JBourne59
JF-Expert Member
- Jan 17, 2020
- 941
- 8,547
UHUSIANO WANGU KIMAPENZI NA HAMIDA
Utangulizi.
'Mama watoto' aliridhia mimi kuandika simulizi hii kwa masharti.
Moja ya masharti nijitahidi kutoacha mlango / milango wazi itakayoruhusu watu kuunganisha dots...
Masharti mengine kwa kuwa ni sehemu ya codes, sintoyaeleza.
Hivyo katika simulizi hii nitaongeza 'chumvi' ama 'kuongeza maji' ili kuleta ladha kusudiwa.
Hamida ni mke wangu ambaye "hajaniacha"
=
=
=
Angalizo:
Picha ni kwa hisani ya "google"
Hazina uhusiano na simulizi hii.
Pia kuna sehemu inaweza kuamsha hisia za mapenzi,
Simulizi hii haina uhusiano na Hamida aliye-trend kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni.
Majina yote ya watu katika simulizi hii hayatokuwa halisi isipokuwa machache sana kwa sababu maalum.
SEHEMU YA KWANZA
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
"Hodiii!, hodi hodi humu ndani"
Nilibisha hodi huku nikigonga mlango kwa kutumia kipande cha chuma kilichoning'izwa maalum kwa ajili hiyo.
"Karibu, fungua mlango umeshindikwa tu"
Sauti nyororo ilisikika kutoka ndani.
"Starehe"
Nilijibu huku nikisukuma mlango mzito wa mbao ulionakshiwa kwa ustadi mkubwa. (Neno 'starehe' enzi hizo ndio lilitumika kujibu pindi ubishapo hodi na kukaribishwa)
Nilipofungua mlango nikakutana na korido ndefu nyembamba (wakati huo iliitwa 'ukumbi' japo siyo kama kumbi tuzijuazo leo), pembeni kulia na kushoto kulikuwa milango, wa kushoto ulikuwa mpana ambapo ulikuwa wazi ukiwa umesitiriwa na pazia zuri jepesi lenye 'kuangaza' (transparent) la rangi nyeupe, upande wa kulia mlango ulikuwa umefungwa, na milango mingine mitatu pia ilikuwa imefungwa.
Mbele mwisho wa korido kulikuwa na mlango ambao ulikuwa wazi kiasi cha kuweza kuona nafasi kubwa iliyokuwepo na sehemu ya uzio wenyeji waliita uani (sikuhizi ukisema uani watu watajuwa ni maliwatoni)
************
"Karibu tupo huku varandani"
Ile sauti nyororo iliendelea kunikaribisha na sauti hiyo ilitokea upande ule wa pazia jepesi angavu ambapo nilivyoingia nikatambua kuwa pale palikuwa ndiyo sebuleni.
Kabla ya kuingia nilivua viatu vyangu (raba - Morogoro shoes), havikutoa harufu mbaya kwa kuwa ndiyo nimevivaa kwa mara ya kwanza baada ya kuvinunua, vilikuwa vya rangi ya bluu na soksi zangu nyeupe. Hapo mlangoni kulikuwa na viatu vya sandarusi vyenye ukubwa tofauti pea tatu... nikajuwa utaratibu wa kuingia humo ni pamoja na kuvua viatu.
Nilipekenyua pazia kulia na kushoto na kupiga hatua kuvuka kivingiti cha mlango na kukanyaga zulia zuri la manyoya manyoya.
Ndani niliwakuta wanawake wawili na mtoto mmoja mdogo wa chini ya miaka mitano. Wale wanawake mmoja alikuwa mwafrika, amejitanda vizuri ushungi huku akiwa ameshika ukili (alikuwa anasuka mkeka).
Wote walikuwa wamekaa chini na kuegemea mito midogo, hapakuwa na viti bali meza ndogo iliyo chinichini sana jirani na zulia.
Yule mwanamke wa pili alikuwa mweupe, asili ya Asia, na sikuweza kufahamu maramoja kama alikuwa Mwarabu ama Mhindi. Alikuwa anakoroga maji ya rangirangi akichanganya sukari na yale maji, bila shaka alikuwa anaandaa "ashkrim", watoto walikuwa wanaita hivyo. Zilikuwa zile "ice-cream" (malai) ambaozo maji huwekwa kwenye "kijikopo" kidogo kisha kuchomekwa kijiti cha chelewa ambapo maji yakiganda kile kijiti huwa ni sehemu ya kushika ashkrim hiyo.
"Karibu uketi"
Alisema yule mwanamke 'mwarabu' huku akiendelea na kazi yake.
Ndipo nikajuwa kuwa ile sauti nyororo ni ya huyo mama.
"HAMIDAAAA"
Aliita yule mama wa kiarabu.
Mara nikasikia sauti mlango fulani ukifunguliwa na kisha hatua za kivivu zikija upande wetu kutokea koridoni.
Pazia lilisogezwa pembeni akachungulia msichana aliye jitanda ushungi.
"Abee"
Yule binti aliitikia huku akimuangalia yule mama mkoroga malai.
"Hebu kamletee mgeni kinywaji"
Yule binti aliondoka bila kusema neno.
"Mzee Mjumbe nimemkuta?"
Niliuliza hivyo baada ya kuwasalimia kama ilivyo desturi na kujitambulisha.
"Tangia alivyoenda msikitini bado hajarudi, bila shaka atakuwa pale Shibam wanapocheza keram na zuna"
Alijibu yule mama huku ameinama akiendelea na kazi yake.
*************************
Michezo ya Keram, Zuna, Karata, Bao ilikuwa maarufu sana kwenye 'kijiwe' cha kahawa na tangawizi pale Shibam na sehemu nyingine jijini Dar es Salaam. Mambo na mipango mbalimbali ilijadiliwa hapo ikiwemo siasa, michezo nk.
Mara yule binti alirudi huku ameshika magi iliyojaa sharubati na mkono wa kushoto ameshika bilauli ya bati.
Alimimina ile togwa kwenye ile bilauli mbele yangu kisha akanipatia. Ilikuwa togwa ya mtama uliokobolewa na kutengenezwa kwa ustadi mkubwa.
Maeneo ya FAYA (fire brigade) hivi sasa, zamani palikuwa na mti wa muembe mkubwa ambapo palikuwa maarufu sana kwa biashara ya togwa hadi eneo hilo likapewa jina la "mwembe togwa"
Pia haikuwa ajabu kukuta sinia yenye maji iliyowekwa chupa za 'fanta' ndani mkiwa na togwa, imezibwa na kipande cha gazeti iliyokunjwa vema kwenye kila chupa, wengine waliweka chupa moja tu ama stuli iliyofunikwa kawa bila kitu ndani, wateja hutambua moja kwa moja kwamba hapo kuna biashara fulani.
**********************
Niliipokea ile bilauli na kuigigida (kuinywa kwa haraka) kwani nilikuwa nataka niondoke niwahi kupeleka ujumbe sehemu nyingine kwa kuwa hapo tayari niliwaachia moja ya barua nilizokuwa nazo.
Nilikuwa nina karatasi kadhaa (barua) za kuwasambazia wajumbe wa nyumba 'kumi kumi' (waliitwa hivyo) kutoka kwa Katibu Kata, Kata ya Magomeni...
Niliwaaga wale wenyeji mle sebuleni na kuanza kuondoka. Yule binti naye akachukuwa ile bilauli pekee na kuacha magi yenye togwa iliyobakia pale sebuleni...
***********
Wakati navaa viatu pale koridoni, Hamida (siyo jina lake halisi) naye akawa anakuja kutoka uani (siyo maliwatoni) huku ameshika bilauli nne mkononi...
Nikawa namuangalia huku nikiwa nafunga kamba za viatu. Mara ghafla mtandio ukateleza akabaki kichwa wazi...
Moyo ulinilipuka paa! Kwa kumuona Hamida vizuri waziwazi...
Aliinama haraka haraka na kuchukuwa mtandio wake lakini kwa bahati mbaya tena zile bilauli zikamponyoka na kuanguka sakafuni...
=
=
=
****
Hivi ndivyo nilivyokutana na Hamida wangu...
***********
Inaendelea post #5
Utangulizi.
'Mama watoto' aliridhia mimi kuandika simulizi hii kwa masharti.
Moja ya masharti nijitahidi kutoacha mlango / milango wazi itakayoruhusu watu kuunganisha dots...
Masharti mengine kwa kuwa ni sehemu ya codes, sintoyaeleza.
Hivyo katika simulizi hii nitaongeza 'chumvi' ama 'kuongeza maji' ili kuleta ladha kusudiwa.
Hamida ni mke wangu ambaye "hajaniacha"
=
=
=
Angalizo:
Picha ni kwa hisani ya "google"
Hazina uhusiano na simulizi hii.
Pia kuna sehemu inaweza kuamsha hisia za mapenzi,
Simulizi hii haina uhusiano na Hamida aliye-trend kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni.
Majina yote ya watu katika simulizi hii hayatokuwa halisi isipokuwa machache sana kwa sababu maalum.
SEHEMU YA KWANZA
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
"Hodiii!, hodi hodi humu ndani"
Nilibisha hodi huku nikigonga mlango kwa kutumia kipande cha chuma kilichoning'izwa maalum kwa ajili hiyo.
"Karibu, fungua mlango umeshindikwa tu"
Sauti nyororo ilisikika kutoka ndani.
"Starehe"
Nilijibu huku nikisukuma mlango mzito wa mbao ulionakshiwa kwa ustadi mkubwa. (Neno 'starehe' enzi hizo ndio lilitumika kujibu pindi ubishapo hodi na kukaribishwa)
Nilipofungua mlango nikakutana na korido ndefu nyembamba (wakati huo iliitwa 'ukumbi' japo siyo kama kumbi tuzijuazo leo), pembeni kulia na kushoto kulikuwa milango, wa kushoto ulikuwa mpana ambapo ulikuwa wazi ukiwa umesitiriwa na pazia zuri jepesi lenye 'kuangaza' (transparent) la rangi nyeupe, upande wa kulia mlango ulikuwa umefungwa, na milango mingine mitatu pia ilikuwa imefungwa.
Mbele mwisho wa korido kulikuwa na mlango ambao ulikuwa wazi kiasi cha kuweza kuona nafasi kubwa iliyokuwepo na sehemu ya uzio wenyeji waliita uani (sikuhizi ukisema uani watu watajuwa ni maliwatoni)
************
"Karibu tupo huku varandani"
Ile sauti nyororo iliendelea kunikaribisha na sauti hiyo ilitokea upande ule wa pazia jepesi angavu ambapo nilivyoingia nikatambua kuwa pale palikuwa ndiyo sebuleni.
Kabla ya kuingia nilivua viatu vyangu (raba - Morogoro shoes), havikutoa harufu mbaya kwa kuwa ndiyo nimevivaa kwa mara ya kwanza baada ya kuvinunua, vilikuwa vya rangi ya bluu na soksi zangu nyeupe. Hapo mlangoni kulikuwa na viatu vya sandarusi vyenye ukubwa tofauti pea tatu... nikajuwa utaratibu wa kuingia humo ni pamoja na kuvua viatu.
Nilipekenyua pazia kulia na kushoto na kupiga hatua kuvuka kivingiti cha mlango na kukanyaga zulia zuri la manyoya manyoya.
Ndani niliwakuta wanawake wawili na mtoto mmoja mdogo wa chini ya miaka mitano. Wale wanawake mmoja alikuwa mwafrika, amejitanda vizuri ushungi huku akiwa ameshika ukili (alikuwa anasuka mkeka).
Wote walikuwa wamekaa chini na kuegemea mito midogo, hapakuwa na viti bali meza ndogo iliyo chinichini sana jirani na zulia.
Yule mwanamke wa pili alikuwa mweupe, asili ya Asia, na sikuweza kufahamu maramoja kama alikuwa Mwarabu ama Mhindi. Alikuwa anakoroga maji ya rangirangi akichanganya sukari na yale maji, bila shaka alikuwa anaandaa "ashkrim", watoto walikuwa wanaita hivyo. Zilikuwa zile "ice-cream" (malai) ambaozo maji huwekwa kwenye "kijikopo" kidogo kisha kuchomekwa kijiti cha chelewa ambapo maji yakiganda kile kijiti huwa ni sehemu ya kushika ashkrim hiyo.
"Karibu uketi"
Alisema yule mwanamke 'mwarabu' huku akiendelea na kazi yake.
Ndipo nikajuwa kuwa ile sauti nyororo ni ya huyo mama.
"HAMIDAAAA"
Aliita yule mama wa kiarabu.
Mara nikasikia sauti mlango fulani ukifunguliwa na kisha hatua za kivivu zikija upande wetu kutokea koridoni.
Pazia lilisogezwa pembeni akachungulia msichana aliye jitanda ushungi.
"Abee"
Yule binti aliitikia huku akimuangalia yule mama mkoroga malai.
"Hebu kamletee mgeni kinywaji"
Yule binti aliondoka bila kusema neno.
"Mzee Mjumbe nimemkuta?"
Niliuliza hivyo baada ya kuwasalimia kama ilivyo desturi na kujitambulisha.
"Tangia alivyoenda msikitini bado hajarudi, bila shaka atakuwa pale Shibam wanapocheza keram na zuna"
Alijibu yule mama huku ameinama akiendelea na kazi yake.
*************************
Michezo ya Keram, Zuna, Karata, Bao ilikuwa maarufu sana kwenye 'kijiwe' cha kahawa na tangawizi pale Shibam na sehemu nyingine jijini Dar es Salaam. Mambo na mipango mbalimbali ilijadiliwa hapo ikiwemo siasa, michezo nk.
Mara yule binti alirudi huku ameshika magi iliyojaa sharubati na mkono wa kushoto ameshika bilauli ya bati.
Alimimina ile togwa kwenye ile bilauli mbele yangu kisha akanipatia. Ilikuwa togwa ya mtama uliokobolewa na kutengenezwa kwa ustadi mkubwa.
Maeneo ya FAYA (fire brigade) hivi sasa, zamani palikuwa na mti wa muembe mkubwa ambapo palikuwa maarufu sana kwa biashara ya togwa hadi eneo hilo likapewa jina la "mwembe togwa"
Pia haikuwa ajabu kukuta sinia yenye maji iliyowekwa chupa za 'fanta' ndani mkiwa na togwa, imezibwa na kipande cha gazeti iliyokunjwa vema kwenye kila chupa, wengine waliweka chupa moja tu ama stuli iliyofunikwa kawa bila kitu ndani, wateja hutambua moja kwa moja kwamba hapo kuna biashara fulani.
**********************
Niliipokea ile bilauli na kuigigida (kuinywa kwa haraka) kwani nilikuwa nataka niondoke niwahi kupeleka ujumbe sehemu nyingine kwa kuwa hapo tayari niliwaachia moja ya barua nilizokuwa nazo.
Nilikuwa nina karatasi kadhaa (barua) za kuwasambazia wajumbe wa nyumba 'kumi kumi' (waliitwa hivyo) kutoka kwa Katibu Kata, Kata ya Magomeni...
Niliwaaga wale wenyeji mle sebuleni na kuanza kuondoka. Yule binti naye akachukuwa ile bilauli pekee na kuacha magi yenye togwa iliyobakia pale sebuleni...
***********
Wakati navaa viatu pale koridoni, Hamida (siyo jina lake halisi) naye akawa anakuja kutoka uani (siyo maliwatoni) huku ameshika bilauli nne mkononi...
Nikawa namuangalia huku nikiwa nafunga kamba za viatu. Mara ghafla mtandio ukateleza akabaki kichwa wazi...
Moyo ulinilipuka paa! Kwa kumuona Hamida vizuri waziwazi...
Aliinama haraka haraka na kuchukuwa mtandio wake lakini kwa bahati mbaya tena zile bilauli zikamponyoka na kuanguka sakafuni...
=
=
=
****
Hivi ndivyo nilivyokutana na Hamida wangu...
***********
Inaendelea post #5