Uharibifu wa mazingira mto Ndumbwi unapoingia baharini

Bulesi

Platinum Member
May 14, 2008
14,211
13,725
Mto Ndumbwi huingia Bahari ya Hindi sehemu za Mbezi Beach. Mto huu una mikoko mingi sehemu hiyo na kama inavyofahamika miti hii ndio mazalia ya samaki hivyo ni muhimu kuhifadhiwa. Huko nyuma kama miaka miwili iliyopita marehemu mama Lwakatare[ R.I.P] alijenga nyumba yake ya kifahali pembeni ya mto huo na sio mbali na ufukwe wa bahari.

Kitendo hicho cha ujenzi ule kulileta malalamiko mengi kwa wana mazingira kwani kilikuwa kinakiuka sheria inayolinda fukwe za bahari. lakini hata hivyo marehemu hakulazimishwa kuvunja jumba lake kama sheria inavyosema kwa kuwa tu alikuwa Mbunge na hivyo kutumia influence yake.

Kwa bahati mbaya sana hapo hapo karibu na nyumba ya marehemu kuna sehemu ya wazi ambayo mara nyingi wavamizi wa viwanja wamejaribu kujenga nyumba sambamba kabisa na mto; huko nyuma juhudi zao zilishindwa kwani Manispaa ya Kinondoni ilikuwa inabomoa majengo na kuta zilizokuwwa zinasimamishwa kinyume na sheria.

Kitu cha kushangaza hivi sasa kuna mtu anazungusha ukuta na kuanza kujenga kwenye hiyo open space ambayo huko nyuma ilikatazwa kwa sababu za kulinda mikoko na mazingira ya sehemu mto unapoingia baharini! Nadhani kwavile bunge li karibu kuvunjwa wavamizi hawa wa viwanja na wafanyakazi wa Manispaa ya Kinondoni wasio waaminifu, wanataka kutumia mwanya huo wakidhania kuwa hakutakuwa na viongozi wa serikali watakaokuwa makini na ulinzi wa mazingira ya mto sehemu hii.

Ningewasihi wahusika katika wizara ya mazingira kufanya haraka na kutembelea sehemu hii na kuona uharibifu unaofanywa na watu wasiojali athari wanazozifanya kwa jamii. Ni muhimu kusimamisha ujenzi unaoendelea mapema iwezekanavyo na pia kuvunja kuta za nyumba zilizojengwa karibu na ukingo wa mto. Nategemea Mheshimiwa Azzan Zungu waziri mwenye dhamana ya mazingira atapata taarifa ya malalamiko haya na kuchuka hatua kabla ya Bunge kuvunjwa.
 
Ushauri mzuri huu

Sasa ninaamini kuwa serikali yetu ni sikivu na pia watendaji wake wanapitia mitandao ya Jamii na kuyafanyia kazi malalamiko yanayotolewa na wananchi hasa humu Jamii forum! Juzi kulikuwa na uzi juu ya uhalibifu wa mazingira ya mto Ndumbwi kwa wavamizi kuzungusha ukuta kwenye open space ambayo iko ukingoni kabisa mwa mto; leo Katika pita pita zangu nimeona ukuta ule uliojengwa umepigwa "X" na maandishi yanayo someka BOMOA HARAKA. Hata hivyo inaelekea kulikuwa na jitihada za kufuta stop order hiyo kwani mafundi walionekana kuchapia cement ili maandishi yasionekane.

Inaelekea hawa wavamizi ni watu wanaojiweza kifedha hivyo wanaweza kukaidi amri hiyo ya kusitisha ujenzi wa uzio; kimsingi NEMC au Manispaa ya Kinondoni wana kila sababu ya kumpiga faini huyo anayejenga , na kuvunja ule uzio na kuhakikisha mvamizi huyo analipa gharama zote za uvunjaji!! Hilo litakuwa fundisho tosha kwa wavunjaji sheria za mazingira.
 
Sasa ninaamini kuwa serikali yetu ni sikivu na pia watendaji wake wanapitia mitandao ya Jamii na kuyafanyia kazi malalamiko yanayotolewa na wananchi hasa humu Jamii forum! Juzi kulikuwa na uzi juu ya uhalibifu wa mazingira ya mto Ndumbwi kwa wavamizi kuzungusha ukuta kwenye open space ambayo iko ukingoni kabisa mwa mto; leo Katika pita pita zangu nimeona ukuta ule uliojengwa umepigwa "X" na maandishi yanayo someka BOMOA HARAKA. Hata hivyo inaelekea kulikuwa na jitihada za kufuta stop order hiyo kwani mafundi walionekana kuchapia cement ili maandishi yasionekane.

Inaelekea hawa wavamizi ni watu wanaojiweza kifedha hivyo wanaweza kukaidi amri hiyo ya kusitisha ujenzi wa uzio; kimsingi NEMC au Manispaa ya Kinondoni wana kila sababu ya kumpiga faini huyo anayejenga , na kuvunja ule uzio na kuhakikisha mvamizi huyo analipa gharama zote za uvunjaji!! Hilo litakuwa fundisho tosha kwa wavunjaji sheria za mazingira.

Namkumbuka naibu waziri wa Wizara ya Mazingira aliyepita (Mh. Luhaga Mpina; kwa sasa waziri wa mifugo) alikua hana mswalia mtume katika kutoza faini kwa waharibifu na wachafuzi wa mazingira.

Mikoko inalindwa sana kwa sababu ni muhimu sana kwa viumbe_bahari (samaki wakiwemo) kama ulivyotaja hapo juu...

Nitashangaa na kusikitika sana mimi kama mdau wa elimu_bahari endapo wavamizi wataendelea kupimana ubavu na mamlaka ilhali wanavunja sheria tulizojiwekea waziwazi na kuharibu ustawi wa ikolojia ya bahari.

Naamini humu kuna watu wa TFS (wakala wa huduma za misitu), NEMC (Baraza la taifa la hifadhi ya mazingira), Tanzania marine parks (Mamlaka ya hifadhi za bahari) na wengineo wanaohusika wanaona humu.

Asante sana mwanzisha uzi kwa kupaza sauti.
 
Kulikua na jamaa kwny ofisi za Mazingira silikumbuki jina lake vizuri ila alikua ana jina kama la watu wa Musoma sijui ni Segito sikumbuki fresh jamaa alikua anaendesha hizo operation za kusimamia watu wanaojenga kwny vyanzo vya maji aisee alikua ni mtata balaa,hakuna cha mswalia mtume mara ya mwisho kama nakumbuka vizuri aliwekwa benchi akapewa na kesi juu.
 
Serikali imelala, inawaza kumsulubu @MBOWE

Nadhani hawa wavamizi wanaamini kwamba serikali imelala kwani kasi wanayotumia kujenga uzio kuzunguka ile open space sio ya kawaida. Uvamizi huu bila ya shaka una mkono wa diwani wa Kawe ambae ni mtoto wa kiume wa marehemu mama Rwakatare kwani haingii akilini kuwa huyu diwani ambae anaishi kwenye nyumba jirani na hiyo open space asijue kile kinachoendelea mbele ya nyumba yao.
Serikali haina budi kumuuliza diwani huyo nani anahusika na ujenzi huo na akipatikana apewe adhabu ya mfano ikiwa ni pamoja na kuubomoa huo uzio uliojengwa kinyume na sheria. Kama huyu diwani angekuwa muadilifu bila ya shaka ujenzi huu wala usingeanza!! Manispaa ya Kinondoni wakisaidiwa na wizara ya mazingira ni lazima wachukue hatua za haraka kuzuia uharibifu unaofanywa kwenye lile eneo.
 
Nadhani hawa wavamizi wanaamini kwamba serikali imelala kwani kasi wanayotumia kujenga uzio kuzunguka ile open space sio ya kawaida. Uvamizi huu bila ya shaka una mkono wa diwani wa Kawe ambae ni mtoto wa kiume wa marehemu mama Rwakatare kwani haingii akilini kuwa huyu diwani ambae anaishi kwenye nyumba jirani na hiyo open space asijue kile kinachoendelea mbele ya nyumba yao.
Serikali haina budi kumuuliza diwani huyo nani anahusika na ujenzi huo na akipatikana apewe adhabu ya mfano ikiwa ni pamoja na kuubomoa huo uzio uliojengwa kinyume na sheria. Kama huyu diwani angekuwa muadilifu bila ya shaka ujenzi huu wala usingeanza!! Manispaa ya Kinondoni wakisaidiwa na wizara ya mazingira ni lazima wachukue hatua za haraka kuzuia uharibifu unaofanywa kwenye lile eneo.
Serikali ya kiboya sana hii, yaani diwani tu kawaweka mfukoni NEMC na wizara nzima, shenzi taipusi pwayipwayi
 
Mawaziri wawili Azzan Zungu wa mazingira na William Lukuvi wa Ardhi are accountable kwa uharibifu unaotokea kule mto Ndumbwi unapoingia baharini [ Mbezi Beach] bila kuchukua hatua. Magufuli anahitaji watu wanaomsaidia kazi kuendesha nchi kufuatana na sheria, hivyo fanyeni kazi zenu msimgoje mpaka yeye aje ndio muanze kushuhurika!!
 
Leo nimeona kwenye gazette la Nipashe naibu Waziri wa mazingira na Muungano ameamuru kuwa NEMC iwaadabishe wale wote waliojenga kinyume na sheria pale Salander bridge!! Hilo agizo kwa NEMC ni lazima liwe kwa wale wote nchi nzima waliokiuka sheria ya mazingira; wakiwemo wale waliojenga Mbezi beach pale mto Ndumbwi unapoingia Bahari ya Hindi!!! Kuhamia Dodoma hakuna maana kuwa serikali haipo tena Dar es salaam.!!!
 
Leo nimeona kwenye gazette la Nipashe naibu Waziri wa mazingira na Muungano ameamuru kuwa NEMC iwaadabishe wale wote waliojenga kinyume na sheria pale Salander bridge!! Hilo agizo kwa NEMC ni lazima liwe kwa wale wote nchi nzima waliokiuka sheria ya mazingira; wakiwemo wale waliojenga Mbezi beach pale mto Ndumbwi unapoingia Bahari ya Hindi!!! Kuhamia Dodoma hakuna maana kuwa serikali haipo tena Dar es salaam.!!!
Haguswi mtu pale
SIASA tu hizo

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Mawaziri wawili Azzan Zungu wa mazingira na William Lukuvi wa Ardhi are accountable kwa uharibifu unaotokea kule mto Ndumbwi unapoingia baharini [ Mbezi Beach] bila kuchukua hatua. Magufuli anahitaji watu wanaomsaidia kazi kuendesha nchi kufuatana na sheria, hivyo fanyeni kazi zenu msimgoje mpaka yeye aje ndio muanze kushuhurika!!
Nchi hii mambo yanafanyikaga kwa mupe muruke

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Nchi hii mambo yanafanyikaga kwa mupe muruke

Hapana kwa hili la uharibifu wa mto Ndumbwi kilio chetu kama vile kimesikika kwani ujenzi uliokuwa unakwenda kasi sana umesimama ; sasa sijui kama wamepewa stop order au vipi!! Lakini jambo la msingi ni wahusika kuwaadabisha wote waliohusika kuanzia kutoa vibari vya kujenga mpaka wenyewe walioomba na kujenga hizo kuta. Ili kuwakomesha hawa wavamizi hizo kuta zote zibomolewe na hilo litakuwa fundisho kwa wengine!!
 
Waziri mpya wa mazingila dada Ummy itabidi amkokote Lukuvi waende wakaone uharibifu uliofanyika na wapimaji viwanja kwenye maangilio ya mto Ndunbwi baharini; msingoje mpaka wananchi wakaenda kuwachongea kwa Mkuu, kwani uharibufu unaofanyika pale ni hasara kubwa kwa Taifa.
 
Weka location tupajueni wapi hasa

Sehemu mto Ndumbwi unaingia Bahari ya Hindi ni sehemu ya Mbezi Beach ; sambamba kabisa na nyumba ya Marehemu mama Lwakatare. Cha kushangaza naambiwa mtoto wake anaeishi kwenye nyumba hiyo na ni diwani wa Kawe; anahusika kwa kificho na ufisadi unaotendeka hapo !!
 
Back
Top Bottom