ujambazi CBA Nyerere Rd: Picha kamili

Mkurabitambo

JF-Expert Member
Feb 3, 2010
230
57
WATU wanaodhaniwa
kuwa ni majambazi
wamevamia na kutumia
mbinu za uhalifu wa
hali ya juu na kupora
magunia ya fedha
kutoka Benki ya
Biashara ya Afrika
(CBA), iliyopo barabara
ya Nyerere, jijini Dar es
Salaam.
Tukio hilo linaloweza
kufananishwa na filamu
za kimafia, lilitokea
jana kati ya saa 2.30 na
saa 2.45 asubuhi.
Waliondoka na magunia
hayo wakiwa
wameyapakia kwenye
magari yao ya kifahari,
bila kuua wala kujeruhi
mtu.
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar
es Salaam, Suleiman
Kova alithibitisha tukio
hilo na kusema fedha
walizoiba zinakadiriwa
kuwa zaidi ya Sh400
milioni.
“Hatufahamu kiasi
kamili lakini,
tulivyowahoji maofisa
wa benki wanasema ni
zaidi ya Sh400 milioni
ambazo zimeibiwa,”
alisema Kova.
Alifafanua kwamba
tayari meneja wa benki,
msaidizi wake na mlinzi
aliyekuwa zamu
wanashikiliwa na polisi
kwa ajili ya mahojiano.
Mashuhuda
Baadhi ya mashuhuda
wa tukio hilo walisema
watuhumiwa hao wa
ujambazi, waliingia
kwenye benki hiyo,
huku wakiwa wamevalia
vitambusho vya benki
kujifafanisha na
wafanyakazi wa benki
hiyo, mbinu ambayo
iliwahadaa watu
waliokuwa kwenye eneo
hilo wasishtuke kwa
lolote.
Vitambulisho hivyo
viliwafanya walinzi wa
benki hiyo kutokuwa na
wasiwasi na
watuhumiwa hao,
jambo lilitoa fursa kwao
kutekeleza uhalifu
katika mazingira ya
urahisi zaidi.
Baada ya kuingia ndani
ya benki, majambazi
hao wakiwa na bastola
yaliwaweka chini ya
ulinzi walinzi wa benki
hiyo .
Wakati hayo yakitokea
mmoja wa majambazi
hao aliamuru
wafanyakazi wa benki
hiyo kuendelea
kuwakaribisha wateja
wao na kila aliyekuwa
akiingia aliwekwa chini
ya ulinzi.
Mtuhumiwa mwingine
wa ujambazi akiwa na
bastola, alimfuata
mtunza funguo wa
chumba maalum cha
kuhifadhia fedha na
chumba cha Mashine za
Kutolea Fedha (ATM) na
kumwambia, atoe
funguo.
“Tena jambazi huyo
alimtaja kwa jina
mtunza funguo huku
akisema naomba
funguo za strong room
tumekuja kuchukua
fedha zetu,” alisema
mmoja wa mashuhuda
akimkariri jambazi huyo
na kusema alipewa
funguo bila kizuizi.
Baadaye majambazi hao
walifanikiwa kufungua
kwenye vyumba hivyo
na kuchukua fedha zote
na, kuzihifadhi kwenye
magunia manne.
Wakati shughuli hiyo
ikiendelea majambazi
wengine waliharibu
mitambo ya kamera
zinazoonyesha watu
wanaoingia na kutoka
kwenye benki hiyo.
“Tunajua mnaturekodi
kwenye kamera zenu na
sisi tunaifahamu vizuri
teknolojia hii, ndiyo
maana tunalazimika
kuharibu mtandao
mzima,” mmoja wa
jambazi alikaririwa
akisema huku akifungua
mtambo wa kamera.
Baada ya kumaliza
kuharibu mitambo ya
kamera, waliondoka na
maguni ya fedha na
kwenda walikoegesha
magari yao ya kifahari
na kupakia.
Walioshuhudia
walisema, majambazi
hao walikuwa
wakitumia magari
matatu ya aina ya
Toyota Land Cruiser,
Nissan Patrol na Toyota
Noah na kwamba,
wakati wakitekeleza
ujambazi huo madereva
wote walikuwa
wamebaki kwenye
magari hayo yaliyokuwa
yameegeshwa karibu na
benki hiyo.
Baada ya magari hayo
kupakia magunia hayo,
madereva hao
waliyaondoa magari
hayo kwa kasi kuelekea
eneo la katikati ya jiji.
Wameendelea kusema
kwamba wakati
majambazi hayo
yanaondoka katika
eneo hilo mnamo saa
2.45 asubuhi, hakukuwa
na msongamano wa
magari katika barabara
ya Nyerere kama
kawaida.
“Unafahamu muda huu
eneo hili huwa na
msongamano wa magari
lakini, tunashangaa
wakati tukio hili
linatokea hakukuwa na
magari hadi tukadhani
labda kuna msafara wa
viongozi,” alisema
mmoja wa mashuhuda.
Baada ya tukio hilo
kumalizika maofisa wa
Jeshi la Polisi walifika
katika benki hiyo
iliyopo kwenye jengo la
Jamana wakiongozwa
na Kamanda wa Kanda
Maalum ya Mkoa wa
Dar es Salaam,
Suleiman Kova.
 
Aiseee babaangu jeshi la policcm wanajisahau sana ndio maana majambazi wana wana2mia mwanya huo kufanya uwalifu,,

ngoja nikapate mbege
 
Kuhusu camera za security, majambazi hao hawaelewi vizuri jinsi zinavyofanya kazi.

Camera zinatuma picha zake moja kwa moja kwenye server na hata kama ukiharibu camera, bado wanaweza kupata picha zilizorekodiwa kabla ya kuharibu mitambo. Picha zote zinakuwa uploaded kwenye DriveHQ FTP server palepale zinapochukuliwa na zinabaki.

"Even if an intruder destroys a security camera, he cannot destroy the recorded data, which can be immensely helpful for tracking down the intruder."
 
Hii lazima itainvolve mlolongo wa watu..kuanzia bank mpaka polisi.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Hawa polisi wetu wangeambiwa ni CDM wameingia hapo mbona wangefika haraka sana!!!!!!!
 
Kuhusu camera za security, majambazi hao hawaelewi vizuri jinsi zinavyofanya kazi.

Camera zinatuma picha zake moja kwa moja kwenye server na hata kama ukiharibu camera, bado wanaweza kupata picha zilizorekodiwa kabla ya kuharibu mitambo. Picha zote zinakuwa uploaded kwenye DriveHQ FTP server palepale zinapochukuliwa na zinabaki.

"Even if an intruder destroys a security camera, he cannot destroy the recorded data, which can be immensely helpful for tracking down the intruder."

Gud Shule. Thanks mkuu
 
kama hawakuvaa ski mask kwa kujidanganya kuharibu camera basi imekula kwao...naipenda set it off starring jada,latipha na vivica fox i suppose
 
Trafiki watakuwa walisafisha njia (barabara) ili jamaa wapite, inawezekana vipi Nyerere ikawa empty saa 2:45 asubuhi halafu wanaelekea mjini!
 
polis wako mapumzikoni wanasubiri kikwete awape amri ya kuua kwenye mikutano ya chadema.wanakula bata.
 
Nchi inayoendelea hupiga hatua za maendeleo kwenye nyanja zote.
 
ingekua ni chadema issue polisi. wote wangehamia cba hadi baba yao mkuu

priorities differ
 
nadhani hata Traffic aliyekuwa pale kwenye Taa (Banda la ngozi) anaweza kuwa alihusika kuyaryhusu magari ili njia iwe nyeupe kwa wazee wa kazi wapite
 
Hii lazima itainvolve mlolongo wa watu..kuanzia bank mpaka polisi.

Polisi wamefacilitate zoezi la kuzuia magari ili watu wao wapite kirahisi hivyo polisi waliokuwa eneo hilo ni sharti wachunguzwa
 
sasa kazi ya ile chopa ya polisi ni nini au ni kwa ajili ya mafuriko tu .kweli tuna safari ndefu kufika hakuna hata kituo kimoja cha televition chenye chopa .mambo kama haya tungekuwa tunayaona live .
 
Kuhusu camera za security, majambazi hao hawaelewi vizuri jinsi zinavyofanya kazi.

Camera zinatuma picha zake moja kwa moja kwenye server na hata kama ukiharibu camera, bado wanaweza kupata picha zilizorekodiwa kabla ya kuharibu mitambo. Picha zote zinakuwa uploaded kwenye DriveHQ FTP server palepale zinapochukuliwa na zinabaki.

"Even if an intruder destroys a security camera, he cannot destroy the recorded data, which can be immensely helpful for tracking down the intruder."

Sio camera zote ndugu yangu! Camera nyingi huwa wanakusanya tapes na kuzipeleka kwenye back up houses. Ninachoshangaa ni kwamba hizo strong room imefunguliwa na mlango mmoja na haikuwa na combinations!
What a weak security!
 
Back
Top Bottom