Uhuru ni kitu gani kwa mwanamke?

Uhuru ni kitu gani kwa mwanamke?

hahahahahahahah eti kama kalio umenishindwa we mwanamke hahah nmecheka sana ila kweli ila jamn mi napenda saana kufatiliwa ila wa kunifatilia ndo sina hana hata huo mda mpka itokee akuulize ni ya kuhesabu
Naanza kukufuatilia
 
Ndoa ni makubaliano na sio mmoja kudhani anamamlaka zaidi ya mwingine. inakubalika familia kuwa na kiongozi kwa maana ya baba anaweza kuwa kiongozi wa familia.

lakini kuwa kiongozi huku hakuna maana ya kwamba mwanaume akachepuke lakini mwanamke haruhusiwi kuchepuka na akikamatwa ni kosa kubwa sana.

kama nilivyosema kuwa ndoa ni makubaliano, yawezekana hata wewe hukupanga kuchepuka lakini ghafla unakutana na mtu anateka hisia zako na unajikuta umemsaliti ingawa hukupanga kabla kuwa nataka kumsaliti. kama hayo yanatokea kwa wanaume basi ijulikane hata kwa wanawake yanawatokea.

hivyo kama unataka kumfuatilia mwananmke kwa kigezo cha hali kuwa mbaya basi ukubali na wewe akufuatilie. kama unataka kukagua simu yake basi uwe tayari na wewe kukaguliwa simu yako na huo ndio uhuru. mnakubaliana ni utaratibu gani mtumie.

mkiamua kufunga mikanda ni nyote na sio wewe kudhani unaweza kufanya lolote hakuna shida ila yeye unampangia cha kufanya.

Habari wana jf,

Kwa mara kadhaa huwa nmeskia kwamba ni vizuri kumpa uhuru mpenzi wako hasa wa kike kwa maana tupunguze kuwafuatilia,tuwe majentromeni maana kum trace ni kuonyesha udhaifu na wivu na upungufu wa kumuamini eti.

Kwa mantiki hii unakuta mtu huyo huyo atakaepewa uhuru baada ya muda anaweza kuanza kukuchezea rafu na dharau juu sasa huwa inatatiza sana, labda tueleweshane huu uhuru unaotakiwa tuwape ni kwamba mnastahili au tuendelee kuwafwatilia nyendo zenu mda wote ukizingatia majanga ni mengi siku hizi!
 
Hakuna kitu napenda kama kufuatiliwa ila isizidi, yaani najisikia burudaniii, sio mtu unamuaga usiku natoka out, uwiii anajibu tu "okey"!! Uwiii yaani nakuwa sikuagi tenaaa na usiniulize.
 
do kufuatiliwa kwa kiasi lakini si unifuatilie kila saa upo wapi? unaongea na nani? aiii inachosha ukiona vipi vipi ndiyo uniulize lakin si kila saa upo nyuma nyuma kama kalio loh
Mchaga katika Ubora Wako
 
Unanifuatilia nimekuwa mfugo wako. Ebo. Hatuhitaji kupewa uhuru bali tunao by default. Utakuja mwanaume wa aina hii anataka ufanye kazi ( uajiriwe au ujiajiri) sababu kukuhudumia hawezi. Hapohapo ndo analeta isuz hizi. Natupa kule. Upuuzi siendekezi. Ukitaka uwe na uwezo wakuwa na mamlaka ya kuamua kunipa ruhusa au la hakikisha unahudumia full na ipasavyo. Vinginevyo mtasoma namba
 
Habari wana jf,

Kwa mara kadhaa huwa nmeskia kwamba ni vizuri kumpa uhuru mpenzi wako hasa wa kike kwa maana tupunguze kuwafuatilia,tuwe majentromeni maana kum trace ni kuonyesha udhaifu na wivu na upungufu wa kumuamini eti.


Uhuru kwa mwanamke unakuja kwa namna mbili. Namna ya kwanza ni pale mwanamke anakuwa na uhuru wa kufanya mambo yake pa si kuingiliwa, kufwatiliwa au kuwa limited. Mfano,kama ni biashara, unampatia uhuru wa kufanya atakavyo.
Uhuru wa pili ni katika mahusiano. Ikumbukwe kuwa WIVU ni sehemu ya mapenzi. Kama huna wivu na mpenzi wako basi humpendi. Lakini wivu huu ukizidi sana ni kero. Ukimpatia uhuru mpenzi wako kufanya maamuzi katika mahusiano ndio uaminifu unashamiri. Mfano, ukimwamini mpenzi wako kiasi kwamba hata ukipata simu yake huwezi kuichokora ndani kuangalia out/in calls ama ujumbe basi unamwamini. Lakini kila jambo comes with a price, siwezi kumwamini mtu ambaye haniamini. I mean trust is a two way traffic. E&O.E
 
  • Thanks
Reactions: DLS
Kila ki2 na wakati wake huwezi fuatilia mtu anaefikiri kama wewe
Afanye yote nicpate ushahidi hapo atakuwa ameshinda akishindwa yeye bac nitakuwa nimeshinda mimi
 
Back
Top Bottom