Mkurabitambo
JF-Expert Member
- Feb 3, 2010
- 230
- 57
WATU wanaodhaniwa
kuwa ni majambazi
wamevamia na kutumia
mbinu za uhalifu wa
hali ya juu na kupora
magunia ya fedha
kutoka Benki ya
Biashara ya Afrika
(CBA), iliyopo barabara
ya Nyerere, jijini Dar es
Salaam.
Tukio hilo linaloweza
kufananishwa na filamu
za kimafia, lilitokea
jana kati ya saa 2.30 na
saa 2.45 asubuhi.
Waliondoka na magunia
hayo wakiwa
wameyapakia kwenye
magari yao ya kifahari,
bila kuua wala kujeruhi
mtu.
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar
es Salaam, Suleiman
Kova alithibitisha tukio
hilo na kusema fedha
walizoiba zinakadiriwa
kuwa zaidi ya Sh400
milioni.
Hatufahamu kiasi
kamili lakini,
tulivyowahoji maofisa
wa benki wanasema ni
zaidi ya Sh400 milioni
ambazo zimeibiwa,
alisema Kova.
Alifafanua kwamba
tayari meneja wa benki,
msaidizi wake na mlinzi
aliyekuwa zamu
wanashikiliwa na polisi
kwa ajili ya mahojiano.
Mashuhuda
Baadhi ya mashuhuda
wa tukio hilo walisema
watuhumiwa hao wa
ujambazi, waliingia
kwenye benki hiyo,
huku wakiwa wamevalia
vitambusho vya benki
kujifafanisha na
wafanyakazi wa benki
hiyo, mbinu ambayo
iliwahadaa watu
waliokuwa kwenye eneo
hilo wasishtuke kwa
lolote.
Vitambulisho hivyo
viliwafanya walinzi wa
benki hiyo kutokuwa na
wasiwasi na
watuhumiwa hao,
jambo lilitoa fursa kwao
kutekeleza uhalifu
katika mazingira ya
urahisi zaidi.
Baada ya kuingia ndani
ya benki, majambazi
hao wakiwa na bastola
yaliwaweka chini ya
ulinzi walinzi wa benki
hiyo .
Wakati hayo yakitokea
mmoja wa majambazi
hao aliamuru
wafanyakazi wa benki
hiyo kuendelea
kuwakaribisha wateja
wao na kila aliyekuwa
akiingia aliwekwa chini
ya ulinzi.
Mtuhumiwa mwingine
wa ujambazi akiwa na
bastola, alimfuata
mtunza funguo wa
chumba maalum cha
kuhifadhia fedha na
chumba cha Mashine za
Kutolea Fedha (ATM) na
kumwambia, atoe
funguo.
Tena jambazi huyo
alimtaja kwa jina
mtunza funguo huku
akisema naomba
funguo za strong room
tumekuja kuchukua
fedha zetu, alisema
mmoja wa mashuhuda
akimkariri jambazi huyo
na kusema alipewa
funguo bila kizuizi.
Baadaye majambazi hao
walifanikiwa kufungua
kwenye vyumba hivyo
na kuchukua fedha zote
na, kuzihifadhi kwenye
magunia manne.
Wakati shughuli hiyo
ikiendelea majambazi
wengine waliharibu
mitambo ya kamera
zinazoonyesha watu
wanaoingia na kutoka
kwenye benki hiyo.
Tunajua mnaturekodi
kwenye kamera zenu na
sisi tunaifahamu vizuri
teknolojia hii, ndiyo
maana tunalazimika
kuharibu mtandao
mzima, mmoja wa
jambazi alikaririwa
akisema huku akifungua
mtambo wa kamera.
Baada ya kumaliza
kuharibu mitambo ya
kamera, waliondoka na
maguni ya fedha na
kwenda walikoegesha
magari yao ya kifahari
na kupakia.
Walioshuhudia
walisema, majambazi
hao walikuwa
wakitumia magari
matatu ya aina ya
Toyota Land Cruiser,
Nissan Patrol na Toyota
Noah na kwamba,
wakati wakitekeleza
ujambazi huo madereva
wote walikuwa
wamebaki kwenye
magari hayo yaliyokuwa
yameegeshwa karibu na
benki hiyo.
Baada ya magari hayo
kupakia magunia hayo,
madereva hao
waliyaondoa magari
hayo kwa kasi kuelekea
eneo la katikati ya jiji.
Wameendelea kusema
kwamba wakati
majambazi hayo
yanaondoka katika
eneo hilo mnamo saa
2.45 asubuhi, hakukuwa
na msongamano wa
magari katika barabara
ya Nyerere kama
kawaida.
Unafahamu muda huu
eneo hili huwa na
msongamano wa magari
lakini, tunashangaa
wakati tukio hili
linatokea hakukuwa na
magari hadi tukadhani
labda kuna msafara wa
viongozi, alisema
mmoja wa mashuhuda.
Baada ya tukio hilo
kumalizika maofisa wa
Jeshi la Polisi walifika
katika benki hiyo
iliyopo kwenye jengo la
Jamana wakiongozwa
na Kamanda wa Kanda
Maalum ya Mkoa wa
Dar es Salaam,
Suleiman Kova.
kuwa ni majambazi
wamevamia na kutumia
mbinu za uhalifu wa
hali ya juu na kupora
magunia ya fedha
kutoka Benki ya
Biashara ya Afrika
(CBA), iliyopo barabara
ya Nyerere, jijini Dar es
Salaam.
Tukio hilo linaloweza
kufananishwa na filamu
za kimafia, lilitokea
jana kati ya saa 2.30 na
saa 2.45 asubuhi.
Waliondoka na magunia
hayo wakiwa
wameyapakia kwenye
magari yao ya kifahari,
bila kuua wala kujeruhi
mtu.
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar
es Salaam, Suleiman
Kova alithibitisha tukio
hilo na kusema fedha
walizoiba zinakadiriwa
kuwa zaidi ya Sh400
milioni.
Hatufahamu kiasi
kamili lakini,
tulivyowahoji maofisa
wa benki wanasema ni
zaidi ya Sh400 milioni
ambazo zimeibiwa,
alisema Kova.
Alifafanua kwamba
tayari meneja wa benki,
msaidizi wake na mlinzi
aliyekuwa zamu
wanashikiliwa na polisi
kwa ajili ya mahojiano.
Mashuhuda
Baadhi ya mashuhuda
wa tukio hilo walisema
watuhumiwa hao wa
ujambazi, waliingia
kwenye benki hiyo,
huku wakiwa wamevalia
vitambusho vya benki
kujifafanisha na
wafanyakazi wa benki
hiyo, mbinu ambayo
iliwahadaa watu
waliokuwa kwenye eneo
hilo wasishtuke kwa
lolote.
Vitambulisho hivyo
viliwafanya walinzi wa
benki hiyo kutokuwa na
wasiwasi na
watuhumiwa hao,
jambo lilitoa fursa kwao
kutekeleza uhalifu
katika mazingira ya
urahisi zaidi.
Baada ya kuingia ndani
ya benki, majambazi
hao wakiwa na bastola
yaliwaweka chini ya
ulinzi walinzi wa benki
hiyo .
Wakati hayo yakitokea
mmoja wa majambazi
hao aliamuru
wafanyakazi wa benki
hiyo kuendelea
kuwakaribisha wateja
wao na kila aliyekuwa
akiingia aliwekwa chini
ya ulinzi.
Mtuhumiwa mwingine
wa ujambazi akiwa na
bastola, alimfuata
mtunza funguo wa
chumba maalum cha
kuhifadhia fedha na
chumba cha Mashine za
Kutolea Fedha (ATM) na
kumwambia, atoe
funguo.
Tena jambazi huyo
alimtaja kwa jina
mtunza funguo huku
akisema naomba
funguo za strong room
tumekuja kuchukua
fedha zetu, alisema
mmoja wa mashuhuda
akimkariri jambazi huyo
na kusema alipewa
funguo bila kizuizi.
Baadaye majambazi hao
walifanikiwa kufungua
kwenye vyumba hivyo
na kuchukua fedha zote
na, kuzihifadhi kwenye
magunia manne.
Wakati shughuli hiyo
ikiendelea majambazi
wengine waliharibu
mitambo ya kamera
zinazoonyesha watu
wanaoingia na kutoka
kwenye benki hiyo.
Tunajua mnaturekodi
kwenye kamera zenu na
sisi tunaifahamu vizuri
teknolojia hii, ndiyo
maana tunalazimika
kuharibu mtandao
mzima, mmoja wa
jambazi alikaririwa
akisema huku akifungua
mtambo wa kamera.
Baada ya kumaliza
kuharibu mitambo ya
kamera, waliondoka na
maguni ya fedha na
kwenda walikoegesha
magari yao ya kifahari
na kupakia.
Walioshuhudia
walisema, majambazi
hao walikuwa
wakitumia magari
matatu ya aina ya
Toyota Land Cruiser,
Nissan Patrol na Toyota
Noah na kwamba,
wakati wakitekeleza
ujambazi huo madereva
wote walikuwa
wamebaki kwenye
magari hayo yaliyokuwa
yameegeshwa karibu na
benki hiyo.
Baada ya magari hayo
kupakia magunia hayo,
madereva hao
waliyaondoa magari
hayo kwa kasi kuelekea
eneo la katikati ya jiji.
Wameendelea kusema
kwamba wakati
majambazi hayo
yanaondoka katika
eneo hilo mnamo saa
2.45 asubuhi, hakukuwa
na msongamano wa
magari katika barabara
ya Nyerere kama
kawaida.
Unafahamu muda huu
eneo hili huwa na
msongamano wa magari
lakini, tunashangaa
wakati tukio hili
linatokea hakukuwa na
magari hadi tukadhani
labda kuna msafara wa
viongozi, alisema
mmoja wa mashuhuda.
Baada ya tukio hilo
kumalizika maofisa wa
Jeshi la Polisi walifika
katika benki hiyo
iliyopo kwenye jengo la
Jamana wakiongozwa
na Kamanda wa Kanda
Maalum ya Mkoa wa
Dar es Salaam,
Suleiman Kova.