Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Miaka michache iliyopita tuliwahi kuwa na mazumzo na watu Fulani kuhusu Punguzo la Programu za komputa zinazotumika sana na Watu nchini haswa zile za Kampuni la Microsoft kama Microsoft Office , Microsoft Windows , Kampuni la Autodesk Kwenye AutoCAD na Adobe Kwenye Adobe CS pamoja na nyingine nyingi .
Katika mazungumzo hayo kampuni hizo zilitaka kuwemo Sheria Mtandao na Nyingine za Hati miliki zitakazolinda Programu zao na wateja wao kwanza pindi watakapotumia Programu hizo au Kila Kampuni kuingia Mkataba maalumu na serikali utakaolinda maslahi ya Bidhaa zao nchini kwanza ndio masuala ya Bei na Punguzo nyingine kuongelewa .
Kusema za ukweli uuzaji na usambazaji wa Programu na Leseni Bandia za Programu umechangia kudhoofisha sana maendeleo ya Teknohama nchini pamoja na kukuza misingi ya Wizi wa Milki ya Programu hizo pamoja na Leseni zake .
Sasa hivi kuna watu wengi nchini haswa walio katika taasisi za elimu ya juu wana kosa fursa za kujifunza zaidi masuala mbalimbali ya teknohama kutokana na hali hii ya wizi wa Leseni za Programu mbalimbali na aina nyingine ya Hujuma za Kiteknohama .
Kama umewahi kutembelea vyuo vikuu karibu vyote vya Tanzania na kuangalia aina ya programu wanazotumia kwenye shuguli zao za kila siku na komputa zao wanazitoa wapi na kama program hizo ni halali au batili ?
Je wewe mwenyewe kwenye komputa unayotumia una programu ngapi ambazo si halali na batili au umezipata kupitia mfumo ambao sio sahihi ? labda leseni unayotumia kwenye program hiyo ni ya mtu mwingine ukaweka kwako kwa kujua au bila kujua ?
Je unavyonunua programu kwenye maduka au sehemu zozote zile unajua haki zako za msingi ni zipi ? kama mtumiaji wa program husika je unapata haki zote kama Huduma kwa wateja , Updates Na Kadhalika ?
Wiki hii kumetokea Tukio la Mzaha kidogo lakini la Maumivu sana kwa mfanyabiashara ambapo mfanyakazi mmoja aliiba Leseni/Keys/Product Keys za Progamu zinazouzwa na Kampuni hiyo kisha kwenda kuuza na zingine akaendelea kuwa nazo kwenye Laptop Yake .
Mtu huyo amegundulika baada ya Mmoja ya watu kuuziwa Bidhaa hiyo kwa njia za kienyeji kuichomeka kwenye Mtandao na kugundulika imeuzwa wakati Risiti na Maelezo mengine Hakuna kwenye Hifadhi ya Kampuni .
Ilivyogundulika hivyo mwenye kampuni ilibidi sasa awasiliane na Waliotengeneza Programu hiyo na kutoa leseni zake ili masuala mengine ya kisheria yaweze kuchukuliwa dhidi ya wale waliohusika .
Watengenezaji wa Programu Walitaka kujua kuhusu Sheria Mtandao za Nchi yetu ( CYBERLAWS ) Zile za Hati Miliki na nyingine nyingi ambazo zingeweza kuwaongoza katika kufuatilia suala hili vizuri na kwa haki , hivyo vyote havikuwepo kwahiyo mfanyakazi aliachichwa kazi tu .
Kwa kosa kama hili watengenezaji wa Programu hiyo wanaweza kuvunja mkataba wa usambazaji wa programu zao kwa nchi ya Tanzania kwa watu wanaopenda kuwa mawakala wa kuuza na kusambaza programu husika pamoja na kusitisha misaada mingine inayohusiana na masomo kwa mawakala wa kuuza na kusambaza programu zao
Hilo ni moja ya matukio mengi yanayoendelea nchini ambayo yanasababisha Suala zima la Teknohama kuwa gumu katika maendeleo yake haswa yanapokuja masuala ya Biashara inayohusiana na Programu za Matumizi ya Kawaida ya Watu kama Uchoraji , Ujenzi na masuala mengine ya Uhandisi .
Ndugu zangu jamaa na marafiki pale tunavyojitoa kwa dhati kupambana na Ufisadi na Hujuma nyingine dhidi ya Uchumi na Maisha yetu pia tupambane dhidi ya Ujangili wa Programu na Leseni Bandia Kwa Maslahi yetu .
Serikali inakosa mapato makubwa kutokana na Watu kutonunua Programu hizi kupitia njia halali kwahiyo hawalipi kodi wala makato yoyote , Ajira nyingi zinapotezwa ambapo wale wanaomaliza mavyuo na mashuleni walitakiwa wawe sehemu ya mauzo na usambazaji wa program hizi au utoaji wa huduma kwa wateja .
NA JE HAWA WANAFUNZI WANAOJIFUNZA MASUALA YA UTENGENEZAJI WA PROGRAMU KWENYE VYUO WATAKAA KWENYE SOKO GANI LA AJIRA KAMA MAMBO NDIO YAKO HIVI ?
Katika mazungumzo hayo kampuni hizo zilitaka kuwemo Sheria Mtandao na Nyingine za Hati miliki zitakazolinda Programu zao na wateja wao kwanza pindi watakapotumia Programu hizo au Kila Kampuni kuingia Mkataba maalumu na serikali utakaolinda maslahi ya Bidhaa zao nchini kwanza ndio masuala ya Bei na Punguzo nyingine kuongelewa .
Kusema za ukweli uuzaji na usambazaji wa Programu na Leseni Bandia za Programu umechangia kudhoofisha sana maendeleo ya Teknohama nchini pamoja na kukuza misingi ya Wizi wa Milki ya Programu hizo pamoja na Leseni zake .
Sasa hivi kuna watu wengi nchini haswa walio katika taasisi za elimu ya juu wana kosa fursa za kujifunza zaidi masuala mbalimbali ya teknohama kutokana na hali hii ya wizi wa Leseni za Programu mbalimbali na aina nyingine ya Hujuma za Kiteknohama .
Kama umewahi kutembelea vyuo vikuu karibu vyote vya Tanzania na kuangalia aina ya programu wanazotumia kwenye shuguli zao za kila siku na komputa zao wanazitoa wapi na kama program hizo ni halali au batili ?
Je wewe mwenyewe kwenye komputa unayotumia una programu ngapi ambazo si halali na batili au umezipata kupitia mfumo ambao sio sahihi ? labda leseni unayotumia kwenye program hiyo ni ya mtu mwingine ukaweka kwako kwa kujua au bila kujua ?
Je unavyonunua programu kwenye maduka au sehemu zozote zile unajua haki zako za msingi ni zipi ? kama mtumiaji wa program husika je unapata haki zote kama Huduma kwa wateja , Updates Na Kadhalika ?
Wiki hii kumetokea Tukio la Mzaha kidogo lakini la Maumivu sana kwa mfanyabiashara ambapo mfanyakazi mmoja aliiba Leseni/Keys/Product Keys za Progamu zinazouzwa na Kampuni hiyo kisha kwenda kuuza na zingine akaendelea kuwa nazo kwenye Laptop Yake .
Mtu huyo amegundulika baada ya Mmoja ya watu kuuziwa Bidhaa hiyo kwa njia za kienyeji kuichomeka kwenye Mtandao na kugundulika imeuzwa wakati Risiti na Maelezo mengine Hakuna kwenye Hifadhi ya Kampuni .
Ilivyogundulika hivyo mwenye kampuni ilibidi sasa awasiliane na Waliotengeneza Programu hiyo na kutoa leseni zake ili masuala mengine ya kisheria yaweze kuchukuliwa dhidi ya wale waliohusika .
Watengenezaji wa Programu Walitaka kujua kuhusu Sheria Mtandao za Nchi yetu ( CYBERLAWS ) Zile za Hati Miliki na nyingine nyingi ambazo zingeweza kuwaongoza katika kufuatilia suala hili vizuri na kwa haki , hivyo vyote havikuwepo kwahiyo mfanyakazi aliachichwa kazi tu .
Kwa kosa kama hili watengenezaji wa Programu hiyo wanaweza kuvunja mkataba wa usambazaji wa programu zao kwa nchi ya Tanzania kwa watu wanaopenda kuwa mawakala wa kuuza na kusambaza programu husika pamoja na kusitisha misaada mingine inayohusiana na masomo kwa mawakala wa kuuza na kusambaza programu zao
Hilo ni moja ya matukio mengi yanayoendelea nchini ambayo yanasababisha Suala zima la Teknohama kuwa gumu katika maendeleo yake haswa yanapokuja masuala ya Biashara inayohusiana na Programu za Matumizi ya Kawaida ya Watu kama Uchoraji , Ujenzi na masuala mengine ya Uhandisi .
Ndugu zangu jamaa na marafiki pale tunavyojitoa kwa dhati kupambana na Ufisadi na Hujuma nyingine dhidi ya Uchumi na Maisha yetu pia tupambane dhidi ya Ujangili wa Programu na Leseni Bandia Kwa Maslahi yetu .
Serikali inakosa mapato makubwa kutokana na Watu kutonunua Programu hizi kupitia njia halali kwahiyo hawalipi kodi wala makato yoyote , Ajira nyingi zinapotezwa ambapo wale wanaomaliza mavyuo na mashuleni walitakiwa wawe sehemu ya mauzo na usambazaji wa program hizi au utoaji wa huduma kwa wateja .
NA JE HAWA WANAFUNZI WANAOJIFUNZA MASUALA YA UTENGENEZAJI WA PROGRAMU KWENYE VYUO WATAKAA KWENYE SOKO GANI LA AJIRA KAMA MAMBO NDIO YAKO HIVI ?