Uislam na Makanisa

Status
Not open for further replies.
Ukimya wa Serikali, hasa Kiongozi mkuu wa nchi ni jambo la hatari, inaonekana waliokuwa wakisema yu nyuma ya udini inadhihirika sasa. Kwa hakika amani ndio njia, iwe iwavyo kwa hatua hizi itafika wakati ambapo hata hao waonekanao kuwa sababu ya amani kwa kutokuwa wepesi wa hasira watachoka na hapo amani itakuwa historia iliyopita. Tuwe makini, tuchukue hatua maana hakuna kupona kwa kizazi hiki ikiwa ujinga huu wa kizandiki utaachwa uendelee.
 
Sasa hapa ndipo nisipokubaliana nanyi kabisa. Kama kweli serikali ilishindwa kwa nini leo wanajenga Hospital na Mashule?..Shule za kata za nini kujenga na serikali ikiwa serikali ilishashindwa toka zamani. Kwa nini kushindwa kwa serikali ktk sektra hizo leo hii mnailaumu serikali na sio kanisa ama viongozi waliopewa jukumu hilo?. Majuzi tu wamefukuzwa naibu waziri wa Afya ili hali kuna ufisadi mkubwa sana kwa waliopewa mamalka na bohari ya madawa na vyombo vinavyochukua jukumu la quote n qoute - Kuendeleza ELIMU na AFYA nchini badala yake leo tunazalisha makabuntas kuliko wakati wowote wa utawala wa Nyerere. Hii ilipangwa na ndio maana swala la kuondoa muafaka huu lisiwe sababu ya kwanza badala ya kuwafukuza mawaziri ambao hawana mamlaka zaidi ya yale waliokabidhiwa.

Kwani nini msijenge mashule yenu na hospitali zenu muishie kuweka roho za korosho kwa wenzenu wakristo ambao pia wanawahifadhi?.

Kama jibu ni kuwa hamuwezi kwa sbb hakuna misaada, basi hao ndugu zenu waislamu wa huko arabuni wana roho mbaya na muwalaumu hao hao maana ndio adui wenu! Me mpaka najiuliza hv labda uislamu ni Uchoyo na kujilimbikizia mali??. Qatar, UAE etc etc ni matajiri wa kutupwa lakini huwezi kuwasikia wametoa sadaka au basi tuseme msaada kwenye budget za nchi masikini kama Znzbar etc.,potelea mbali kujenga hospitali au shule. Zaidi zaidi misikiti.. Na hata Znzbar kwa uchoyo wao baada ya kuona kuna dalili ya mafuta..wameongeza chokochoko ya kujitoa ili wafaidi wenyewe.

Kimsingi,hao mnaowachomea makanisa ndio wanaowa-fund katika bajeti zenu na ndio wanaoingiza kipato kikubwa kwa kuja kutalii huko na nyie kupata ajira na maisha kuendelea..!

Hamumjui ADUI yenu..kalaghabao na ubwezi wenu, you are just masikini wa akili na utu wakubwa!
 
Mleta mada anasema Vurugu za waislam zinaashiria upungufu katika mafundisho ya dini yao!! kama tabia za waumin huashiria udhaifu kwenye mafundisho, atusaidie tusiojuwa kutafsiri wale mapadri waloshiriki kuwakusanya na kisha kuwachinja Watutsi kule Rwanda inaashiria nini kwenye mafundisho ya Dini yao?, Yule muasi Joseph Konny anaeuawa watoto na kina mama Uganda ili asimamishe Amri Kumi kwenye Dola la Uganda ina ishara gani kwenye mafundisho ya Dini?, Slobadan Milosovick alokuwa akipitisha katapira kwenye Miili ya kina mama wa Kiislam ilimaanisha nini kwenye Imani yake!! Mleta mada aende akajifunze Historia Adolf Hitler alipokuwa akinyonga wayahudi alipata back up ya Dini gani? then ndo afanye majumuisho ya mada aloileta ili apate muktadha kwa alichokileta ili aonekane ametazama beyond his Horizon!
 
Mkandara,Saint Ivuga,FJM,Pharaoh,

..ELIMU na AFYA ni masuala ya muungano.

..MOU inafanya kazi huku Tanganyika tu, Zanzibar wana wizara zao wenyewe za elimu na afya.

..ingekuwa suala hili linahusiana na Waislamu wa Tanganyika basi kungekuwa na mantiki kuibua suala la MOU, tatizo ni kwamba mtafaruku huu umetokea Zanzibar[ambako hakuna mou] ingawa wananchi wa huko asilimia 99% ni Waislamu.

..kwa kweli kama mmekuwa mkisiliza mihadhara ya UAMSHO na zaidi kufuatilia kinachoandikwa ktk mtandao wa www.mzalendo.net, basi hamtashangazwa kabisa na kutokea kwa vurugu hizi, na zaidi kuchomwa moto kwa makanisa.

..kuna watu wamekuwa wakilalamika waziwazi na kwa muda mrefu kwamba muungano umesababisha MAKANISA kuwa mengi mno Zanzibar. Kuna watu wanaona makanisa ni kero huko Zanzibar. Wengine wanalalamika kwamba muungano ni agenda ya ku-CHRISTIANIZE Zanzibar, au ni CRUSADE dhidi ya UISLAMU.

..Sasa kama kauli hizo zimekuwa zikitolewa kwa muda mrefu, nini kinachowashangaza kwamba ktk maandamano ya kupinga muungano makanisa yamekuwa ni target??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom