Ujenzi wa barabara za 'flyovers' Dar kuanza Septemba 2014

Ujenzi wa barabara za 'flyovers' Dar kuanza Septemba 2014

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,933
TazaraBomba(2).png

Mafundi wa kampuni ya ujenzi ya RJR wakiwa kazini kwenye
makutano ya barabara za Mandela na Nyerere jijini Dar es Salaam

10437337_10152416897224857_57971254973257182_n.jpg

Flyover inayotazamiwa kuoteshwa hapo makutano ya Mandela na Nyerere (TAZARA)


Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), Mhandisi Patrick Mfugale, amesema ujenzi wa barabara zipitazo juu (flyover) kati ya Mandela na Nyerere utaanza rasmi mwezi Septemba mwaka huu. Katika mahojiano na NIPASHE Jumapili, mhandisi Mfugale, alisema ujenzi huo utaanza mara baada ya kukamilika kuondoa nguzo za umeme na mabomba ya maji, zoezi ambalo linaendelea hivi sasa.

NIPASHE ilifika jana eneo hilo ambalo litajengwa barabara hizo na kukuta makandarasi wakiendelea na zoezi la kuhamisha mabomba. Akizungumza na gazeti hili, Msimamizi wa zoezi hilo, Peter Mitondo, tayari wamekamilisha uondoaji wa mabomba ndani ya Tazara na sasa wapo kwenye barabara kuu za magari.

Alisema uhamishaji huo wa mabomba ya maji kwenye barabara ya Tazara ili kupisha ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.

Alipoulizwa ujenzi huo utachukua muda gani kukamilika, msimamizi huyo alisema hafahamu kwa kuwa mkandarasi atakayehusika atakuwa mwingine. Alisema mkandarasi wa sasa anayehusika kwenye kuyaondoa mabomba hayo ya maji ni kampuni za pamoja ambazo ni RJR, RJ na Jos Harsen.

Source: Nipashe
 
Jk piga kazi achana na porojo za Bavicha.

Wezi wa EPA wangapi wamesharejesha??!! Na majina vipi yanapatikana kwa watu wa Msoga tu ama???!!

Nina ndugu yangu kafungwa kwa wizi wa kuku,nikimlipia mtamuachia serikali sikivu ama msamaha ni kwa wezi wa multibillion tu??!!
 
Rais Kikwete anamaliza kipindi chake kama vile anaanza vile....

I wish angeongezewa miaka mingine miwili tu na kwetu Iringa tungekuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa.

Halafu utasikia wale mbulumundu wakidai hakuna maendeleo, sijui maendeleo maana yake nini???
 
treni ya mwakiembe imeishia wapi kwanza kabla ya kuongelea hayooo
 
Jk piga kazi achana na porojo za Bavicha.
Kazi kwenda kukopa?

Escrow ac inatosha kutegeneA fly over katika junction za dar zote.

Kazi gani ya kumleta Terrence?

Kaz kuhudhuria misiba?
 
Rais Kikwete anamaliza kipindi chake kama vile anaanza vile....

I wish angeongezewa miaka mingine miwili tu na kwetu Iringa tungekuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa.

Halafu utasikia wale mbulumundu wakidai hakuna maendeleo, sijui maendeleo maana yake nini???
Maendeleo ni kumleta Terrence nankwenda kukopa
 
Wezi wa EPA wangapi wamesharejesha??!! Na majina vipi yanapatikana kwa watu wa Msoga tu ama???!!

Nina ndugu yangu kafungwa kwa wizi wa kuku,nikimlipia mtamuachia serikali sikivu ama msamaha ni kwa wezi wa
multibillion tu??!!
Na wale wa 10% sijui hapa watachukua ngapi yarabii!
 
Mimi nadhani maendeleo ni kujikopesha ruzuku na kukiuizia cahama migari mibovu kwa bei mbaya sana. Bila kusahau kujilipa mshahara mkubwa sana huku ukidai kuwa ukiupata urais utakula mihogo ili uchumi ukue...

Mkuu umenichekesha sana,mwingine kaenda ulaya kalia asaidiwe ambulance ya jimbo lake, amepewa tamaa ikamtawala na kuziuza, pesa anajenga ghorofa lake njiro, ndiyo maendeleo yao.
 
treni ya mwakiembe imeishia wapi kwanza kabla ya kuongelea hayooo

Pengine tunaelekea kufikiria njia za mkato kuondoa msongamano wakati tatizo lisitatuliwe. Dar hakuna magari mengi ya kutisha isipokuwa barabara ni chache na pengine barabara zote kuwa karibu mjini tu wakati kuna wakazi wengi pembezoni mwa jiji kunakotakiwa kujengwa barabara za kutosha za kutoka na kuingia pia barabara kubwa inayozunguka jiji kama belt way.
 
nionavyo mm kabla ya kukurupuka na miradi mikubwa ya hivyo ilikuwa busara kwa kuhakikisha miundombinu (barabara) ya maeneo mengine imekaa vizuri mfano hakuna barabara za kueleweka kitunda, kivule, goba, makongo, temeke, na kwingineko miradi ambayo ingecgukua pesa kidogo na ingenufaisha wengi kuliko kujionesha kwa mradi mmoja mkubwa kama huo ambao hautokuwa na faida kubwa ukiacha sifa.
 
Flyover mnazitaja kienyeji enyeji tu
Brazili zinadondoka na hamna uchakachuaji hapa kwetu si zitakuwa kaburi?
Barabara za chini bado zinatushinda tunakimbilia za juu haya ni maajabu ya dunia
Labda uniambie wanataka kuweka kamoja kakuombea kura 2015
 
Tanzania ijayo hiyo mjukuu wangu atafaidi,
Ila barabara za chini ni bora kuliko hizo flyover.
 
Yaani vitu ambavyo ni vya msingi serikali kuvifanya sisi tunaona extraordinary...

Ndio maana hawa wanasiasa vimburukutu wataendelea kuwatumia Watanzania kama misukule vile...
 
Back
Top Bottom