BIG X
JF-Expert Member
- Nov 4, 2011
- 777
- 212
Kama kawaida yao, wameshirikiana na askari wetu wanaokula kodi zetu. Na muda si mrefu watakamata watu wa uongo waje kutudanganya watanzania kama siku zote wanavyofanyaga. Mambo kama hayo huwa yanasukwa muda mrefu sana, usikute hata wenye bank wanahusika. Kifupi yani ungebahatika kujua mchezo unavyochezwa na waliohusika, ungecheka mpaka mbavu ziume, maana inakuwaga ni michezo ya kuigiza kwa ajili ya lengo fulani. Mengine yote yatakayofuata ni taratibu za kawaida kama vile wanafanya kazi kufuatilia.