Uhusiano wangu kimapenzi na "Hamida"

JBourne59

JF-Expert Member
Jan 17, 2020
941
8,547
UHUSIANO WANGU KIMAPENZI NA HAMIDA

Utangulizi.

'Mama watoto' aliridhia mimi kuandika simulizi hii kwa masharti.

Moja ya masharti nijitahidi kutoacha mlango / milango wazi itakayoruhusu watu kuunganisha dots...

Masharti mengine kwa kuwa ni sehemu ya codes, sintoyaeleza.

Hivyo katika simulizi hii nitaongeza 'chumvi' ama 'kuongeza maji' ili kuleta ladha kusudiwa.

Hamida ni mke wangu ambaye "hajaniacha"
=
=
=

Angalizo:
Picha ni kwa hisani ya "google"
Hazina uhusiano na simulizi hii.

Pia kuna sehemu inaweza kuamsha hisia za mapenzi,

Simulizi hii haina uhusiano na Hamida aliye-trend kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni.

Majina yote ya watu katika simulizi hii hayatokuwa halisi isipokuwa machache sana kwa sababu maalum.





SEHEMU YA KWANZA
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

"Hodiii!, hodi hodi humu ndani"

Nilibisha hodi huku nikigonga mlango kwa kutumia kipande cha chuma kilichoning'izwa maalum kwa ajili hiyo.

"Karibu, fungua mlango umeshindikwa tu"

Sauti nyororo ilisikika kutoka ndani.

"Starehe"

Nilijibu huku nikisukuma mlango mzito wa mbao ulionakshiwa kwa ustadi mkubwa. (Neno 'starehe' enzi hizo ndio lilitumika kujibu pindi ubishapo hodi na kukaribishwa)

Nilipofungua mlango nikakutana na korido ndefu nyembamba (wakati huo iliitwa 'ukumbi' japo siyo kama kumbi tuzijuazo leo), pembeni kulia na kushoto kulikuwa milango, wa kushoto ulikuwa mpana ambapo ulikuwa wazi ukiwa umesitiriwa na pazia zuri jepesi lenye 'kuangaza' (transparent) la rangi nyeupe, upande wa kulia mlango ulikuwa umefungwa, na milango mingine mitatu pia ilikuwa imefungwa.

Mbele mwisho wa korido kulikuwa na mlango ambao ulikuwa wazi kiasi cha kuweza kuona nafasi kubwa iliyokuwepo na sehemu ya uzio wenyeji waliita uani (sikuhizi ukisema uani watu watajuwa ni maliwatoni)
************

"Karibu tupo huku varandani"
Ile sauti nyororo iliendelea kunikaribisha na sauti hiyo ilitokea upande ule wa pazia jepesi angavu ambapo nilivyoingia nikatambua kuwa pale palikuwa ndiyo sebuleni.

Kabla ya kuingia nilivua viatu vyangu (raba - Morogoro shoes), havikutoa harufu mbaya kwa kuwa ndiyo nimevivaa kwa mara ya kwanza baada ya kuvinunua, vilikuwa vya rangi ya bluu na soksi zangu nyeupe. Hapo mlangoni kulikuwa na viatu vya sandarusi vyenye ukubwa tofauti pea tatu... nikajuwa utaratibu wa kuingia humo ni pamoja na kuvua viatu.

Nilipekenyua pazia kulia na kushoto na kupiga hatua kuvuka kivingiti cha mlango na kukanyaga zulia zuri la manyoya manyoya.

Ndani niliwakuta wanawake wawili na mtoto mmoja mdogo wa chini ya miaka mitano. Wale wanawake mmoja alikuwa mwafrika, amejitanda vizuri ushungi huku akiwa ameshika ukili (alikuwa anasuka mkeka).

Wote walikuwa wamekaa chini na kuegemea mito midogo, hapakuwa na viti bali meza ndogo iliyo chinichini sana jirani na zulia.

Yule mwanamke wa pili alikuwa mweupe, asili ya Asia, na sikuweza kufahamu maramoja kama alikuwa Mwarabu ama Mhindi. Alikuwa anakoroga maji ya rangirangi akichanganya sukari na yale maji, bila shaka alikuwa anaandaa "ashkrim", watoto walikuwa wanaita hivyo. Zilikuwa zile "ice-cream" (malai) ambaozo maji huwekwa kwenye "kijikopo" kidogo kisha kuchomekwa kijiti cha chelewa ambapo maji yakiganda kile kijiti huwa ni sehemu ya kushika ashkrim hiyo.

"Karibu uketi"

Alisema yule mwanamke 'mwarabu' huku akiendelea na kazi yake.

Ndipo nikajuwa kuwa ile sauti nyororo ni ya huyo mama.

"HAMIDAAAA"

Aliita yule mama wa kiarabu.

Mara nikasikia sauti mlango fulani ukifunguliwa na kisha hatua za kivivu zikija upande wetu kutokea koridoni.

Pazia lilisogezwa pembeni akachungulia msichana aliye jitanda ushungi.

"Abee"
Yule binti aliitikia huku akimuangalia yule mama mkoroga malai.

"Hebu kamletee mgeni kinywaji"

Yule binti aliondoka bila kusema neno.

"Mzee Mjumbe nimemkuta?"

Niliuliza hivyo baada ya kuwasalimia kama ilivyo desturi na kujitambulisha.

"Tangia alivyoenda msikitini bado hajarudi, bila shaka atakuwa pale Shibam wanapocheza keram na zuna"

Alijibu yule mama huku ameinama akiendelea na kazi yake.
*************************

Michezo ya Keram, Zuna, Karata, Bao ilikuwa maarufu sana kwenye 'kijiwe' cha kahawa na tangawizi pale Shibam na sehemu nyingine jijini Dar es Salaam. Mambo na mipango mbalimbali ilijadiliwa hapo ikiwemo siasa, michezo nk.

Mara yule binti alirudi huku ameshika magi iliyojaa sharubati na mkono wa kushoto ameshika bilauli ya bati.

Alimimina ile togwa kwenye ile bilauli mbele yangu kisha akanipatia. Ilikuwa togwa ya mtama uliokobolewa na kutengenezwa kwa ustadi mkubwa.

Maeneo ya FAYA (fire brigade) hivi sasa, zamani palikuwa na mti wa muembe mkubwa ambapo palikuwa maarufu sana kwa biashara ya togwa hadi eneo hilo likapewa jina la "mwembe togwa"

Pia haikuwa ajabu kukuta sinia yenye maji iliyowekwa chupa za 'fanta' ndani mkiwa na togwa, imezibwa na kipande cha gazeti iliyokunjwa vema kwenye kila chupa, wengine waliweka chupa moja tu ama stuli iliyofunikwa kawa bila kitu ndani, wateja hutambua moja kwa moja kwamba hapo kuna biashara fulani.
**********************

Niliipokea ile bilauli na kuigigida (kuinywa kwa haraka) kwani nilikuwa nataka niondoke niwahi kupeleka ujumbe sehemu nyingine kwa kuwa hapo tayari niliwaachia moja ya barua nilizokuwa nazo.

Nilikuwa nina karatasi kadhaa (barua) za kuwasambazia wajumbe wa nyumba 'kumi kumi' (waliitwa hivyo) kutoka kwa Katibu Kata, Kata ya Magomeni...

Niliwaaga wale wenyeji mle sebuleni na kuanza kuondoka. Yule binti naye akachukuwa ile bilauli pekee na kuacha magi yenye togwa iliyobakia pale sebuleni...
***********

Wakati navaa viatu pale koridoni, Hamida (siyo jina lake halisi) naye akawa anakuja kutoka uani (siyo maliwatoni) huku ameshika bilauli nne mkononi...

Nikawa namuangalia huku nikiwa nafunga kamba za viatu. Mara ghafla mtandio ukateleza akabaki kichwa wazi...

Moyo ulinilipuka paa! Kwa kumuona Hamida vizuri waziwazi...

Aliinama haraka haraka na kuchukuwa mtandio wake lakini kwa bahati mbaya tena zile bilauli zikamponyoka na kuanguka sakafuni...

=
=
=
****
Hivi ndivyo nilivyokutana na Hamida wangu...
***********

Inaendelea post #5
 
KWA WASOMAJI WAPYA

Nitaweka simulizi ya "Rose" wa Lindi kisha nitaweka sehemu ya kwanza na ya pili ya simulizi inayoendelea ya UHUSIANO WANGU KIMAPENZI NA HAMIDA ili tuende pamoja.




James Jason
"ROSE"
****"***

Mwaka 1977, mwezi sita tarehe ishirini mwanzoni, ilikuwa majira ya alasiri nipo bandarini Dar es Salaam nasubiria turuhusiwe tuingie ndani ya meli, Ms Mtwara. Safari yangu ilikuwa inaishia Lindi, kazi fulani hivi ya muda mfupi.

Nilikuwa kijana barobaro mwenye mwili kama wanariadha, ndani ya ajira miezi sita ama saba hivi, mwenye shauku ya safari, na kwa mara ya kwanza ndio natarajia kupanda meli, kabla ya hapo sikuwahi kupanda chombo cha majini chenye kutumia injini ingawaje nilishawahi kupanda mtumbwi kuvuka mto Sibiti (Iramba / Meatu) na kuogelea nilikuwa najuwa hivyo sikuwa na hofu ya safari bali shauku ya kuona "dunia ya bahari" ilivyo.

Kusini ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, njia ya barabara ilikuwa na changamoto sana enzi hizo hivyo njia nyepesi ilikuwa ni kupanda ndege (ndege za lift twin walter ama buffalo) ama meli (Mv Lindi ama Ms Mtwara).

Baada ya muda mfupi tukaruhusiwa kuingia ndani ya meli, nikaingia kisha nikaelekezwa sehemu yangu (daraja la pili). Nikaweka sanduku langu vizuri (chapa 'swata' au 'smata', sikumbuki vizuri.

Ndani ya apartment yetu nilimkuta abiria mmoja mzee wa makamo tayari amekaa anasoma gazeti, baada ya kumsalimia nikasimama jirani na dirisha nikiangalia mandhari ya bandari. Mara akaingia abiria mwingine lakini cha ajabu alikuwa mwanadada, akapigwa na butwaa kukuta ndani tupo wanaume wawili, akatoka nje, (alimfuata mhudumu ili aoneshwe sehemu yake.)

Haikupita muda mrefu akaingia abiria mwingine, mwanaume, kwa umri alionekana mkubwa kuliko mimi lakini hakuwa mzee.

Honi kadhaa zilipigwa kuashiria meli inataka 'kung'oa nanga' na kuanza safari, nikachungulia nje dirishani nikaona kuna mzee mmoja anaogelea kwa umahiri mkubwa akielekea upande wa mbele kumalizia kutoa kamba nene iliyoishikilia meli ibanane vyema na gati.

Honi ziliendelea na meli ikaanza kuondoka taratibu. Mara yule mdada na mhudumu walikuja kwenye apartment yetu, mhudumu akamsihi akae nasi kwa kuwa meli imejaa sana na apartment zote zilizokuwa na wanawake zimejaa.

Bila shaka kulikuwa na utaratibu wa kuwaweka wanaume peke yao na wanawake peke yao, au mchanganyiko wa kifamilia kweye daraja la kwanza na pili (lakini daraja la tatu ilikuwa ni mchanganyiko haswa - a.k.a kajamba nani).

Nikawa nazungumza ya yule abiria mwingine aitwaye John (siyo jina lake) kuhusu safri za baharini na mazingira ya huko tuendako, yule mzee wa makamo alikuwa bize na magazeti na dada alikuwa ametulia tu (sura iliyofura kwa hasira na labda woga.

Hali iliendelea hivyo hadi tulipotoka "nje" kabisa (nje = mbali na ufukweni / bandarini).

Hali ya bahari mara ikaanza kubadilika, upepo mkali ulikuwa unavuma lakini hakukuwa na mvua, bali mawimbi yalianza kuongezeka ukubwa. Nikamsikia John akisema "bora MV Lindi" haiyumbishwi sana, lakini hii leo tutakoma..."

Abiria huyu (John) niliyekuwa naongea naye alikuwa ni mwenyeji wa Mtwara na anapajuwa Lindi vizuri. Niliendelea kumuuliza maswali kadha wa kadha na yeye alikuwa akijibu kadri ya alivyokuwa anajuwa.
^^^^^^^^^^

Mara tukaona yule dada kama anahangaika hivi hatulii (akiwa amekaa), kisha akainamisha kichwa. Dada huyu alikuwa mweusi kiasi, ki umri alionekana mkubwa kwangu kama miaka miwili hivi, alikuwa amevaa gauni la rangi ya kahawia yenye "V" shingoni na mikono mifupi, halikuwa gauni refu sana lakini lilifunika magoti, alikuwa amevaa viatu ya kawaida vya ya rangi ya udhurungi vya kutumbukiza na hakuwa na mizigo bali begi lake la mkononi ambalo lilikuwa kubwa kiasi.

Ghafla yule dada akafungua mlango akatoka nje, mie nikabaki nashangaa, jamaa yangu akaniambia kuwa amezidiwa huyo ameenda kutapika. Jamaa akaniuliza kama nilishawahi kusafiri majini, nikamjibu hapana, akaingiza mkono kwenye mkoba wake akatoa ndimu ananipatia, akaniambia ukihisi kichefuchefu nusa hiyo ndimu.

Tulikuwa tayari tumeshakuwa mbali kabisa na nchi kavu na jua la magharibi lilianza kuonesha miale yake mizuri ya dhahabu, hali ya bahari bado haikuwa shwari, mawimbi yaliendelea kuzidi.

Mara yule dada akarudi huku akihema na kuyumbayumba, akaketi, 'akajiinamia'

Wakati huo wote hatukuwa tumeongea naye, alionekana kama ana kisirani fulani hivi hivyo tuliepusha kubadilishana lugha zisizofaa.

"Dada, chukuwa hii, inusenuse itakusaidia", hatimaye nilivunja ukimya kwa kumpa ile ndimu niliyopewa.

"Ahsante" alisema huku akinyoosha mkono na kuichukuna na kuanza kuinusa. Lakini haikupita muda akainuka tena kwenda nje, safari hii nami nikamfuata. Akaingia maliwatoni, nikawa namsubiria kwa nje. Haikupita muda mrefu akatoka, akaniuliza na wewe unataka kutapika? Nikamjibu hapana, bali nilikufuata wewe nilidhani utahitaji msaada.

Ikawa sasa tumefungulia mzungumzo, nikamwambia , tusirudi ndani, tushuke daraja la tatu labda utapata nafuu. Tukashuka, lakini haikusaidia, kila akiona mtu anatapika naye anajibu kwa kutapika (kwa wale wasafiri wa mara kwa mara wa majini wanafahamu hali hii)

Abiria walitapika sana, na meli ilikuwa imejaza haswa! Tukaamua kurudi kwetu huku tunayumbayumba.
=
=
=

Giza likaingia, hali haikutulia, baada ya muda kupita tukatangaziwa kuwa meli itasitisha safari kwa muda hadi kupambazuke, kisha ikaelekea bandari ya wapi sijui ndio Kilwa ikashusha nanga nje kidogo ya 'bandari'.

Maeneo tulipotia nanga bahari ilikuwa ya mawimbi madogo kiasi cha kufanya kuwa na utulivu mkubwa melini. Hakuna kutapika tena, na watu walianza stori za hapa na pale. Hamu ya chakula cha jioni ikàanza.

Abiria wengi walikuwa wamebeba vyakula vyao, lakini mimi sikubeba chakula, wala yule jamaa yangu (John) wala yule binti. Tukaenda wanapouza vyakula (ndani ya meli) tukanunua wali mbaazi na kurudi chumbani na kuanza kula. 'Mchele kitumbo' haukuwa na ladha tamu lakini mbaazi zilikuwa tamu balaa . Yule 'mzee wa magazeti' akatoa vikopo vya nyama ya kopo na biskuti zake na juisi (orange squash) akachanganya na maji ya kwenye bomba akawa anakula na kunywa. Alitugawia sote ile juisi, ilikuwa nzuri sana na katika kuzungumza naye tukajifunza kuwa alikuwa ni askari wa Jeshi la wananchi.

Poleni kwa maelezo marefu, sikuwa na hata wazo la kula 'tunda kimasihara' hadi hapo.
^^^^^^

Katika mazungumzo na huyo dada nikajuwa kuwa anaelekea Lindi pia, ameajiriwa na ndio 'first appointment' yake lakini alienda Dar Utumishi kufuata nyaraka zake nyingine muhimu, hivyo hii kwake ilikuwa mara yake ya pili kusafiri baharini, na Lindi pale ni Mwalimu katika Shule ya msingi fulani hapo mjini.

Tuliendelea na stori za hapa na pale hadi usiku wa manane yule dada akawa hoi kwa usingizi, tukamruhusu apande 'deck' ya juu kulala. Yule mzee naye akajilaza chalichali 'deck' ya chini, mie nikapanda deck ya juu yake na chini ya yule dada akalala jamaa yangu John.
=
=
=

Nilistushwa na honi ya meli, kuchunglia dirishani kumbe kumekucha kabisa, na meli ilikuwa inang'oa nanga.

Hali ya bahari ilikuwa shwari kabisa. Nilipiga mswaki (kutumia dawa ya meno bonamed) na kunawa uso, wengine pia walifanya hivyo na safari iliendelea tukiwa sasa tumezoeana kama tuliwahi kufahamiana kabla.
=
=
=

Hatimaye meli ilifika Lindi bandarini. Tuliamua kuongozana wote pamoja wakati wa kushuka kwenye meli. Tulikaguliwa (ukaguzi wa kawaida) na maafisa wa bandarini kisha kuruhusiwa kuendelea.

Mbele alikuwa yule mzee, akifuatiwa na John, mimi kisha yule dada. Nikaiona Lindi na watu waliochangamka. Tukafika sehemu za kuegeshea magari na teksi.

Yule mzee alifuatwa na Landrover 108 chasis fupi ya jeshi, tukabaki watatu (ofcourse pamoja na abiria wengine wengi waliokuwa aidha wakiwasubiri wenyeji wao ama usafiri, wengine waliendelea kutawanyika kwa kutembea.

Dereva mmoja hivi mtanashati akatufuata na kutusalimia, "mnaelekea wapi nikupelekeni?" Aliuliza. Kwa kuwa tulikuwa tumesimama pamoja alidhani safari yetu ni moja yule, John akamjibu tupeleke posta kwanza (siyo mbali kutoka bandarini), kuna simu alikuwa anataka kupiga.

Enzi hizo simu zilikuwa za waya, unaenda Shirika la "posta na simu" unaikuta simu zile za kuingiza sarafu. Waliobahatika walikuwanazo zile za kukoroga (unazungusha 'hendeli" kisha unapokelewa na mhudumu anakuunganisha na namba unayotaka. Baadaye zikaja zile za mezani za kukoroga kwa namba, hii ilikuwa ya kisasa sana enzi hizo)

Ukimpata 'operator ' wa simu, naye anahangaika kukutafutia namba uliyotaka, akiipata ndipo anakupigia hapo ulipo (kama ni kibandani au nyumbani ama ofisini) kisha anakuunganisha. Haikuwa ajabu kusubiri kwa zaidi ya nusu saa kupata namba unayotaka.
^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^

Tukaingia kwenye teksi, dada mbele, sisi siti za nyuma na dereva akachukuwa sanduku langu na mkoba wa John akaweka kwenye buti. Hao tukaanza kuelekea Posta.

Teksi ikafika Shirika la posta na simu, John akaenda ndani, kwenye teksi tukabaki watatu, yaani, dereva, yule dada na mimi. Dereva wa teksi alikuwa mcheshi na mzungumzaji mno, alituuliza habari za safari tukamjulisha hali ilivyokuwa, tuliendelea na stori mbili tatu, hatukuwa 'bored'

Baada ya nusu saa kupita yule dereva akasema ataongeza gharama ya muda wa kusubiri. Alikuwa dereva mstaarabu sana, nakumbuka jina lake mpaka leo, ndugu Mansoor. Teksi yake aina ya Peugeot 404, nafikiri ndiyo ilikuwa teksi iliyopambwa vizuri kuliko zote Lindi kwa wakati huo. Ilikuwa ya rangi ya maziwa, ndani kwenye 'driving mirror' alining'iniza sanamu ya ndege (shorwe) wa plastiki ambapo gari ikiyumba ile sanamu inatoa milio fulani hivi kama ndege wa porini, tairi zina 'wheel cap' nzuri za silva pia nyuma ameweka antena ya redio ndefu na uzito kidogo nchani na kuifanya iwe inayumbayumba. Hakika alikuwa anaipenda teksi yake. Wahenga wa waliokaa Lindi miaka hiyo ambao wamo humu watakuwa wanamfahamu Mansoor 'dereva teksi.'

Baada ya kama dakika kumi, John akaja, akutuambia bado hajapata simu aliyokusudia, hivyo alishusha mkoba wake, akaniachia noti mbili za shilingi kumi (20/-) na kuturuhusu tuendelee. Aliniuliza nitafikia wapi, nikamwambia kuwa nina mwenyeji wangu yupo National Housing baada ya kupanda mlima 'wapiwapi' (just a hill) laini namba (kapuni) nyumba namba (kapuni). Aliahidi kunitafuta kwa ajili ya kuendeleza urafiki.

Tulimwacha akiingiza mkoba wake ndani na kuendelea kusubiri simu, sisi hao tukaondoka. Nikamuuliza yule binti anashukia wapi, akajibu yeye anakaa maeneo ya Sokoine ndani ya hospitali. (hakuwa nesi) bali kuna ndugu yake ni daktari amefikia kwake. Lakini alitaka aende 'somewhere' Likotwa kufuata mayai kwanza (kulikuwa na ufugaji wa kuku wengi maeneo hayo), hivyo ruti tukaamua tuende Likotwa (sijui jina nimepatia maana ni miaka mingi) kisha turudi National Housing halafu amalizie Hospitalini.

Hadi muda huo wazo la kula tunda kimasihara wala halikuwepo, ilikuwa ni ujamaa tu ambao Nyerere alikuwa anajaribu kuujenga na wiki mbili baadaye nilimuona Nyerere "live" kwa mara ya kwanza pale Rahaleo uwanjani alipozuru Lindi.

Baada ya kuchukuwa mayai hao tulirudi hadi nyumba za 'National housing', tukapinda kulia kuacha njia kuu, tukafika 'line' husika tukapinda kushoto kuingia mtaani, macho yangu yote kwenye namba za nyumba, hatimaye nikaiona nyumba lengwa.

Kama mnavyojuwa nyumba za 'neshinali' wakati huo, zimenyooka kwenye mstari na nyumba mbili zimeungana (kwa hadhi ya nyumba zile), ukiingia unakutana na sebule, kushoto chumba na kulia chumba, kuna choo na bafu na jiko. Ndani kuna vitanda vya chuma "banco". Kulikuwa na mabakuli makubwa imara sana yameandikwa TG na messtin imara sana pia imeandikwa TG, jiko la "stove", taa za kandili pamoja na pasi chapa jogoo (ya mkaa).

Kulikuwepo na "kiti cha uvivu" kimoja (wahenga wanavijua hivi, siku hizi vipo vichache sana), pia ilikuwepo meza ndogo ya kahawa pamoja na viti viwili vya mbao mninga vya kukunja. (Kadiri ninavyoandika nakumbuka mengi lakini siwezi kuandika yote ngoja niwahi kwenye 'masihara")

Mlango husika ulikuwa umefungwa na hakukuwa na dalili ya mwenyeji ndani, nikashusha sanduku langu, mara akatokea jirani akatukaribisha na kunijulisha kuwa mwenyeji wangu amepatwa na dharura kidogo ameenda Mnazi mmoja huenda atarudi kesho, akanikabidhi funguo.

Kuanzia hapa shetani akaanza kufanya kazi yake, nikajikuta namwambia yule dada ashukie hapa tupumzike kidogo kisha nimsindikize kwake ambapo hapakuwa mbali kwa kutembea.

Nikamsaidia kushusha trei zake tano za mayai, nikamlipa dereva teksi hela yake na chenji nilimuachia (shilingi 5, hela ndefu wakati huo).

Jirani atakusaidia kuingiza sanduku langu, mie bize na mayai, dada na mkoba wake. Pale sebuleni jirani akatuacha akatoka kuendelea na mambo yake.

Wote tukawa tunashangaa shangaa mandhari ya ndani ya nyumba, hapakuwa vitu vingi kama nilivyoeleza hapo juu. Akiwa amekaa kwenye kiti nami kwenye kiti kingine tulipiga stori mbili tatu za kawaida huku nikimuangalia sasa kwa jicho la tatu.

Dada ameumbika vizuri, macho angavu, ndipo nilipoanza kuona kiuno kilivyogawika vyema, mtoto wa Kinyamwezi kutoka Tabora, kifuani chuchu saa sita na robo, 'mgongo' bambataa linalochipukia, rangi nyeusi asilia, nywele nyeusi zimefungwa mtindo wa 'mabutu', very simple and natural. Hakika Rose (siyo jina lake halisi) alikuwa ameumbika sana.

Nikawasha redio ya mbao (all transistor radio), stesheni ya Radio Tanzania, kisha nikamuacha sebuleni akiangalia magazeti yaliyopo kwenye meza ya kahawa nikaanza kukagua nyumba, chumba kimoja kilikuwa wazi (kimeshindikwa tu) na kingine kilikuwa kimefungwa kwa funguo (chumba cha mwenyeji), nikaingiza begi langu chumbani.
Trei za mayai pamoja na mkoba wake nikaweka chini ya meza (lakini siyo sakafuni), kisha nikaenda jikoni. Nilikuta kumeandaliwa staftahi (chai kwenye birika la bati, mikate, jam na Tanbond)

Nikaenda maliwatoni, nikaona pako sawa, nikarudi sebuleni ili kumuonesha 'dada' Rose wapi choo kilipo kisha nikawasha jiko (stove) kwa ajili ya kupasha chai. Chai ilikuwa inanukia vizuri sana (green lebel)

Ikumbukwe kuwa mwenyeji wangu alikuwa anatarajia niwasili mapema asubuhi lakini tulilazimika kuchelewa kwa sababu ya hali ya hewa (dhoruba) baharini.

Rose alivyotoka maliwatoni akanifuata jikoni, akaanza kunisaidia 'kuandaa meza'

Hakika tulikuwa na njaa, na tuliifakamia mikate yote iliyokiwepo jikoni.

Mida ilikuwa imeenda na matumbo yalikuwa yameshiba vyema. Kushiba kwa tumbo kulianzisha njaa nyingine ambayo sasa shetani alikuwa bega kwa bega nami....

...Nikamwambia akaoge, maana joto lilikuwa kali, chai pamoja na safari. Akaingia chumbani kujiandaa, mie nikabaki sebuleni nikisikiliza redio.

Hakyanani, kuna wanawake wameumbika jamani, 'si kwa Singida Dodoma ile', alipita amevaa khanga mbili, moja kajifunga kiunoni na nyingine amejifunga kuzuia matiti. Matiti yake hayakuhitaji sidiria japo alivaa wakati tupo safarini, sasa niliyaangalia vizuri japo yalifunikwa na khanga ya juu. Huku mnara mie upo juu hatari huku ukinesanesa ndani ya chupi yangu ya 'jinja' na kunifanya nihisi maumivu, fasta nikaingia chumbani na kufungua begi langu na kuchukuwa taulo na kujifunga baada ya kuvua nguo nilizovaa.

Paaap, nikaibana 'pipe' (dushe) kwa juu na taulo kuzuia Rose asione na kuifanya pipe isinesenese (kwa mtindo ule wa nataka tena)

Alichukuwa muda mrefu bafuni, sikutaka kumfuata; alipotoka nami nikaenda bafuni kuoga, nikaonana ameanika chupi yake 'zaiboni', nikainusa, hahahha , nikairudisha alipoianika, nilioga fasta na kurudi chumbani na kuingia bila hodi.

Lahaulaaaa, nilimkuta ameinama anapaka mafuta miguuni, alishtuka na kusimama, "jamani James ungebisha hodi nijifunge..." Alisema huku akijaribu kuchukuwa khanga iliyopo kitandani.

Hakuiwahi, tayari nilikuwa nyuma yake nikiwa nimejifunga taulo na kumkumbatia kwa kumshika tumboni kwa mikono niwili.

Nikambusu nyuma ya shingo yake, akageuka kiasi kama anataka kuniangalia, nikambusu shavuni na kumwambia naomba leo ubaki hapa unipikie chakula cha jioni, kesho ndipo uende kwenu Sokoine. Alisitasita lakini hatimaye alilainika. (Weweeeee)

Wakati nambembeleza abaki, nilikuwa natalii mbuga zote kuanzia kaskazini hadi kusini, bahari ya hindi hadi ziwa Tanganyika, by then sikuwa na elimu kubwa ya mahaba japo baadye sana nilipata fursa ya kusoma baadhi ya vitabu mfano "the perfumed garden" na "French sex art manners" nk. vilivyonipa ujuzi wa kutosha, katika maisha yangu nimewapagawisha sana wanawake.

Kwa uhaba huo wa ujuzi kimbilio langu lilikuwa matiti, makalio, kin*embe. Sikuwa najuwa habari ya "password" (nywira), kunyonyana ulimi, kupiga deki wala nini. Niliendelea kutomasa tomasa nikiwa nyuma yake mikono nikiwa nimeshusha 'Ikulu' yake, kiwanja cha mpira nikifanya fujo za hapa na pale, mara akageuka akaniambia ninyonye titi hili, 'dakeki..., nilinyonya chuchu ile kiboya boya kisha nikahamia chuchu ya pili...

Wakati huo hatukuwa na hofu ya maradhi yatokanayo na ngono, hakuna habari ya condom, tishio lilikuwa ni kisonono na kaswende ambapo pia siyo wengi walikuwa wakiugua.

Rose akaanza kupagawa kama amepatwa na maruhani, macho legelege, miguu yake ikaanza kukosa nguvu, akaniambia siwezi kusimama tena, nikamlaza kidandani na kuendelea kunyonya chuchu zake ndefu nyeusi. "Endelea vivyo hivyo lakini kwa taratibu" alisema. Mnara wangu tayari ulikuwa hauwezi tena kuvumilia, nikatoa taulo tupa kule chini, akaa mkao pendwa chali, huku amekunja miguu na kuitanua kiasi. Da! Kitumbua hiki hapa kimetuna na kimenona, kis*mi kimesimama vyema (visimi virefu type), nikamshikisha dushe ili aingize, aliposhika dushe alitoa macho huyo! na kuguna mmh, akaanza kuiparaza paraza hadi ikapata utelezi, akasema ingiza...

Nilipata tabu kidogo kupenya na ile naingiza tu, sidhani kama hata tako 23 zilifika, mabeberu hawa hapa! Akaonesha kama kushangaa hivi lakini "sekunde chache" tu dushe likaanza 'kudhikiri' tena likiwa bado ndani ya papuchi, akasema "he!" (Ile ya kushangaa)

Nilipampu nje ndani nje ndani, Rose alilia milio yote, ile miguno ya chini kwa chini siyo sauti kubwa, nilisugua haswa, shuka likaloa, kitanda kilikuwa kinaninyima uhuru wa kupiga mikito vizuri, mneso ulikuwa mkubwa, kwa wanaojuwa vitanda vya chuma vya banco vya wakati huo wanaelewa, nikamwambia tushushe godoro chini, tukavuta shuka upande ili tupate sehemu kavu, hapo Rose ameshako*joa mara kadhaa mie bado (sijamwaga la pili)

Niliendelea na kifo cha mende safari hii nikiwa nafika vizuri napotaka huko ndani, mara nikamuona ananikwaruza mgongoni na kunikandamiza, mzee baba nikadidimiza yote, pipe ikawa inabanwa na kuachiwa mara kadhaa mara akalegea mikono na kuhema juu kwa juu kama vile mtu anayekosa pumzi (oxygen); kwa kubanwa na kuachiwa kule kwa dushe nikaona mabeberu haooo mbioni, nikaongeza tako kadhaa mara haooo!

Nikawa hoi nami, nikiwa juu ya kifua chake, dushe ndani, akaanza kuifinyafinya dushe huku akiniangalia na kutabasamu , nikamuuliza nitoe, akasema subiri. Sekunde chache baadaye dushe likaanza kunywea akaniambia toa. Taratibu nikatoa dushe huku yeye akiifuta na khanga yake, kisha nikainuka.

Tukaenda bafuni wote, tukaoga na kuchezeana sana hadi dushe likasoma mnara maximum, tukaelekea chumbani fasta, akashika "mfumbati" wa banco, (chuma mboga), nikalambisha kwenye kin*embe kama vile nakosea pa kuingiza akaishika na kuizamisha...

Nilikandamiza akaruka kwa kusogea mbele, akaniambia usizamishe yote, nikawa napiga ndani nje kwa kuzingatia atakavyo, mtoto wa Tabora akaanza kuonesha ujuzi wa 'kulisakata rhumba', mie nikawa sina kazi kubwa nime relax huku yeye "akishika hatamu ya uongozi", mara namuona ananiangalia huku ametumbua mijicho utafikiri mjusi amebanwa na mlango na sauti ikaanza , aaa, aaah , Aaah AAAAH huku ikiongezeka volume na ni ile sauti ya kutokea kifuani (siyo mdomoni wala kooni, kwa wanamuziki wanaelewa)

Papuchi ilikuwa chapachaa, mie dushe bado limedisa 'to the maximum', misuli ya dushe imesimama balaa huku ikiwa imefunikwa na bao la "Rose" sehemu sehemu, nikazidi kupampu, akasema amechoka miguu haina nguvu, nikamwambia anipandie juu nikalala chali. Akajivutavuta akapanda, kuingiza kitu na boksi, K ya motooo, dushe likaenda kugusa sehemu akasema aakh, kisha akanilalia kifuani akaanza kupiga tako yeye, nafikiri ilimsaidia dushe lisimguse sehemu ya ndani zaidi maana alikuwa ana control yeye kiwango cha 'penetration.'

Aliendelea kufanya ufundi wake hadi wazungu wakaja.
^^^^^^^^^^^^^^^^^^

Rose alikuwa mtamu sana, hakuwa 'sealed' lakini papuchi haikuwa na 'mileage' nyingi.

"James umenito*mba vizuri yani nimekojoa mara nyingi haijawahi kunitokea, halafu mbo*o yako tamu sana, inajaa vizuri" aliniambia, nami nikamsifia kwa kuwa na papuchi safi na yenye mileage ndogo, ndipo akaniambia alianza kutumika Chuo cha ualimu na boyfriend wake wa kwanza ambaye bado yupo naye lakini amepangiwa kufundisha Mkoa wa Tanga na yeye ndio amepangiwa Lindi miezi sita iliyopita.

Hapa ndipo akafunguka kuwa anaishi na baba yake wa hiyari ambaye ni daktari hospitali ya Lindi (rafiki wa baba yake mzazi)

Alifunguka pia kuwa alikuwa ana miezi kadhaa tangia atoke chuo cha Ualimu Tukuyu hawajakutana tena na boy friend wake ambaye walipanga wataoana, wanawasiliana kwa barua.

Tukaongea mengi, hasa kutaka kumjuwa yeye zaidi, baadaye akaelekea jikoni kuangalia chochote cha kupika.
=
=
=

Tulilala hapo, kesho yake ndio nikamsindikiza kwao.

Niliendelea kufaidi utamu wa Rose hadi nilivyoondoka Lindi wiki nane baadaye.

Tuliendelea kuwasiliana kwa barua hadi niliposafiri ughaibuni nikawa bize na masomo, nilivyomkumbuka nikamuandikia barua ambayo haikujibiwa hadi leo.

Sijui ilimfikia ama watu wa posta walivyoona barua toka ng'ambo wakaichana wakidhani watakuta Paundi?, sijui aliipata akanipotezea?, sijui alifariki?

Popote ulipo Rose nakukumbuka sana, kama umo humu Jf kwa maelezo haya lazima utakuwa umejijuwa. Nitafute PM "nikupe zawadi zako kutoka Uingereza"

Bila shaka sasa atakuwa umestaafu Serikalini kama mimi.
^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^
^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^
~~~~MWISHO~~~~

Angalizo: Picha hauna uhusiano na stori
IMG-20200121-WA0001.jpeg


James Jason
 
.... Hamida.....


SEHEMU YA PILI
******************

Kabila langu ni Taturu, baba yangu alibahatika kufanya kazi na Padri fulani mkoa wa Singida, hivyo masikio yangu yalinusurika kutobolewa, mimi pamoja na mdogo wangu niliyemuachia ziwa.

Miezi kadhaa nikiwa nimerudi nchini kutoka masomoni Ulaya, nikiwa mwajiriwa wa RTC maarufu kama UGAWAJI enzi hizo (siyo TRC), nilimtafuta Rose (wa Lindi; stori yake ipo kwenye uzi wa kula tunda kimasihara), Rozi hakujibu barua zangu tangia nilipo kuwa Ulaya. Miaka mitano ilikuwa imeshapita sasa.

=

Rose nilimuacha Lindi na kurudi Dar es Salaam baada ya kuwa naye Lindi kwa uhusiano wa mapenzi motomoto ya miezi miwili. Nikiwa Dar tulikuwa tunawasiliana kama kawaida lakini sikupata bahati ya kuonana naye ana kwa ana hadi leo hii ninapoandika haya.

=

Nilikata tamaa ya kuendelea kumtafuta, kazi yangu nayo ilichangia kwa kuwa nilikuwa bize mno hususani baada ya kurudi masomoni na kupandishwa cheo...

Labda mchumba wake aliendeleza uhusiano wao na kumuoa, hivyo aliamua kukata mawasiliano, hii ndiyo dhana kuu niliyobaki nayo, nahisi mtoto wake wa kwanza ni damu yangu.
************************

James mimi nilikuwa "kiwembe" sana kabla ya kukutana na Rose, umri wa kuoa ulikuwa umeshafika hivyo nilidhani kwake Rose ningehitimisha useja.

Baada ya kukata tamaa niliamua kuendeleza wimbi la 'ubazazi', kutembea na kila binti mrembo niliyemtaka...

Uingereza 'sikutembea' hovyo, nilikuwa na girl friend mmoja tu mwanchuo mwenzangu aliyetokea Hispania, Sue Parterson. Miss Sue ndiye aliyenipatia kitabu "Frech Sex Art Manners" kilichoandikwa na G. Valensin, nilijifunza mengi lakini uhusiano wangu na binti Paterson haukuwa wa malengo ya mbali, hivyo niliachana naye miaka miwili kabla ya kurudi nchini (nilidumu yaye kwa miaka miwili na miezi tisa hivi) ambapo nilienda Kaskazini zaidi kuchukuwa post graduate diploma fulani.

Enzi hizo kabla ya kwenda Ulaya hususani Uingereza, kulikuwa na utaratibu wa kupata semina fupi pale British Council, kwa ajili ya kuwaweka sawa kukabiliana na mazingira ya huko. Nakumbuka pamoja na mambo mengine tulifundishwa kufunga tai (japo nilikuwa najuwa kabla)

Nilivyorudi Tanzania, nikapewa nafasi nzuri katika RTC (Regional Trading Company), nikatumia kufahamika kwangu na umuhimu wangu kujipatia mabinti warembo kila uchao hadi siku hiyo moyo uliponilipuka kwa kumuona Hamida.
*************************************

Makatibu Kata walitusaidia sana katika kazi zetu, nikazoeana na Katibu kata mmoja ambaye alikuwa Kata ya Magomeni.

Kulikuwa na mkutano uliandaliwa kati ya Uongozi wa Kata na wajumbe wa nyumba kumi kumi kuhusiana na hali ya upatikanaji wa bidhaa katika mkoa.

Nchi ilikuwa imetoka vitani, (Tanzania vs Uganda), hali ya uchumi ilikuwa imeyumba hivyo wajumbe walitakiwa kuwaandaa waananchi katika mashina yao kukabiliana na hali inayoanza kujitokeza.

Mzee Katibu Kata rafiki yangu nilipomtembelea afisini kwake, (nyuma ya Hotel Travertine hivi sasa) ndipo akaniomba nimsambazie barua kwa baadhi ya wajumbe Magomeni Mapipa; alikuwa hajisikii vizuri (alikuwa ana homa)

Magomeni Mapipa enzi hizo palikuwa maarufu sana, hapo ndipo kulikuwa na U-turn kubwa kwa ajili ya magari aina ya 'Ikarus' kugeuzia.

Mabasi haya pamoja na mabasi mengine yalikuwa yanamilikiwa na Shirika la UDA (Usafiri Dar es Salaam) ambapo walikuwa na mabasi yaliyotengenezwa na kampuni mbalimbali ikiwemo Mercides Benz (German), Isuzu (Japan), Ikarus (Hungary) nk.

Wanafunzi walikuwa wanapenda sana kupanda Ikarus, na waliyaita "ikarus kumbakumba" maana likija moja lilikuwa linapakia abiria wengi kwa mara moja. Mfano wake ni kama haya mabasi ya Kichina ya BRT yale marefu.
*****************************

Wakati nimechuchumaa nafunga viatu kamba huku nikimuangalia Hamida akiwa ameinama kuokota mtandio wake pamoja na bilauli zile, yule mama mwenye sauti nyororo nikamsikia akisema " Kwema huko?, taratibu mnatushtua na presha hizi..."

"Ziliniponyoka, ngoja nikazisuuze tena nizilete"

Hamida alijibu, nikaisikia sauti yake nyororo akiongea sentesi nzima.

Maa shaa Allah kumbe naye ana sauti kama ya yule mama Mwarabu.

"Kwaheri Hamida"

Nilijikuta nimeropoka huku nikirudi kinyumenyume kuelekea mlango wa kutokea nje. Hamida hakujibu kitu, aliinama na kugeuka akaelekea uani (siyo maliwatoni), mtandio alijifunika kichwani lakini kwa kuutupia tu.

Niligeuka na kuvuta mlango kwa ndani na kutoka nje.
***********

Mzee Burhani ni mjumbe wa nyumba kumi katika mtaa huo nilipotoka, ni mzee kwenye hekima na mcheshi sana, muislamu safi na mwenye kuipenda familia yake na jamii aiongozayo kwa ujumla.

"Salama leko"

Nilisalimia kama waislamu wanavyosalimia, waliitikia lakini mzee mmoja wa makamo akaniambia, wewe James inabidi ujifunze kusalimia vizuri...

Hatusemi salama leko bali tunasema Assalaam aleikum. Pale pale nikarudia

"Assalaam aleikum"
Wakaitikia tena kwa wingi.

"Inabidi usilimu kijana."
Mzee Burhani alidakia.

"Hahhaha" nilicheka, kisha nikamwambia kuwa ule ulikuwa ni 'mguu wake'

Kwakuwa haikuwa siri nilimueleza kuwa nilipitia nyumbani kwake na kuacha barua na kumpa yaliyo ndani kwa ufupi, kisha nami nikajisogeza kwenye benchi nikaketi huku nikiangalia wanavyocheza keram.
_____


SEHEMU YA TATU
*******************

Pale Shibam kwenye 'kijiwe cha kahawa' nilikaa dakika chache tu, 'niliwapiga' raund moja ya tangawizi wale wazee waliokuwepo pale kisha nikaaga na kuondoka kumalizia kusambaza zile barua nilizobakinazo.

Nilinyonga batavus yangu (aina fulani ya motorcycle) na kuwaka nikaendelea mitaa mingine.

Kabla ya machweo nilikuwa nimeshamaliza kazi niliyopewa na 'Mzee Katibu Kata', hivyo nilielekea moja kwa moja nyumbani.

Hapo Dar nilikuwa naishi kwenye nyumba za Shirika la nyumba (NHC) zilizokuwepo Magomeni Mapipa (jirani na Tanesco Magomeni), zilikuwa nyumba bora sana enzi hizo. Miaka mitano nyuma nilikuwa nakaa 'kota' zilizokuwepo jirani na kituo cha afya Magomeni Mapipa (hospitali)

Ilikuwa siku ya Ijumaa, jua limezama nami nipo ndani kwangu nikizinyoosha (kupiga pasi) nguo la kutokea usiku huo pamoja na nguo nyingine...

Ilikuwa ni nadra sana kwa vijana wa kariba yangu ifikapo mwisho wa juma (weekend) kuwepo nyumbani baina ya saa mbili na nusu usiku hadi saa sita usiku (wengine hadi alfajiri)

Nilikuwa mpenzi sana wa muziki wa dansi hususani DDC Mlimani Park Orchestra, hivyo kila jumamosi nilikuwa sikosi pale DDC Kariakoo, Magomeni Kondoa ama Lango la jiji.

Ijumaa hii nilipanga kwenda sinema, (Empire). Zama hizo kumbi za sinema ndiyo zilikuwa kimbilio letu kwa ajili ya kuburudika na filamu mbalimbali.

Starehe za sinema miaka hiyo kwa Dar es Salaam kimbilio la 'wanyonge' lilikuwa pale Oysterbay, Drive-in Cinema, ambapo screen ilikuwa kubwa na imewekwa juu sana kiasi cha kuweza kuonekana na watu wote hata walio nje ya ukumbi, hivyo wasiokuwa na uwezo wa kulipia kuingia (na magari yao), walikaa nje kwenye majani mafupi ama vumbini, wakifuatilia filamu, mbu nao walipata lishe ya kutosha.

Kulikuwa na kituo cha daladala eneo la Drive-in Cinema baadaye makondakta wa madaladala wakawa wanafupisha kuita jina lote na kupaita "drai"

Cameo, Empire, Empress, Avalon na Odeon cinema ni baadhi ya kumbi za sinema zilizokiwa maarufu sana Dar enzi hizo. Ratiba yangu wiki hiyo ilikuwa ijumaa kwenda sinema (Empire), jumamosi DDC kariakoo na jumapili kutulia nyumbani baada ya ibada kwa ajili ya maandalizi ya jumatatu kazini.
****************

Saa mbili kasoro robo (tuliita saa mbili kasorobo) nilikuwa tayari nimemaliza kazi muhimu nikafungulia redio (RTD) kipindi pendwa cha michezo, nakumbuka siku hiyo kilitangazwa na Julius Nyaisanga (R.I.P)

Nilibahatika pamoja na vitu vingine, kurudi na radio cassete (music system) kutoka Ulaya. Kabla ya hapo nilikuwa na radio cassete ya kawaida pamoja na 'player ya santuri' (turntable). Kurudi na music system enzi hizo ilikuwa ni fahari sana...

Saa mbili na robo hivi baada ya kusikiliza taarifa ya habari na mazungumzo baada ya habari, nilikuwa tayari kutoka.

Nilichukuwa pikipiki yangu (batavuz) na kuelekea Butiama Restaurant kupata pilau safi ya moto kabla ya kuelekea mjini maeneo ya posta mpya (mtaa wa maktaba) ukumbi wa Empire kuangalia filamu ya Kihindi iitwayo Kurbaan. (Ile kurbaan ya zamani maana sikuhizi nasikia kuna kurbaan mpya na kurbaaniyan)

Filamu hiyo ilitangazwa kwenye kurasa za magazeti maarufu ya enzi hizo, pamoja na mabandiko (posters) kwenye ubao wa matangazo wa Empire.

Filamu nilizianza kuzipenda tangia nipo shule ya kati (middle school), kuna wamisionari walikuwa wanatuletea filamu ya maigizo ya maisha ya Yesu, na kule kijijini kwetu kuna wakati landrover fulani ilikuja na kutuonesha filamu ya namna ya ukulima bora, sikumbuki hata ilikuwa taasisi gani. Kuna baadhi ya viongozi na watu maarufu nilianza kuwaona kupitia filamu hiyo tuliyoletewa kijijini kwetu.
*************************************

Trela (trailer) ilikuwa imeanza tangia saa mbili, mie nilifika saa tatu kasoro kidogo tu, Saa tatu kamili filamu ingeanza.

Waonesha filamu enzi hizo walitumia projector kubwa sana zenye kutumia 'film' (mkanda kwenye magurudumu) kama kitunzia / chanzo cha picha. Mikwaruzo kwenye sauti na picha na chengachenga zilikuwa ni sehemu ya burudani pia kwani hakukuwa na namna bora zaidi wakati huo.

Nikakata tikiti (tiket / ticket) na kuruhusiwa kuingia ndani. Nikapanda ngazi fasta na kuangaza sehemu iliyokuwa wazi, nikapaona nikaenda kuketi; filamu ikaanza na wote tulianza kufuatilia.
***************************

Katika sinema za Kihindi, pamoja na uzuri wa maudhui, lakini pia nilikuwa napenda nyimbo zao. Lugha ilikuwa inatumika ya Kihindi, japo sehemu chache walichanganya na Kiigereza, hakukuwa na sub-titles za kutusaidia, bali kulikuwa na 'spoilers' ukumbini 'much know' sana na kuanza kuhadithia (uongo ulikuwa mwingi sana), usiombee uwe jirani nao! lakini bado tulikuwa tunafurahia.

Katika filamu hiyo pia kulikuwa na nyimbo nyingi, lakini kuna songi (wimbo) mmoja uliniteka hisia sana.

Natamani niwaimbie hapa lakini nimeusahau, ila nakumbuka 'tone' yake.

Kuna Mwimbaji mmoja maarufu sana wa taarabu (R.I.P) aliuiga kwa kuweka maneno ya Kiswahili, aliuta LEILA

Leila Leila Leila, Ewe wangu Leila, kila mtu hapa, akupenda wewe..

Huo ndio wimbo uliniteka sana kiasi cha kunifanya nimkumbuke Hamida...

Wimbo ulikuwa unaimbwa kwa Kihindi, lakini ulikuwa una hisia sana, nilijikuta nimetumbua macho kuangalia screen lakini mawazo yote ni kwa Hamida..., nitampataje Hamida! Kwa uzuri wake, bila shaka kila mtu anampende Hamida (niliwaza)

=

Kulikuwa na Mapumziko mafupi kwenye filamu hizo (half-time), waoneshaji walikuwa wana rewind mikanda na kuandaa mkanda mwingine kwa ajili ya muendelezo, pia kuwapa nafasi watazamaji kunyoosha miguu na kwenda maliwatoni, kununua viburudisho (bisi zikiwemo ), pia kutoa nafasi ya baadhi ya watazamaji kufuta machozi ama kurudi katika hali zao za kawaida maana filamu zilikuwa zinateka hisia haswa vile vile simema yenyewe ilikuwa ni ndefu (long play), ilitumia dakika 90 kufikia halftime.

Wakati wa halftime, nilimpata dada mmoja na kumshawishi tukae pamoja kwa kuwa siti niliyopata palikuwa na nafasi nne ama tano wazi, ilikuwa siti za katikati nyuma kabisa ambapo juu yake kulikuwa kunapita ule mwanga mkali ya projector.

Alikubali baada ya ushawishi mkubwa, alikuwa yeye na rafiki zake wawili wote wakitokea maeneo ya Upanga. Tukanunua bisi (pop-corn) na chingamu (chewing gum) na kurudi ukumbini.

Kipindi cha pili kiliendelea, na tuliendelea kufurahia filamu hadi mwisho. Ilikuwa saa sita na robo hivi usiku tulipotoka ukumbini.

Niliwalipia taksi (co-cabs) wale rafiki zake, siye kwa kutumia kibatavuzi hao tukawa tunawafuata kwa nyuma kuelekea makutano ya barabara ya maktaba na bibi titi (Ali Hassan Mwinyi Rd. iliitwa hivyo kabla), walikunja kulia kufuata barabara hiyo hadi mbele kidogo ya Redcross na kukunja kushoto...

Wao walisimama nyumba fulani nasi tukapitiliza kuitafuta barabara ya Umoja wa mataifa, tukakunja kushoto ili kuelekea faya ili tuikamate barabara ya Morogoro.

Saa saba na dakika chache tulikuwa tayari tumefika mtaani kwangu. Palikuwa kimya sana, kulikuwa na kile 'kibaridi cha Dar cha usiku', nikafungua mlango, nikaingiza pikipiki na kumkaribisha dada niliyekuja naye.

"karibu sana Egline" (siyo jina lake halisi), nilimkaribisha.

Egline alikuwa mtoto wa mwansheria fulani ambaye wiki hiyo alikuwa safarini Nairobi, hivyo siku hiyo walipata fursa nzuri ya kujivinjari walipotaka bila kikwazo, mama yao hakuwa na "noma". Wale rafiki zake kumbe ni watoto wa mama yao mkubwa, walikuja kumtembelea mama yao mdogo kutokea Same - Kilimanjaro.

Ndani nilikuwa nina vinywaji kwenye jokofu dogo (friji), kulikuwa kuna fanta, double cola, pilsner na brandy (Cognac ya Ufaransa) ambayo ilikuwa kwenye kabati lingine.
*******

Tuliamka saa tatu asubuhi baada ya kengele ya kwenye saa kubwa ya mezani (alarm clock) kulia....

Baada ya staftahi nilimchukulia teksi kwenda kwao...

Kulala na Egline ilikuwa ni starehe ya usiku mmoja tu. Usiku ule tulifaidi vinywaji na ngono kiasi, sikuwa vizuri kutokana na mawazo juu ya Hamida.

Naanzaje kumpata Hamida? Nazidi kujiuliza, nilitamani kumuoa kabisa kwa kuwa alikuwa na sifa zote za kuwa mke bora (kwa mujibu wa moyo wangu)

Mimi ni mfuasi wa Roman Catholic, niliyependwa sana na Padri Petro aliyekuwa anafanya kazi na baba yangu Mission ya Chemchem Iramba Singida, Padri ambaye ndiye aliyenisaidia sana katika masomo yangu kabla ya middle school na wakati wa middle school. Niliwaza.

Mimi, ambaye kabila langu ni Mtaturu (siyo Mnyaturu), Mwafrika mweusi, naanzaje kumpata Hamida. Hamida ambaye hata hajui kwamba kuna James anayemtaka, sembuse (seuze) kumuoa.

Mawazo yalinijaa hadi nikapitiwa na usingizi nikiwa sebuleni kwenye makochi. Nilikuja kushtuka ikiwa tayari saa tisa alasiri, njaa inauma.

Nikaenda kujimwagia maji, nikavaa kisha nikatoka kuelekea Shibamu.
*****************************

Itaendelea...
IMG-20200125-WA0000.jpeg
IMG-20200125-WA0003.jpeg


James Jason
 
SEHEMU YA NNE
******************

Bourne ni babu yake James, mzee wa Kitaturu (kabila linalofanana na Wamang'ati), wahamiaji kutoka kandokando ya ziwa Eyas, Manyara hadi kuja Iramba katika harakati za kutafuta maisha bora.

Jason, mtoto wa saba kati ya watoto kumi na mmoja wa mzee Bourne, alibahatika kufanya kazi na Padre (Padri) kwenye Mission fulani iliyopo Chemchem - Iramba. James ni mtoto wa kiume wa kwanza katika uzao wa Jason ambaye alikuwa na watoto watano, yaani Dada zake James wawili walianza kuzaliwa, kisha James, halafu mdogo wake James wa kiume na kitinda mimba alikuwa wa kike.

Elimu ya madarasani katika maisha ya wawindaji na wafugaji haikuwa kipaumbele, lakini kwa bahati nzuri kutokana na bidii ya mzee Jason, yule padri aliahidi kumsaidia watoto wake wapate elimu. Elimu hiyo ilimfanya James afike shule ya Sekondari Kibaha na kukaa huko miezi 10 na wiki mbili bila kurudi Kijijini. James anasimulia safari yake...
****************************************

Mwaka 1961 nikiwa nina miaka saba, dada zangu waliandikishwa kusoma shule ya msingi Chemchem, nami katika msafara huo niliwasindikiza tukiambatana na baba yetu Jason. Dada zangu wote walipimwa kwa kujishika masikio kwa kuzungusha mkono mmoja kichwani na kuweza kuyagusa masikio yao, wakaandikishwa. Kiumri dada zangu hao wakubwa wamepishana miezi kumi na minane tu kuzaliwa. Dada yangu aliyeniachia ziwa tumepishana miaka miwili.

Hamu ya kujiunga shule nami inanijia, nilitamani nami nivae sare zile za shule.

Nikajipeleka kwa Mwalimu muandikishaji, akaniambia shika sikio, aaah wapi! Sikulifikia, nikafanya hila na kulishika lakini aligundua na kuniambia wewe uje mwakani
=
=
=

Mwaka uliofuata nilimsumbua sana baba anipeleke kuniandikisha shule, hatimaye alifanya hivyo lakini kwa bahati mbaya muandikishaji yule yule alinikataa kwa kusema bado sijafikia 'umri', na kweli siku hiyo pia sikuweza 'kugusa sikio'.
**********************************

Nilishachoka kazi ya kuchunga ng'ombe mbuzi na kondoo, maisha ya kupigana chenga na nyoka wa porini ama kupambana nao, maisha ya kula ugali mgumu asubuhi kwa mlenda pori na kushinda bila kula hadi jua lizame, maisha ya kujitafutia matunda ya porini na kula kufidia pengo la njaa, maisha ya kufunga 'lubega' (kuvaa shuka moja jeusi kama kaniki), maisha ya kupiga miluzi na kelele kudhibiti mifugo isiingie kwenye mashamba ya watu... Nilikuwa nimechoka kwa kuwa sasa kazi ya uchungaji ilinielemea, dada zangu muda mwingi walikuwa shuleni.

Sikujali "mzigo" utamuelemea nani, nikamwambia baba kuwa nitaenda shuleni vivyo hivyo.

Siku iliyofuata nilienda kinyemela na kuingia darasa la kwanza na kukaa nyuma kabisa kwenye sakafu kama wanafunzi wengine huku nikiwa nimevaa lubega...

Huku nyuma baba alitafuta utaratibu wa ng'ombe kwenda machungani kwa kuchanganya na ng'ombe za jirani, pia alimuelezea Padri juu ya maamuzi niliyofanya. Padri alimuambia aniache waone itakuwaje.

Darasani siku hiyo sikuwa najibu chochote, lakini masomo nilikuwa nayaelewa vizuri. Siku ya pili tena nilienda shuleni, Mwalimu wa hesabu alikuwa anapenda kuuliza maswali mara kwa mara, nakumbuka kuna swali wanafunzi wenzangu liliwashinda mie nikanyoosha mkono na kujibu kwa usahihi. Mwalimu alifurahi sana.

Mwalimu wa hati naye alipoingia, wakati anakagua vibao vyetu vya kuandikia (tulianza kuandika kwenye vibao vyeusi vidogo, tulikuwa tunapewa chaki), alikuta nimeumba vizuri herufi zote alizotufundisha. Akachukuwa ubao wangu na kuondoka nao....

Sijui nini kiliendelea kwenye afisi (ofisi) za walimu lakini niliona siku chache baadaye baba ameniletea kaptula na shati (sare za shule), nilifurahi sana.

Wakati huo, siyo wazazi wote waliweza kuwa na sare za shule, kwa msaada wa Padri Petro mambo yalienda vizuri (Petro siyo jina halisi, na majina yote kwenye stori hii si halisi isipokuwa majina machache sana kwa sababu maalum)
****************************

Ilipofika wakati wa majaribio ya nusu muhula, nilipata masomo yote mia kwa mia na kuwa mwanafunzi wa pili darsani nikitanguliwa na Abel ambaye alikuwa wa kwanza. Muda wote wakati nahudhuria darasani nilikuwa siendi mstarini wala kufuata taratibu zingine za shule, wala jina langu halikuwemo kwenye 'rejista' ya mahudhurio.

Lakini baada ya matokeo hayo, jina langu likaanza kuitwa darasani, Padri aliniletea suruali ya mtumba aina ya jeans (rangi ya bluu), ilikuwa kama 'ovaroli' lakini isiyo na mikono, mikanda yake nyuma inaweka alama ya 'X' na mbele kifuati inaziba. Japo ilikuwa ndefu kiasi lakini niliifurahia sana.
******************************************

Baba alikuwa akifanya kazi ya kumsaidia Padri katika kampeni yake ya kupanda miti (alikuwa anatunza bustani ya vitalu)

Umbali kutoka kwenye 'boma' yetu hadi shuleni ni parefu kiasi cha kutembea saa nzima njiani. Tulikuwa tunakaa mbugani baina ya mto Sibiti na Misheni ya Chemchem. Nyumba zetu zetu zilikuwa tatu, nyumba za miti zilizokandikwa kwa matope yaliyochanganywa na kinyesi cha ng'ombe, sakafu nayo imesilibwa vizuri kwa "nilu" ya kinyesi cha ng'ombe, vitanda ni miti ilishoshindiliwa chini vizuri (matendegu) kisha juu kuwambwa ngozi ya ng'ombe. Nyumba kuu aliishi baba, mama na wadogo zangu, nyingine alikuwa anaishi babu, bibi alishafariki nikiwa mdogo, na nyumba nyingine nilikuwa nakaa mimi na dada zangu. Nyumba zote zilikuwa zimeezekwa kwa kuwekwa miti na kujaza udongo (tembe), kando ya nyumba hizi ndipo kulikuwa na zizi la mifugo ambalo uzio wake ulikuwa majani ya miba.
Tulishazoea maisha hayo na umbali kutoka boma hadi boma palikuwa parefu sana.
*****************************************

Niliendelea na msomo na kufanya vizuri darasa na nne mwaka 1965 na kuchaguliwa kujiunga na midle school Tabora.

Januari 1965, Padri Petro alinifuata nyumbani kwa ajili ya kunipeleka Kinampanda kwa usafiri wa pikipiki (BMW), tulikuwa tunaiita tukutuku, ina shafti ya mfumo wa upeleshi (propeler shaft) na kitu kama maboksi mawili nyuma kila upande ambayo yalikuwa hayaondolewi muda wote. Ilikuwa pikipiki ya rangi ya kijani iliyoiva.

Kwa mara ya kwanza nilipanda pikipiki (na chombo cha moto kwa ujumla), kabla ya hapo nilikuwa napanda mikokoteni ya kuvutwa na ng'ombe kwenye harakati za kupeleka mazao mnadani ama mambo ya shambani, ujenzi, na usafirishaji wa vitu vingine.
********

Niliagwa vizuri na familia, mama yangu alinihusia niwe na tabia njema na kusoma kwa bidii, dada zangu walikuwa wananipungia mikono huku machozi yakiwalengalenga, Babu alisemasema maneno yake (Kitaturu cha ndani - 'kubonga' ) ambayo sikuwa nayaelewa kisha akaniambia "nenda salama mjukuu waku na Mungu akusaidie", mdogo wangu wa kiume niliyemuachia ziwa alinipa mkono na kunitakia safari njema, wala hakuniangalia sana, aliingia ndani.

Nikiwa nimemshikila Padri vyema, huku nimevaa fulana na jeans yangu ambayo sasa ilikuwa inanitosha vyema, niliangalia nyuma na kuona boma letu na familia wakiwa bado wananipungia mikono, niliwapungia nami kisha nikamshikilia vizuri Padri.

Tukafika Chemchem 'Mission' akaniacha nje kwa muda, akaingia afisini kwake, na baada ya muda akaniletea peremende (pipi fulani hivi ) na kuniambia niendelee kumsubiri.

Alivyorudi tuliendelea na safari, tulivuka mito mikubwa miwili ambayo kwa wakati huo haikuwa na maji yanayotembea (mito ile hupitisha maji kwa wingi sana wakati wa mvua lakini ndani ya siku ne au tano maji huisha. Wanakijiji hutumia maji hayo kwa matumizi mbalimbali. Maji yakikauka mtoni, wanakijiji huchimba kwa kutumia mabakuli ya bati ama mabakuli ya kienyeji (wanaita 'vipeyu'), kiasi cha futi moja ama mbili kwenda chini unakutana na maji, ila kiangazi unaweza kuchimba hadi meta (mita) moja na nusu. Lakini sisi kule mbugani unafuu tulikuwa tunaupata wakati wa mvua tu, nyakati za kiangazi ilibidi kutumia mifugo na mkokoteni kufuata maji sehemu za mbali.

Maisha yalikuwa yenye changamoto nyingi, msimu wa njaa kali nikiwa darasa la nne tulikuwa "tunashindia" viazi vilivyo menywa na kukatwa slesi kisha kukaushwa juani, mengine huchemshwa kwanza (makela / chepe, mapalage, matobolwa), kupopoa mabuyu kisha unga wake kutengeneza 'uji' ilikuwa kawaida, kula matunda ya "mihama" (palm), ambayo tembo huyapenda sana kuyala, ilikuwa ndio pona yetu machungani. Mizizi ya mimea fulani (ilonge) hizi nayo ilituokoa nyakati hizo, matunda pori aina mbalimbali yalitusaidia, hususani 'mitogo' ambayo ilikuwa na sukari na unafaguna kama bigijii (big G)
***********************************

Safari iliendelea tukapita kijiji cha Ibaga, Mkalama, Gumanga kisha tukaacha njia ya kuelekea Nduguti na kushika njia ya kulia na kuukabili mlima mrefu ambapo tulipoupandisha dakika chache baadaye tukafika Kinampanda (Mission), tulipokelewa na masista wa Kilatino (Latin American nuns) (nilijuwa baadaye sana)

Nilioneshwa ukarimu mkubwa sana pale, chakula kizuri na kuoneshwa chumba cha kupumzika. Padri Petro baadaye alikuja kunijulisha kuwa safari nyingine itakuwa kesho kuelekea Singida mjini kisha Itigi ambapo nitapanda treni kuelekea Tabora.
******************************************

Kesho yake majira ya saa nne hivi, mimi pamoja na masista kadhaa tulielekezwa tupande gari fulani hivi (baadaye sana nilikuja kulifahamu kuwa ni UNIMOG - Mercedes Benz iliyotengenezwa "under licence" kutoka Argentina. Ilikuwa na rangi fulani hivi khaki iliyopauka.

Tulikwea nyuma (kwenye bodi) na kukaa kwa mtindo wa kuangaliana, kijana mdogo nikiwa peke yangu, masista wa kilatino walikuwa wengi na wachache walikuwa waafrika.

Safari ilianza, Padri Petro tulimuacha hapo, kabla ya safari alinipatia sanduku dogo ambalo aliniambia ameniwekea baadhi ya mahitaji yangu muhimu. Nilimpungia mkono wa kumuaga naye alifanya hivyo.
******************************************

Safari iliendelea hadi nilipoanza kuona 'bwawa' kubwa, ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuona bwawa la namna hiyo ambapo baadaye masista waliniambia lile ni ziwa dogo liitwalo Singidani.

Mji wa Singida ukaanza kuonekana vyema na nilifurahi moyoni kuona nyumba nyingi pamoja na nyingi zikiwa zimeezekwa bati.

Tukapita Bomani kisha tukaelekea Singida mjini, kuna sehemu tulisimama kidogo lakini alishuka "mzungu" mmoja aliyekaa mbele (hakuwa dereva), akaingia kwenye jengo fulani kisha baada ya muda mchache alirudi tuaendelea na safari kuelekea Itigi.

Barabara haikuwa rafiki, tuliwasili Itigi majira ya jioni, na wale masista wote walipanda treni ya abiria iliyotoka Mwanza kuelekea Dar.

Mie nikabaki na yule mzungu, baadaye aliniletea chakula na muda mfupi baada ya kula nilipatwa na usingizi...

Niliamshwa alfajiri wakati treni nyingine ya abiria iliyotoka Dar kuelekea Mwanza ilipokuwa inakaribia kuwasili. Muda wote wa kusubiri tulikuwa eneo la kupumzikia aribia pale Itigi Railway station.
********************************

Itaendelea...

James Jason
 
SEHEMU YA TANO
*******************

Yule mzungu alilichukuwa blangeti (blanket) alilonifukika nilipopitiwa na usingizi, na kuniambia nijiweke tayari huku akinikabidhi tikiti (tiketi) yangu. Ni kadi fulani hivi ndogo na ngumu sana rangi kama ya pinki.

Nikasikia sauti honi kali, 'bila shaka itakuwa ndiyo treni hiyo' niliwaza. Kweli muda si mrefu treni ikaanza kuonekana, ikapitiliza tulipokuwa tumesimama...

"Kumbe ndefu hivi!" Nilishangaa kwa sauti...

Pamoja na kupitiliza lakini bado niliona urefu uliobakia kushoto kwangu.

Haraka haraka nikaingia kwenye treni, behewa nililoingia lilikuwa limejaa sana (daraja la tatu), sikupata hata nafasi ya kumpungia mkono yule mzungu aliyenisindikiza.

Begi nilikuwa nimeweka kichwani na kulishikilia kwa mkono mmoja huku nikihangaika kutafuta nafasi ya kuliweka. Tulikuwa tumejaa sana kiasi kwamba hata kupiga hatua kusogea ilikuwa ni kwa shida.

Baada ya dakika chache nikasikia tena zile honi kali, safari hii zikiwa kali zaidi, ilipolia honi kubwa mara ya pili nikasikia psiiiiiiiiiiiiiii, chwaaaa! Nikayumba sana, kumbe ndio ilikuwa imeanza kuondoka.

Bahati nzuri baba mmoja akanionea huruma akaniambia shusha begi lete hapa, nikampatia, akalisokomeza chini ya siti aliyokaa.

Uhuuuu! Nilipata nafuu, nikamshukuru na nikaanza mchakato wa kusimama vizuri.
******

Safari iliendelea, huku nikisikia sauti "mziki" wa aina yake kwa jinsi gurudumu za treni zinavyopita kwenye reli. (Kata mti panda miti, kata mti panda miti..) Sauti hiyo iliendelea kusikika japo si kwa maneno bali hisia.

Kufika sehemu fulani, kukawa na utulivu mkubwa sana ndani ya behewa, treni nayo ilikuwa inaenda taratibu kuliko mwanzo...

"Sekenke hiyo..." Alisikia kijana mmoja akisema. Mie hata sielewi maana yake nini, lakini baadaye kidogo treni ilirejea kwenye mwendo wake wa kawaida.

Baada ya utulivu na nafasi kuanza kuonekana kidogo baadhi ya abiria walikuwa wanatembea kwenda mabehewa mengine, wengine walipita wakielekea msalani, kuna muda alipita mtu mwenye sare (siyo polisi) alikuwa anagonganisha vitu kama vijiko, nilisikia pia kuna hoteli humo humo (bafeti, kama alivyotamka mama mmoja) lakini sikupata bahati ya kwenda huko. Pia kuna wakati walipita watu wengine watatu wenye sare, mmoja akiwa ni askari, walikuwa wanakagua tikiti (tiketi / ticket), walipofika kwangu nilimpatia kisha akaiminya na kidude fulani hivi cha rangi ya silva na kuweka alama ya 'V' kwenye tikiti hiyo.

Baadaye nikajipenyeza katikati ya miguu ya abiria waliokaa na kufikia dirishani, nilichungulia na kuona mandhari ya mapori vya vichaka vifupi, treni ilipofika kwenye kona nikaweza kuyaona mabehewa karibuni yote vizuri zaidi.

Kwa saa zaidi ya sita safari iliendelea...
*********

Hatimaye tuliwasili Tabora, nilishuka na kuelekea sehemu ya abiria kupumzika, nilishangaa kuwaona watu wengi wenye ugonjwa wa akili, wajasiri-amali (haiandikwi wajasiria-mali) nao walichangamkia fursa ya kuwauzia abiria bidhaa zao...

Mara nikasikia tangazo lililonihusu kutoka kwenye kipaza sauti...

Nilifuatwa na watu wawili wa Kanisa la Morovian (MCWT), nikapelekwa hostel...

Kesho yake nikapelekwa Sikonge chini ya uangalizi wa MCWT na kuendelea na masomo huko hadi mwisho wa mwaka.

Nusu muhula nilibaki Mission ya MCWT Sikonge...

Disemba mwanzoni nilirudi Kijijini Iramba, safari hii nilipewa 'Warrant' (karatasi fulani hivi ya 'light blue') ambayo ilikuwa kama tikiti safarini...

=

Kufika Kijijini, familia yangu ilifurahi, yule Padri Petro aliondoka kurudi kwao Latin America, alikuwepo Padri mwingine ambaye hakupenda jinsi nilivyopelekwa 'Morovian...' badala ya 'Roman...' (Nahisi walikuwa na mpango fulani ambao sikuujuwa). Hivyo sikupata ushirikiano mzuri kutoka misheni ya chemchem tena.

Mradi wa miti pale Misheni Chemchem ulisimama, baba alianzisha kitalu jirani na mto fulani hivi mbali kidogo na Mission ya Chemchem.

Nilitumia lori fulani hivi (Leyland Albion) maarufu kama "Kaza moyo" kwenda Singida kutokea kijijini, ama mabasi ya mzee Amri Said (Blue line baadaye Yellow line), kutoka Singida hadi Itigi usafiri ulikuwa wa mabasi ya 'Relwe.'

=

Niliendelea na masomo hadi nikahitimu darasa la nane 1967...

=

Mwaka huo kabla ya kuhitimu darsa la nane babu yangu mzee Bourne alifariki, aliugua ugonjwa wa kushindwa kuhema vizuri, alikuwa mtumiaji mzuri wa "goso / gozo" (tumbaku kali inayosokotwa kama sigara)

=

Mwaka 1969 nilichaguliwa kwenda darasa la tisa (form one) shule ya sekondari Tabora. (Tabora Central School, kama ilivyojulikana wakati inaanzishwa), nilijifunza mengi hapo ikiwemo mafunzo ya awali ya kijeshi. Nilihitimu mwaka 1972.

Mwaka 1975 nilihitimu kidato cha sita shule ya sekondari Kibaha. Mwaka uliofuata nilipata kazi ya muda National Milling Corporation (NMC) na mwaka mmoja baadaye nilipata ajira ya kudumu RTC (Regional Trading Company) Dar.

=

Wakati huo wote, sikuwa uhusiano wa kimapenzi 'serious', bali mabinti wa kijijini Iramba kwa kujificha sana.

Malezi ya ki-mission, huenda yalisababisha pia. Siku moja moja sana wakati nipo Kibaha nilikuwa napotelea Mwanalugali ama maili moja kupooza nye*ge.


Baada ya kuanza kazi NMC na kisha RTC ndipo 'ukiwembe' ulipoanza. Hata sijui nilipatwa na pepo gani!
**********

Nawaza historia ya maisha yangu, nilipotoka na hadi nilipo sasa, 'fujo' zote nilizofanya kuhusiana na uhusiano na mabinti mbalimbali...

"Naona sasa inatosha..." Nilijikuta nasema kwa sauti...

...Bado nilikuwa pale Shibam kijiwe cha keram. Jioni nilienda DDC kariakoo kwenye dansi, lakini wala sikuwa na 'mzuka' wala 'sikuopoa goma' (sikutafuta binti wa kustarehe naye)

Nilitumia siku ya jumapili jioni kumtembelea mzee Katibu Kata, alikuwa akiishi somewhere "kwa Ali Maua" Mwananyamala Dsm. Madhumuni yalikuwa pamoja na kumjulia hali, lakini pia kupata ushauri wake katika mawazo yaliyonijaa kuhusiana na Hamida, mtoto wa Mzee Burhani.
^^^^^^^^^
^^^^^^^^^

Itaendelea.
IMG-20200128-WA0001.jpeg
IMG-20200128-WA0005.jpeg
IMG-20200128-WA0004.jpeg
IMG-20200128-WA0003.jpeg
IMG-20200128-WA0000.jpeg


James Jason
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom