Uhalisia wa filamu za kizungu

Uhalisia wa filamu za kizungu

Mapondo Mapoka

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2015
Posts
274
Reaction score
135
Moja ya vitu navyokua najiuliza bila majibu ni
pale napoangalia filamu za wenzetu mataifa tajiri/
duniani. Utaona wanatumia vitu vya thaman sana
kuigizia na wanaviharibu haribu mfano utakuta
vitu kama ndege za kivita na gari za kivita
zinaharibiwa na zaidi utaona watu wanavyokufa
kwa kwa vifaa vya kijeshi na mambo mengine
mengi. Je hua kunauhalisia wote hata kidogo
japo nikwel wenzetu wameendelea sana
kiteknolojia? Mwenye uelewa juu ya hilo naomba
anijuz
 
Matangazo ya kibiashara at the same time wanatoa uhondo wa picha kwa watakao tazama as uhalisia ndo watakiwa zaidi.
 
Natamani nikuelezee ila natumia simu ila niwape ushauri tu jaribu kwenda kununua movie original (mara nyingi zinakuwa na behind the scene ) inaonyesha jinsi picha ilivyotengenezwa,jinsi ulivyodanganywa na mengi tu utayajua wanaoweza wanaweza kukuelezeeni inavyokua
 
Baadhi ya vitu hua ni kweli vinatumika na kuharibiwa, niliwahi kuona behind the scene ya LOST ni kua walitumia ndege ndogo na kuikata katikati, kwenye movie utaona hiyo ndege ilianguka kwenye kisiwa huko kusikoishi watu, kwaio kuna baadhi ya vitu wanatumia kweli.
 
wenzetu kwasababu ya maendeleo ya kiteknolojia na uchumi mzuri naweza amini kua baadhi ya mambo ni kweli.
 
Ndiyo maana utasikia movie hii imetumia dola milioni nyingi,we unadhani kwanini?
 
Mengine huwa ni kweli kama movies za Jackie Chan na Tony Jaa some stunts huwa ni kweli bila kupindisha
 
Inategemea unasongelea ukweli upi

Nadhani aliekushauri uende youtube atakuwa kakupa wazo zuri sana

Nenda youtube na search jina la move unayoitaka na uongezee na behind the scene

Kifupi ni kwamba matukio mengi yakufikirika au ya hatari au yakuharibu vitu vya thamani sana huwa sio yakweli, yanakua edited

Hivi kwaakili ya kawaida kabisa unadhani movie kama Godzila, 2015 nk yale magotofa yanayoanguka na kulipuka na ule umati wa watu wanaokufa na mamilipuko ni kweli

maranyingi kazi zile hufanywa kwenye studio maalumu kisha software zinamalizia
 
Mengine huwa ni kweli kama movies za Jackie Chan na Tony Jaa some stunts huwa ni kweli bila kupindisha

Kwa vitu vidogo vidogo mfano kuruka umbali mdogo nk anaweza kufanya mwenyewe lakini usalama wa mwigizaji ni jambo kubwa sana

Sio hao tu wanaofanya waigizaji wote wanafanya mambo mengine kiukweli lakini yakufikirika na magumu teknolojia itafanya kazi yake
 
Back
Top Bottom