ho chi minh
JF-Expert Member
- Sep 27, 2016
- 32,904
- 163,077
Kuna bendi nyingi zilijaribu kupiga na kuimba na kujizolea mashabiki wengi ndani na nje ya Afrika lakini bado Tp OK Jazz ilikuwa mbele tuMavatiku alipoingia OK Jazz 1975 ndo Franco alipohamia kupiga Mi Solo na Mavatiku akawa anapiga solo gitaa. Jamaa mahiri sana. bahati mbaya kuna wakati Franco aliwahisi wanampamgo wa chini kwa chini kuanzisha bendi (mavatiku na ndombe) ndo ukawa mwisho wao. ndombe alikuja kurudi baadae. Mavatiku yeye alirudi kwenye project ya Lisanga ya Banganga (Franco, Ley na Mavatiku). Na josky alitupia sana hapo mavocal. Hao niliowataja hapo ukiacha Franco wote ni baada ya Mavatiku. Usimsahau Fan Fan na Bholen huko nyuma.
Kwangu mimi TP OK Jazz haitatokea tena. Ilikuwa bendi ya aina. Leo Simaro anatimiza 80 years-probably mtunzi bora kupita wote DRC.Kuna bendi nyingi zilijaribu kupiga na kuimba na kujizolea mashabiki wengi ndani na nje ya Afrika lakini bado Tp OK Jazz ilikuwa mbele tu
Zaiko langa langa,Kwangu mimi TP OK Jazz haitatokea tena. Ilikuwa bendi ya aina. Leo Simaro anatimiza 80 years-probably mtunzi bora kupita wote DRC.
[emoji23][emoji23][emoji23]kilema cha mguu ila Franco alitafuna hvyo hivyo
Wakuu habarini za muda huu,
View attachment 717548
View attachment 717549
Zimeanzishwa thread nyingi kuhusu Franco na Mobutu, historia ya Mobutu imeelezwa na ya Franco pia, leo naleta historia ya uhusiano wa watu hawa wenye majina makubwa Africa na ulimwenguni, mwanasiasa na gwiji la muziki.
View attachment 717532
View attachment 717529
KUNYONGWA KWA KINA EVARISTE KIMBA
Mnamo mwaka 1965 Mobutu anakua rais wa Zaire na kuagiza kunyongwa kwa watu zaidi ya 6 wengi wao wakiwa mawaziri wa serikali aliyoipindua katika eneo la matonge jijini Leopold Ville (Kinshasa) kwa kosa la uhaini, mamilioni ya watu wanashuhudia hadharani, mmoja wao ni Franco, baada ya hapo Franco akatunga nyimbo iitwayo Luvumbu Ndoki (Luvumbu mchawi) hii ni hadithi ya kikongo kuhusu Mfalme Luvumbu aliyeuwa ndugu zake wa karibu kwa ajili ya kujinufaisha.
Nyimbo hii inaonekana na mamlaka kama dhihaka kwa mobutu kutokana na kitendo chake cha kunyonga mawazili wale Franco anakamatwa na kuachiwa alafu anakimbilia Brazaville kwa miezi 6 mpaka pale mambo yalipokuwa shwari.
AUNTHENTICATION POLICY (Zairenisation)
Mnamo mwaka 1971 mobutu anabadili jina la Congo kuwa Zaire, sarafu kua Zaire, pamoja na miji kuitwa majina ya kiafrika, Leopoldville inakua Kinshasa, Elizabeth Ville inakua Kisangani na kadhalika, kutokana na sera ya uafrika mpaka majina ya watu yanabadilishwa.
Bendi ya Franco, Tp Ok jazz inaandamana na mobutu nchi nzima kueneza sera ya mobutu na kutoa album iitwayo belela unthenticite na congress ya mpira.
MALIPO YA KAZI
Mobutu anampa Franco eneo la ardhi pale Kinshasa, Franco anajenga night club iliyoitwa un Deux trois, pia Mobutu baada ya kubinafsisha kampuni za kigeni anampa Franco kampuni ya muziki iitwayo mazadi.
JACKY NA HELEINE(nyimbo za Franco)
Franco añatoa nyimbo mbili Jacky na heleine ambazo serikali iliziona hazina maadili na kumpa Franco kifungo cha miezi 6 jela, na bar yake kufungwa miezi 2, alivobisha kua hazina maadili mama yake alisikilizishwa, yote haya yalifanywa na Kengo wa Dondo aliyekua attorney general.
Mobutu anamtoa jela Franco baada ya week 3 na kumshusha cheo Kengo wa Dondo kua balozi wa Zaire nchini Ubelgiji, Franco anaimba nyimbo ya kumponda Kengo iitwayo trailleur (anasema fundi nguo akikinyanganya sindano utawachomaje watu? Yaani kengo kaporwa madaraka na Mobutu)
Franco anaimba lettre a mr le directeur general (barua kwa director general) nyimbo ambayo añawaponda viongozi wa serikali kwa rushwa na usimamizi mbovu, hii inachukuliwa na wengi kama diss song kwa Mobutu.
Mwka 1984 anaimba nyimbo ya kumsifu Mobutu iliyoitwa Candida na biso, wakati wa uchaguzi ambapo watu walitakiwa kujibu ndio au apana kama wanamtaka Mobutu, hakukua na wapinzani.
Mobutu alifadhili band nyingi kubwa za muziki nchini Zaire, ikiwemo TP OK JAZZ
KIFO CHA FRANCO
Franco anafariki jijini Ubelgiji mwka 1989, Mobutu akiwa Ufaransa ziarani,
Mobutu anatangaza siku 4 za maombolezo na radio zote kupiga nyimbo za Franco tu, mwili wa Franco unapelekwa Palais du people kuagwa
View attachment 717547
Mobutu aliporudi aliitembelea familia ya Franco pamoja na kaburi.
Kwa kiasi kikubwa Mobutu alimtumia Franco katika ku mobilize watu kwenye siasa zake na pia Franco alinufaika sana kwa kuendesha magari ya kifahari kama mercedes benz na kuishi vizuri, kuliko wanamuziki wengi wa Congo na nje ya Congo
Mkuu nilikuwa nakazia kile ulichokisema kwani kuna wengine walifikira tofauti na ndo maana umekula like. Pole kama haikuja kwa maudhui hayo.Hicho ulichokieleza nimekielezea vizuri kwenye comments zangu zilizofuatia ukizipitia utaona,na hakuna mahali nimesema Tabu ley alikuwa ok jazz
Oooh Ok...do you relate to Mobutu family?The greatest musician to ever live in africa,,,and the president of the then zaire (drc)
Not at all, he is just a role modal to meOooh Ok...do you relate to Mobutu family?
Madilu System alikuwa mwanamuziki wa Afrisa International ya Tabou Ley, ilipofika safari ya kwenda ulaya akachujwa kwa mizengwe akiwa Airport. Akaona enough is enough akaomba kujiunga na OK Jazz na Franco hakuwa na hiyana. Akawa mwimbaji pamoja na waimbaji vinara wa OK Jazz- Josky, Ntessa na wengineo. Alifanya hivyo kwa miaka takribani 2/3. Ilipotokea safari ya ulaya dakika ya mwisho akapata namba. Franco wakati huo ndo amemaliza project yake ya "Lisanga ya Banganga" ambayo ilitoa santuri si chini ya 6 akiwa na Tabou Ley, Mavatiku Vissi na Josky Kiambukuta. Akiwa huko ulaya akapata idea ya wimbo wa Non au "Libala oh Libala 1982/83. Akamjaribu Madilu kama ataweza kuuimba. Baada ya kuelekezana ndo mwimbo ule ukasukwa na madilu akapiga duet na Franco na pia kuimba solo vipande vingine. Sauti ya Madilu ikapaa na OK Jazz wakaonekana wamekuja vipya-Franco akanogewa ndo akawa anatunga nyimbo za style ile (pamoja na Mamouu, Mario etc). Hapo Madilu ndipo alipopanda chati hadi kufikia 1986 Josky na Ntessa wakazira kwani waliona Franco macho yake yako kwa Madillu tu. Wakatoka OK Jazz wakatoa nyimbo kama Selengina. Ntessa alirudi kwa style ya Collaboration na OK Jazz (Album kama mbili), Josky alijiunga tena na kuongoza kikosi cha waimbaji wa OK Jazz. Baada ya kutokuelewana kati ya Familia ya Franco (Dada Yake) na Papa Simaro Lutumba 1993 Familia wakamvua Simaro uongozi, ndipo wanamuziki wote wakaiacha OK Jazz wengi wao wakianzisha Bana OK chini ya uongozi wa Simaro. Madilu akaamua kwenda solo, lakini akahakikisha mdundo wake na karibu nyimbo zake zinafuata beat ya OK Jazz na Solo ya Luambo. Alijitahidi pia akajenga bendi yake Bana Syste ambayo ukisikiliza album zake utaona role model wake ni Luambo. Si tu alitembelea nyota ya Franco bali aliishi muziki wa Odemba (style ya OK Jazz). Mwenyewe alidai kila anapoingia studio-anamuona Luambo kazini akimwongoza. Ndogo ndogo inasema mama wa Madilu ni dada wa mke wa Simaro (Maman Kelani).Asante sana mkuu kwa kumbukizi muruwa kabisa. Inaelekea Madilu ni alikuwa anatembelea sana nyota ya Franco baada ya kifo chake maana naona karibu nyimbo kadhaa za Franco kazifanyia remix. Naomba baadae utuwekee uhusiano wa hawa jamaa wawili Madilu na Franco. Na vp kuhusu Tabu ley na Mbiliabel nao walikuwa na mahusiano gani ya kimuziki na Franco.
Madilu System alikuwa mwanamuziki wa Afrisa International ya Tabou Ley, ilipofika safari ya kwenda ulaya akachujwa kwa mizengwe akiwa Airport. Akaona enough is enough akaomba kujiunga na OK Jazz na Franco hakuwa na hiyana. Akawa mwimbaji pamoja na waimbaji vinara wa OK Jazz- Josky, Ntessa na wengineo. Alifanya hivyo kwa miaka takribani 2/3. Ilipotokea safari ya ulaya dakika ya mwisho akapata namba. Franco wakati huo ndo amemaliza project yake ya "Lisanga ya Banganga" ambayo ilitoa santuri si chini ya 6 akiwa na Tabou Ley, Mavatiku Vissi na Josky Kiambukuta. Akiwa huko ulaya akapata idea ya wimbo wa Non au "Libala oh Libala 1982/83. Akamjaribu Madilu kama ataweza kuuimba. Baada ya kuelekezana ndo mwimbo ule ukasukwa na madilu akapiga duet na Franco na pia kuimba solo vipande vingine. Sauti ya Madilu ikapaa na OK Jazz wakaonekana wamekuja vipya-Franco akanogewa ndo akawa anatunga nyimbo za style ile (pamoja na Mamouu, Mario etc). Hapo Madilu ndipo alipopanda chati hadi kufikia 1986 Josky na Ntessa wakazira kwani waliona Franco macho yake yako kwa Madillu tu. Wakatoka OK Jazz wakatoa nyimbo kama Selengina. Ntessa alirudi kwa style ya Collaboration na OK Jazz (Album kama mbili), Josky alijiunga tena na kuongoza kikosi cha waimbaji wa OK Jazz. Baada ya kutokuelewana kati ya Familia ya Franco (Dada Yake) na Papa Simaro Lutumba 1993 Familia wakamvua Simaro uongozi, ndipo wanamuziki wote wakaiacha OK Jazz wengi wao wakianzisha Bana OK chini ya uongozi wa Simaro. Madilu akaamua kwenda solo, lakini akahakikisha mdundo wake na karibu nyimbo zake zinafuata beat ya OK Jazz na Solo ya Luambo. Alijitahidi pia akajenga bendi yake Bana Syste ambayo ukisikiliza album zake utaona role model wake ni Luambo. Si tu alitembelea nyota ya Franco bali aliishi muziki wa Odemba (style ya OK Jazz). Mwenyewe alidai kila anapoingia studio-anamuona Luambo kazini akimwongoza. Ndogo ndogo inasema mama wa Madilu ni dada wa mke wa Simaro (Maman Kelani).
madiluu kafundshwa mzk na luambo makiadi,na walikuwa pmj ktk band ya okk jazz hadi akifariki madilu akachukua usukaniAsante sana mkuu kwa kumbukizi muruwa kabisa. Inaelekea Madilu ni alikuwa anatembelea sana nyota ya Franco baada ya kifo chake maana naona karibu nyimbo kadhaa za Franco kazifanyia remix. Naomba baadae utuwekee uhusiano wa hawa jamaa wawili Madilu na Franco. Na vp kuhusu Tabu ley na Mbiliabel nao walikuwa na mahusiano gani ya kimuziki na Franco.
mkuu ID yako imenikumbusha mwanamzk wa okk jazz alieitwa simaro lutumba masiyaMkuu nilikuwa nakazia kile ulichokisema kwani kuna wengine walifikira tofauti na ndo maana umekula like. Pole kama haikuja kwa maudhui hayo.
ukweli mtupuKuna ndugu yangu mmoja alikuwa anapenda kujiita Franco Luambo Makiadi. Wakati huo nikiwa bado mdogo nikienda kumtembelea nilifurahia sana vituko vyake,alikuwa anajisahau na hata kujitambulisha kwa jina hilo alipotakiwa.
Alifanana tabia na Franco kwa kila kitu.
Enzi hizo kulikuwa na furaha za kweli. Nimemiss sana nyakati hizo
umechambua vizur kwel hongeraMadilu System alikuwa mwanamuziki wa Afrisa International ya Tabou Ley, ilipofika safari ya kwenda ulaya akachujwa kwa mizengwe akiwa Airport. Akaona enough is enough akaomba kujiunga na OK Jazz na Franco hakuwa na hiyana. Akawa mwimbaji pamoja na waimbaji vinara wa OK Jazz- Josky, Ntessa na wengineo. Alifanya hivyo kwa miaka takribani 2/3. Ilipotokea safari ya ulaya dakika ya mwisho akapata namba. Franco wakati huo ndo amemaliza project yake ya "Lisanga ya Banganga" ambayo ilitoa santuri si chini ya 6 akiwa na Tabou Ley, Mavatiku Vissi na Josky Kiambukuta. Akiwa huko ulaya akapata idea ya wimbo wa Non au "Libala oh Libala 1982/83. Akamjaribu Madilu kama ataweza kuuimba. Baada ya kuelekezana ndo mwimbo ule ukasukwa na madilu akapiga duet na Franco na pia kuimba solo vipande vingine. Sauti ya Madilu ikapaa na OK Jazz wakaonekana wamekuja vipya-Franco akanogewa ndo akawa anatunga nyimbo za style ile (pamoja na Mamouu, Mario etc). Hapo Madilu ndipo alipopanda chati hadi kufikia 1986 Josky na Ntessa wakazira kwani waliona Franco macho yake yako kwa Madillu tu. Wakatoka OK Jazz wakatoa nyimbo kama Selengina. Ntessa alirudi kwa style ya Collaboration na OK Jazz (Album kama mbili), Josky alijiunga tena na kuongoza kikosi cha waimbaji wa OK Jazz. Baada ya kutokuelewana kati ya Familia ya Franco (Dada Yake) na Papa Simaro Lutumba 1993 Familia wakamvua Simaro uongozi, ndipo wanamuziki wote wakaiacha OK Jazz wengi wao wakianzisha Bana OK chini ya uongozi wa Simaro. Madilu akaamua kwenda solo, lakini akahakikisha mdundo wake na karibu nyimbo zake zinafuata beat ya OK Jazz na Solo ya Luambo. Alijitahidi pia akajenga bendi yake Bana Syste ambayo ukisikiliza album zake utaona role model wake ni Luambo. Si tu alitembelea nyota ya Franco bali aliishi muziki wa Odemba (style ya OK Jazz). Mwenyewe alidai kila anapoingia studio-anamuona Luambo kazini akimwongoza. Ndogo ndogo inasema mama wa Madilu ni dada wa mke wa Simaro (Maman Kelani).
afadhali umenisaidia kumjibukama hukuwahi kupenda Mziki wa Franco basi hujawahi penda muziki kabisa ndugu yangu
catch youWikipedia uisome na macho matatu, inamapungufu ya kutosha kuhusu hawa wanamuziki.
ktk cm yangu hapa Nina nyimbo 500 HIV za Franco kila cku lazma nisikilizSawa mkuu tuachie sisi tufurahie vitu adimu na midundo adimu. Franco was a genious hana mfano.