SEHEMU YA PILI
******************
Kabila langu ni Taturu, baba yangu alibahatika kufanya kazi na Padri fulani mkoa wa Singida, hivyo masikio yangu yalinusurika kutobolewa, mimi pamoja na mdogo wangu niliyemuachia ziwa.
Miezi kadhaa nikiwa nimerudi nchini kutoka masomoni Ulaya, nikiwa mwajiriwa wa RTC maarufu kama UGAWAJI enzi hizo (siyo TRC), nilimtafuta Rose (wa Lindi; stori yake ipo kwenye uzi wa kula tunda kimasihara), Rozi hakujibu barua zangu tangia nilipo kuwa Ulaya. Miaka mitano ilikuwa imeshapita sasa.
=
Rose nilimuacha Lindi na kurudi Dar es Salaam baada ya kuwa naye Lindi kwa uhusiano wa mapenzi motomoto ya miezi miwili. Nikiwa Dar tulikuwa tunawasiliana kama kawaida lakini sikupata bahati ya kuonana naye ana kwa ana hadi leo hii ninapoandika haya.
=
Nilikata tamaa ya kuendelea kumtafuta, kazi yangu nayo ilichangia kwa kuwa nilikuwa bize mno hususani baada ya kurudi masomoni na kupandishwa cheo...
Labda mchumba wake aliendeleza uhusiano wao na kumuoa, hivyo aliamua kukata mawasiliano, hii ndiyo dhana kuu niliyobaki nayo, nahisi mtoto wake wa kwanza ni damu yangu.
************************
James mimi nilikuwa "kiwembe" sana kabla ya kukutana na Rose, umri wa kuoa ulikuwa umeshafika hivyo nilidhani kwake Rose ningehitimisha useja.
Baada ya kukata tamaa niliamua kuendeleza wimbi la 'ubazazi', kutembea na kila binti mrembo niliyemtaka...
Uingereza 'sikutembea' hovyo, nilikuwa na girl friend mmoja tu mwanchuo mwenzangu aliyetokea Hispania, Sue Parterson. Miss Sue ndiye aliyenipatia kitabu "Frech Sex Art Manners" kilichoandikwa na G. Valensin, nilijifunza mengi lakini uhusiano wangu na binti Paterson haukuwa wa malengo ya mbali, hivyo niliachana naye miaka miwili kabla ya kurudi nchini (nilidumu yaye kwa miaka miwili na miezi tisa hivi) ambapo nilienda Kaskazini zaidi kuchukuwa post graduate diploma fulani.
Enzi hizo kabla ya kwenda Ulaya hususani Uingereza, kulikuwa na utaratibu wa kupata semina fupi pale British Council, kwa ajili ya kuwaweka sawa kukabiliana na mazingira ya huko. Nakumbuka pamoja na mambo mengine tulifundishwa kufunga tai [emoji1787] (japo nilikuwa najuwa kabla)
Nilivyorudi Tanzania, nikapewa nafasi nzuri katika RTC (Regional Trading Company), nikatumia kufahamika kwangu na umuhimu wangu kujipatia mabinti warembo kila uchao hadi siku hiyo moyo uliponilipuka kwa kumuona Hamida.
*************************************
Makatibu Kata walitusaidia sana katika kazi zetu, nikazoeana na Katibu kata mmoja ambaye alikuwa Kata ya Magomeni.
Kulikuwa na mkutano uliandaliwa kati ya Uongozi wa Kata na wajumbe wa nyumba kumi kumi kuhusiana na hali ya upatikanaji wa bidhaa katika mkoa.
Nchi ilikuwa imetoka vitani, (Tanzania vs Uganda), hali ya uchumi ilikuwa imeyumba hivyo wajumbe walitakiwa kuwaandaa waananchi katika mashina yao kukabiliana na hali inayoanza kujitokeza.
Mzee Katibu Kata rafiki yangu nilipomtembelea afisini kwake, (nyuma ya Hotel Travertine hivi sasa) ndipo akaniomba nimsambazie barua kwa baadhi ya wajumbe Magomeni Mapipa; alikuwa hajisikii vizuri (alikuwa ana homa)
Magomeni Mapipa enzi hizo palikuwa maarufu sana, hapo ndipo kulikuwa na U-turn kubwa kwa ajili ya magari aina ya 'Ikarus' kugeuzia.
Mabasi haya pamoja na mabasi mengine yalikuwa yanamilikiwa na Shirika la UDA (Usafiri Dar es Salaam) ambapo walikuwa na mabasi yaliyotengenezwa na kampuni mbalimbali ikiwemo Mercides Benz (German), Isuzu (Japan), Ikarus (Hungary) nk.
Wanafunzi walikuwa wanapenda sana kupanda Ikarus, na waliyaita "ikarus kumbakumba" maana likija moja lilikuwa linapakia abiria wengi kwa mara moja. Mfano wake ni kama haya mabasi ya Kichina ya BRT yale marefu.
*****************************
Wakati nimechuchumaa nafunga viatu kamba huku nikimuangalia Hamida akiwa ameinama kuokota mtandio wake pamoja na bilauli zile, yule mama mwenye sauti nyororo nikimsikia akisema " Kwema huko?, taratibu mnatushtua na presha hizi..."
"Ziliniponyoka, ngoja nikazisuuze tena nizilete"
Hamida alijibu, nikaisikia sauti yake nyororo akiongea sentesi nzima.
Maa shaa Allah kumbe naye ana sauti kama ya yule mama Mwarabu.
"Kwaheri Hamida"
Nilijikuta nimeropoka huku nikirudi kinyumenyume kuelekea mlango wa kutokea nje. Hamida hakujibu kitu, aliinama na kugeuka akaelekea uani (siyo maliwatoni), mtandio alijifunika kichwani lakini kwa kuutupia tu.
Niligeuka na kuvuta mlango kwa ndani na kutoka nje.
***********
Mzee Burhani ni mjumbe wa nyumba kumi katika mtaa huo nilipotoka, ni mzee kwenye hekima na mcheshi sana, muislamu safi na mwenye kuipenda familia yake na jamii aiongozayo kwa ujumla.
"Salama leko"
Nilisalimia kama waislamu wanavyosalimia, waliitikia lakini mzee mmoja wa makamo akaniambia, wewe James inabidi ujifunze kusalimia vizuri...
Hatusemi salama leko bali tunasema Assalaam aleikum. Pale pale nikarudia
"Assalaam aleikum"
Wakaitikia tena kwa wingi.
"Inabidi usilimu kijana."
Mzee Burhani alidakia.
"Hahhaha" nilicheka, kisha nikamwambia kuwa ule ulikuwa ni 'mguu wake'
Kwakuwa haikuwa siri nilimueleza kuwa nilipitia nyumbani kwake na kuacha barua na kumpa yaliyo ndani kwa ufupi, kisha nami nikajisogeza kwenye benchi nikaketi huku nikiangalia wanavyocheza keram.
_____
Itaendelea...
James Jason