Mpingapumba
Member
- Nov 28, 2012
- 33
- 4
Kama za chini zimewashinda ndo za juu wataweza wasije sababisha maafa mana za chini hazimalizi mwezi zinakuwa na mashimo watengeneze kwanza za chini kwa viwango vizuri
kabisa yani
Kama za chini zimewashinda ndo za juu wataweza wasije sababisha maafa mana za chini hazimalizi mwezi zinakuwa na mashimo watengeneze kwanza za chini kwa viwango vizuri
Kinachofanyika sasa hivi ni kuongeza wimbi la magari kujazana mjini badala ya kuandaa barabara nyingi pembezoni mwa jiji ambako kuna wakazi wengi na pia kuandaa belt way ambayo ingekuwa kwa kiwango cha divided way with three or four lanes kila upande kuanzia Mbezi Beach - Mbezi Juu - Pugu - Mbagala hadi Kigamboni. Kisha barabara nyingine kadhaa zinazoungana na hiyo toka mjini. Hilo lingekuwa suluhisho la kupunguza msongamano na magari yangekuwa yanapendelea huko kwenye barabara ya kwenda haraka na kasi badala ya mjini ambako kuna ucheleweshaji wa foleni na mataa.
Just thinking deep...sehem ipi inahitaji ufanisi zalidi/pana abiria wengi JNIA au Stand ya Ubungo?and how Abt traffic light,magari yanayotoka kwa kasi kwenye izo flying over si yatakwenda kujazana kwenye mataa ya ubungo ?au yanayotoka airport,Gomz,vingunguti,kiwalani n.k si yatakwenda kujazana mataa ya chang'ombe?nway it's a gud start,and I real appreciate it but they should have thought beyond that sio solving ya tatzo moja iongeze jingine
Ukitaka kkuona flyover nenda Kenya. hii ya Tazara is a day pipe dream na haita materialize. you can quote me. watch my words
Nchi ambazo walibuni ujenzi wa flyovers ni baada ya kuona hakuna namna nyingine kwa vile barabara zote zimeshajengwa na msongamano unaongezeka. Kwatu tungehitaji kwanza uboreshaji wa barabara za pembezoni ambazo zingevutia waendesha magari kukimbilia huko kukwepa foleni za mjini, lakini kwa kinachoendelea ni sawa na kuongeza tatizo juu ya tatizo.
hilo naloneno mkaka,HAKUNA MAGARI MENGI DARPengine tunaelekea kufikiria njia za mkato kuondoa msongamano wakati tatizo lisitatuliwe. Dar hakuna magari mengi ya kutisha isipokuwa barabara ni chache na pengine barabara zote kuwa karibu mjini tu wakati kuna wakazi wengi pembezoni mwa jiji kunakotakiwa kujengwa barabara za kutosha za kutoka na kuingia pia barabara kubwa inayozunguka jiji kama belt way.
sio kweli....flyover kwenye busy junctions ni kitu muhimu tangu enzi na enzi....pia kwenye highway/motorway exit flyover ni lazima kuruhusu kuingia na kutoka na kubadili barabara bila kusimama na kuathiri flow ya traffic....uboreshe barabara za pembeni au usiboreshe barabara za pembeni flyovers ubungo/tazara/chang'ombe ni muhimu....tena zimechelewa sana.
Baltimore (USA)
Washington DC
DC
London UK
Houston USA

Una ubia naye wa magogoni?Jk piga kazi achana na porojo za Bavicha.
kujenga viwanja vya ndege, kwa shirika gani la ndege? Hata za wenzetu soon zitaishia nchi jirani, sie wa kcc tunaomba ajenge reli.Rais Kikwete anamaliza kipindi chake kama vile anaanza vile....
I wish angeongezewa miaka mingine miwili tu na kwetu Iringa tungekuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa.
Halafu utasikia wale mbulumundu wakidai hakuna maendeleo, sijui maendeleo maana yake nini???
Sijui unamaanisha nini sasa.Tanzania ijayo hiyo mjukuu wangu atafaidi,
Ila barabara za chini ni bora kuliko hizo flyover.
Belt way ni barabara kubwa inayozunguka kandokando ya vitongoji vya jiji ambayo huunganisha route mbalimbali zinazoingaia jijini. Belt way huwa ya kiwango cha express way with meridian divided way. Picha hapo chini kwa baadhi ya majiji nchini Marekani na jiji la London ambayo yana beltway kama ninayoongelea.
View attachment 171101 Baltimore (USA) View attachment 171102Washington DCView attachment 171103DCView attachment 171111London UK View attachment 171112Houston USA
Flyovers kwenye makutano ya highway nchini Marekani.
View attachment 171105 View attachment 171106 View attachment 171107 View attachment 171108 View attachment 171109 View attachment 171110
Flyover zilizo nyingi ni zile ambazo zinaunganisha barabara kuu zaidi ya moja ambapo huwa na ramp ways za kutokea na kuingilia. Barabara za kawaida hazina flyover isipokuwa chache ambazo kuna sababu maalumu au zinakatisha highway au express way.
Walichojitahidi ni kujenga barabara nzuri na zinazovutia kuendesha kwa raha zaidi nje ya jiji ili kuvutia watu waende huko ili kupunguza msongamano wa magari mjini. Kama kukiwa na events downtown ndo unaona utitiri wa magari vinginevyo watu hupendelea huko kunako beltway kwa sababu wataenda kasi na kufika mapema waendako kuliko usumbufu wa mataa mjini.
Udhaifu wa mipambo miji barabara Dar
Kwa nini magari yamejanaza mjini zaidi kuliko pembezoni mwa jiji na vitongoji vyake?
Hivyo basi hujaona umuhimu wa kuwa na barabara huko pembeni zinazounganisha au kusababisha magari kutojazana mjini?
- Anayetoka Mbagala kwenda Pugu, Kisarawe, Mbezi juu, nk lazima apitie mjini.
- Wa kutoka Kigamboni kwenda sehemu yo yote ya jiji lazima apitie mjini isipokuwa tu kama anaenda Mbagala.
- Anayetoka Bagamoyo, Mbezi beach, na maeneo mengine ya huko lazima apitie mjini kuelekea upande mwingine.
- Wa kutoka Mbezi juu kwenda Mbagala kwanda upande wo wote wa jiji lazima apitie mjini.
tazara junction inaunganisha barabara kubwa jijini dar kama sio tanzania nzima.....kwa hiyo flyover ni lazima ijengwe pale whether utajenga hizo beltway or hutajenga hizo beltway......
umuhimu wa beltway(mimi nimezoea orbital/circular refer M25 au A4O6 london)naujua na inahitajika dar lakini hauondoi umuhimu wa kujenga flyover tazara...we need flyovers kwenye junction zote kubwa zinazounganisha barabara ya mandela/morogoro/kawawa/sam nujoma
Ujenzi unaanza pale project designing inapoanza.., so ujenzi unaweza ukafanyika hata miaka miwili na usione hata nguzo moja ikijengwa.., lakini kumbe ujenzi unaendela kwa kasi sana.., hii hatua unayoona ya kuhamisha mabomba na nguzo ni hatua za mwisho mwisho za ujenzi na ni ishara kwamba ujenzi unakaribia kukamilika.., kazi kubwa ya ujenzi imeshafanywa na project designers.., hawa wanachofanya ni ku-materialize tuu.., which is very simple.., kuwa na imani dogo.Hizo ni hadithi za siku mingi mpaka bungen 2shasikia ilishaanza
Chang’ombe flyover imefikia patamuUjenzi unaanza pale project designing inapoanza.., so ujenzi unaweza ukafanyika hata miaka miwili na usione hata nguzo moja ikijengwa.., lakini kumbe ujenzi unaendela kwa kasi sana.., hii hatua unayoona ya kuhamisha mabomba na nguzo ni hatua za mwisho mwisho za ujenzi na ni ishara kwamba ujenzi unakaribia kukamilika.., kazi kubwa ya ujenzi imeshafanywa na project designers.., hawa wanachofanya ni ku-materialize tuu.., which is very simple.., kuwa na imani dogo.
Kwa hiyo MATAGA waje wasome hapa hizi flyover mnazopiga kelele kwamba amejenga Mungu mfu wenu hazikuanza Jana. Acheni kupotosha umma.Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), Mhandisi Patrick Mfugale, amesema ujenzi wa barabara zipitazo juu (flyover) kati ya Mandela na Nyerere utaanza rasmi mwezi Septemba mwaka huu. Katika mahojiano na NIPASHE Jumapili, mhandisi Mfugale, alisema ujenzi huo utaanza mara baada ya kukamilika kuondoa nguzo za umeme na mabomba ya maji, zoezi ambalo linaendelea hivi sasa.![]()
Mafundi wa kampuni ya ujenzi ya RJR wakiwa kazini kwenye
makutano ya barabara za Mandela na Nyerere jijini Dar es Salaam
![]()
Flyover inayotazamiwa kuoteshwa hapo makutano ya Mandela na Nyerere (TAZARA)
NIPASHE ilifika jana eneo hilo ambalo litajengwa barabara hizo na kukuta makandarasi wakiendelea na zoezi la kuhamisha mabomba. Akizungumza na gazeti hili, Msimamizi wa zoezi hilo, Peter Mitondo, tayari wamekamilisha uondoaji wa mabomba ndani ya Tazara na sasa wapo kwenye barabara kuu za magari.
Alisema uhamishaji huo wa mabomba ya maji kwenye barabara ya Tazara ili kupisha ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.
Alipoulizwa ujenzi huo utachukua muda gani kukamilika, msimamizi huyo alisema hafahamu kwa kuwa mkandarasi atakayehusika atakuwa mwingine. Alisema mkandarasi wa sasa anayehusika kwenye kuyaondoa mabomba hayo ya maji ni kampuni za pamoja ambazo ni RJR, RJ na Jos Harsen.
Source: Nipashe