndiyo inapokea mzigo kutoka juu na kuleta msawazo wa jengo lako. Kwa sababu linta inapokea mzigo inatakiwa iipokee kwa usawa.
Kwanza kazi ya nondo ni nini kwenye linta??
Kazi ya nondo kwenye linta ni kuzuia kani(force) za mvutano ndani ya jengo lako!
Kwa nini sasa nondo tatu hazifai??
Ni kwa sababu standards zinashauri nondo lazima zifungwe symmetrically arranged. Ili zinapopokea mzigo na kuusambaza uwe sawa sawa.
Nondo tatu siyo symmetrically arranged. Sasa mzigo ukizidi kudogo tuu, jengo unaanza kuliona limeeanza nyufa na hata hiyo linta unaanza kuiona inapinda.
Suluhisho!
Ongeza nondo nyingine ziwe nne ili angalau ulete msawazo wa upokeaji wa mzigo na usambazaji wake.
Pia weka na nguzo kwenye kila kina na maungio ya jengo lako (kama ni nyumba kubwa na unataka idumu muda mrefu).
Ila kama ni banda tuu, komaa na aina ya ujenzi wako. Ila kama ni dream house, fuata hako kaushauri.
Jiandae kuangukiwa na nyumba.Unazikata na kuzitandaza kabisa kule kwenye box za linter, wakati unamwaga zege ndo unazinyanyua zikae ktk umbo hilo sasa. Niliona fundi wangu anafanya hivyo.
Ndio nataka kufanya hivi na mimi, 2 za mm 12 kwenye msingi wa mawe na tatu kwenye lintelYah itakuwa bora,nadhani wengi ndo tunavyoweka mimi niliweka mbili kwenye kiuno cha msingi lintel nikaweka tatu nyumba ilinyeshewa mvua siyo chini ya miaka saba na sehemu niliyojenga palikuwa na udongo wa mfinyanzi ila nyumba haikupata crack yoyote.