Ujane unapotumika kuhalalisha uvivu/umaskini

Ujane unapotumika kuhalalisha uvivu/umaskini

educator2025

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2013
Posts
403
Reaction score
464
Naelewa kuondokewa na mwenzi wa maisha inauma na kubadilisha muelekeo wa maisha. Sasa hiv kumezuka hali ya wanawake waliofiwa na waume zao (Wajane) kutumia hali yao ya kuwa wajane kulia lia ooh mimi mjane mimi mjane! huku hajishughulishi.

Hivi majuzi stendi ya Mwenge kulikuwa na bomoa bomoa sasa wameibuka kina mama wanajiita "WAJANE" eti kwanini serikali imewabomolea wakati wao ni wajane.

Kuwa mjane sio maana yake ufanye vitu kiholela bila kufuata sharia. KUWA MJANE SI TIKETI YA KUWA MVIVU na KULALAMA TU. KAMATA FURSA sahau yaliyopita. SONGA MBELE.
 
Ni kweli watu wengine wamechukulia situation ya kufiwa na wenzao/wazazi kama kisingizio cha kutojishughulisha. mimi nawafahamu watu waliofanikiwa pamoja na kufiwa na waume zao au wazazi wao. WATANZANIA tuache kulalamika tu TUCHUKUE HATUA
 
Wengi wao ni wajane mchana tu. Nyumba ya pazia chungulia.
 
mbona mama rwakatare ni mjane na katoka kimaisha. japo source ya utajiri wake siijui ka kweli lakini amejitahid haswaa hata kama ni kweli anauza sembe.
 
Umetumia neno sharia badala ya sheria sichangii tena full kifuchefu
 
Ukitembelea sehemu za Moshi/Arusha hata Nairobi utagundua wafanyabiashara nyingi (kubwa na ndogo) ni KINAMAMA wanaume ni kama hawapo, HONGERENI KASKAZINI na wa-KENYA hasa Wakikuyu
 
Umetumia neno sharia badala ya sheria sichangii tena full kifuchefu
Wazee wakutokwa povu kupigania dini ziluzokuja na meli,babu zenu wakagawa ardhi,utu,madini na kila kitu chao wakapewa hizo dini.
Sheria ni neno lenye asili ya kiarabu na neno lake la asili ni hilo "Sharia", sasa kama linakukereketa anza kutumia kiingereza maana maneno ya kiarabu kwenye kiswahili yako mengi balaa.jina tu la lugha ni neno la kiarabu.upo somoo?
 
Igeni mfano wa wajane toka MACHAME wako ngangari mpaka raha.
Cc. MISS Chagga
 
Ila hata vitabu vitakatifu vimeandik din nzuri ni kuwasaidia mayatima,wajane na etc...ila asiefanya kazi na asile...
 
mbona mama rwakatare ni mjane na katoka kimaisha. japo source ya utajiri wake siijui ka kweli lakini amejitahid haswaa hata kama ni kweli anauza sembe.
Labda km amefariki baadaye lkn waliachana kila mtu akashika njia yake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom