Ni kweli rushwa ipo sana, nilishuhudia mama mmoja tarehe 12 February akihitaji passport ya kwenda matibabu nje alizungushwa sana mara aambiwe apeleke vielelezo mara vitambulisho, tukamshauri aombe kuonana na Mkurugenzi wa Uhamiaji, baada ya wale wahudumu kugundua kuwa yule mama yupo kwenye hiyo process ya kwenda kwa Mkurugenzi, wakampa pass in less than one hour kitu kilichoashiria kuwa walikuwa wameprint tayari isipokuwa hawakutaka kumpa, mwingine alikuwa anasafiriri kwenda Nordic countries, tena huyu alikuwa anarenew naye wakamwambia ataiapta kesho yake, alipokwenda kwa boss wao akaambiwa asubiri passport apewe siku hiyohoyo na akapewa.
Mchezo wa rushwa unachezwa na wale maofisa waliopo kwenye yale madirisha siyo viongozi, nilichojifunza ni kuwa ukipata nafasi ya kuonana na viongozi ukawaambia shida yako wakakuelewa basi hutoi hata senti moja