Uhuru wa kuabudu nao umeanza kuondoka...(?)

Baija Bolobi

JF-Expert Member
Feb 25, 2009
1,093
1,726
Tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, uhuru na sura zake mbalimbali, umepungua au kwisha kabisa. Ilianza na kuondoa uhuru wa kukutana/kukusanyika - wananchi wakavumilia.

Ikafuata uhuru wa kujieleza. Siku hizi polisi wetu ni rahisi kumkamata mtu aliyetoa maoni yake mtandaoni kuliko kumkamata mwizi au jambazi anayevamia benki. Kila kukicha ni kukimbizana na vijana wanaotoa mawazo yao mitandaoni. Hili nalo likavumilika.

Uhuru wa kupata habari nao ukasombwa na sheria mpya. Waziri wa habari siku hizi anaweza kufungia gazeti, redio, TV mpaka blogu. Waziri asiye na bajeti ya kusomesha waandishi wa habari, ana bajeti ya kununua pingu za kuwafunga wanapotoa mawazo yao. Anafungia gazeti kwa kusema uwongo; baada ya wiki, serikali inamtumbua mtu aliyetajwa katika habari iliyofungia gazeti hilo!

Sasa uhuru wa kuabudu nao umeingiliwa. Spika wa bunge ana mamlaka mpaka misikitini na makanisani. Nguvu ya spika kuamuru kukamatwa kwa mbunge aliyeonekana kanisani akiabudu imetokea katiba gani? Nguvu ya polisi kuzuia wanaotaka kukutana na kufanya sala/dua imetokea katiba gani? Ibada na imani ni mambo binafsi ya watu. Wako wanaoabudu "mungu" wao aitwaye Ndugai lakini wapo wenye shetani wao aitwaye "bashite". Wote hawa wana uhuru usiopaswa kuingiliwa kwa sababu ni imani.

Tutaanza kupata wakimbizi wanaokimbia nchi.
 
Yalianza hivi hivi nchi nyingi
Watu waliteswa wakapigwa wakanyimwa haki wakawekwa tabaka la pili sasa imekua too much yaani hapa kwetu mpaka na maombi mnazuia
Leo nimeshuhudia na macho yangu pale kinondoni ufipa watu wakipigwa virungu na kuingizwa kwenye magari ya polisi kwa nguvu kisa tu walivaa tshert za pray for lissu
Hii ni haki kweli? Hii ni ya kitimamu?
Haya wanafafanya watanzania?
Mikutano mmezuia, mnateka, maandamano mnazuia, hamjaridhika mnawaandama viongozi wa upinzani, mmeanza sasa kuwakamata wanachama na wananchi wanaounga mkono upinzani

Mnajenga uadui mkubwa sana ambao hamtoweza kuuondoa
Ndo maana imefika mahali hata serikali ikipata jambo baya au janga raia wanashangilia maana tayari mnaendeleza uonevu na dhulma
Dhulma ina mwisho wake na nawaambia huu uadui na huu ukandamizaji unaofanya na utawala wa awamu ya tano ni sawa na bomu linaloundwa na litalipuka soon
Raia wakichoka watafanya yao naomba tusije kuja kulaumiana baadae yakishatokea
Mnatengeneza uasi ambao soon utalighalimu taifa zima na utawala wa ccm
Tukichoka tutaliamsha dude
 
Tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, uhuru na sura zake mbalimbali, umepungua au kwisha kabisa. Ilianza na kuondoa uhuru wa kukutana/kukusanyika - wananchi wakavumilia.

Ikafuata uhuru wa kujieleza. Siku hizi polisi wetu ni rahisi kumkamata mtu aliyetoa maoni yake mtandaoni kuliko kumkamata mwizi au jambazi anayevamia benki. Kila kukicha ni kukimbizana na vijana wanaotoa mawazo yao mitandaoni. Hili nalo likavumilika.

Uhuru wa kupata habari nao ukasombwa na sheria mpya. Waziri wa habari siku hizi anaweza kufungia gazeti, redio, TV mpaka blogu. Waziri asiye na bajeti ya kusomesha waandishi wa habari, ana bajeti ya kununua pingu za kuwafunga wanapotoa mawazo yao. Anafungia gazeti kwa kusema uwongo; baada ya wiki, serikali inamtumbua mtu aliyetajwa katika habari iliyofungia gazeti hilo!

Sasa uhuru wa kuabudu nao umeingiliwa. Spika wa bunge ana mamlaka mpaka misikitini na makanisani. Nguvu ya spika kuamuru kukamatwa kwa mbunge aliyeonekana kanisani akiabudu imetokea katiba gani? Nguvu ya polisi kuzuia wanaotaka kukutana na kufanya sala/dua imetokea katiba gani? Ibada na imani ni mambo binafsi ya watu. Wako wanaoabudu "mungu" wao aitwaye Ndugai lakini wapo wenye shetani wao aitwaye "bashite". Wote hawa wana uhuru usiopaswa kuingiliwa kwa sababu ni imani.

Tutaanza kupata wakimbizi wanaokimbia nchi.
Tatizo swala la lissu linataka kugeuzwa mtaji kwa chadema bora wazuiwe tuu maana kama ibada zikafanyike kwenye nyumba za ibada makanisa na misikiti ipo acheni uhuni uhuni.
 
Malalamiko ya Uhuru wa kuabudu yanalalamikiwa kwenye JF tena jukwaa la siasa.

Hizi siasa hizi!!!!!
 
Kuna watu wanaabudu Ng'ombe lkn hawajakatazwa, kwani hapa tatizo nini hasa. Kumuombea Lisu kunaipa serikali tabu gani?
 
Tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, uhuru na sura zake mbalimbali, umepungua au kwisha kabisa. Ilianza na kuondoa uhuru wa kukutana/kukusanyika - wananchi wakavumilia.

Ikafuata uhuru wa kujieleza. Siku hizi polisi wetu ni rahisi kumkamata mtu aliyetoa maoni yake mtandaoni kuliko kumkamata mwizi au jambazi anayevamia benki. Kila kukicha ni kukimbizana na vijana wanaotoa mawazo yao mitandaoni. Hili nalo likavumilika.

Uhuru wa kupata habari nao ukasombwa na sheria mpya. Waziri wa habari siku hizi anaweza kufungia gazeti, redio, TV mpaka blogu. Waziri asiye na bajeti ya kusomesha waandishi wa habari, ana bajeti ya kununua pingu za kuwafunga wanapotoa mawazo yao. Anafungia gazeti kwa kusema uwongo; baada ya wiki, serikali inamtumbua mtu aliyetajwa katika habari iliyofungia gazeti hilo!

Sasa uhuru wa kuabudu nao umeingiliwa. Spika wa bunge ana mamlaka mpaka misikitini na makanisani. Nguvu ya spika kuamuru kukamatwa kwa mbunge aliyeonekana kanisani akiabudu imetokea katiba gani? Nguvu ya polisi kuzuia wanaotaka kukutana na kufanya sala/dua imetokea katiba gani? Ibada na imani ni mambo binafsi ya watu. Wako wanaoabudu "mungu" wao aitwaye Ndugai lakini wapo wenye shetani wao aitwaye "bashite". Wote hawa wana uhuru usiopaswa kuingiliwa kwa sababu ni imani.

Tutaanza kupata wakimbizi wanaokimbia nchi.
eti bavicha wanafanya maombi!! eti wamenyimwa uhuru wa kuabudu!!! mi nacheka saaaaana!! na hizi siasa uchwara. hivi ni lini bavicha imegeuka kuwa zehebu!? hadi kufikia kunyimwa uhuru wa kuabudu!!?. hahahahahaa huu ujanjaujanja haujawahi kuicha salama hii bavicha
 
Siyo kazi ya chama cha siasa kuandaa ibada, nadhani hapa tunachanganya siasa na dini. Viongozi wa dini ndiyo hasa walitakiwa kuandaa mkutano wa maombi siyo Chadema, maana Chadema imesajiliwa kueneza siasa.

Jambo la maombi kwa ajili ya Tundu Lissu ni jambo jema, lakini isitumike vibaya, ingekuwa vema tukaacha haya malumbano yasiyo na tija tukamuacha Mh. Lissu apone kabisa na arejee kulijenga Taifa kuliko kila siku kusuguana kwa ajili yake.
 
Tatizo swala la lissu linataka kugeuzwa mtaji kwa chadema bora wazuiwe tuu maana kama ibada zikafanyike kwenye nyumba za ibada makanisa na misikiti ipo acheni uhuni uhuni.

Itakapotokea
1. Upande wa wa pili wanataka kuomba itakuwaje?

2. Ipo siku serikali itawataka watu wajitolee damu....je itakuwaje?
 
Siyo kazi ya chama cha siasa kuandaa ibada, nadhani hapa tunachanganya siasa na dini. Viongozi wa dini ndiyo hasa walitakiwa kuandaa mkutano wa maombi siyo Chadema, maana Chadema imesajiliwa kueneza siasa.

Jambo la maombi kwa ajili ya Tundu Lissu ni jambo jema, lakini isitumike vibaya, ingekuwa vema tukaacha haya malumbano yasiyo na tija tukamuacha Mh. Lissu apone kabisa na arejee kulijenga Taifa kuliko kila siku kusuguana kwa ajili yake.

Spika anapofunguwa bunge kwa sala kila siku nikiongozi wa dinigani?

Anapoliongoza bunge kumuombea maisha marefu rais anafanya kama kiongozi wa dinigani?
 
Back
Top Bottom