jojipoji koromije
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 1,127
- 1,634
Naombeni kujua mwenye ufahamu atufahamishe inakuwaje hawa mawaziri wa Rais Samia mpaka sasa wako Ofisini wakati Bunge limeshavunjwa. Inavyoeleweka kikatiba Waziri hutokana na Mbunge, Mbunge anapo poteza haki ya kuwa Mbunge automatically anapoteza hadhi ya kuwa Waziri. Na iko wazi ki Katiba tunapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu Rais atavunja Bunge na Baraza la Mawaziri, na Wizara zitakuwa chini ya Watendaji Wakuu wa Wizara husika ambao kimfumo tulionao ni Makatibu Wakuu wa Wizara mpaka baada ya Uchaguzi Mkuu ambapo Rais aliyseshinda atateua baraza lake la Mawaziri kutoka miongoni wa wabunge wake walioshinda Uchaguzi au atakaowateua. Sasa Mawaziri hawa wa sasa hivi kila siku wako ofisini na barabarani na wakitoa maelekezo kila siku wakati kisheria hawana haki hizo. Nashawika kuwa na mashaka na hawa Mawaziri wasije wakafanya mambo yasiyokuwa na maslahi kwa Nchi ikiwemo kuingia mikataba isiyo na maslahi kwa Nchi na utakapompeleka Mahakamani watashinda kwani wanaweza kabisa kusema yeye hakuwa Waziri. Ni sheria ikampa ushindi. Awamu Hii tunashuhudia uvunjwaji wa sheria na kanuni ambazo ni za hatari sana. Aliye karibu na Mama amwambie hao watu wapishe ofisi za Umma; Makatibu Wakuu waendelee na Majukumu yao. Over