Uhakiki wa umri ufanywe, wafanyakazi wengi wamedanganya umri

kkarumekenge

JF-Expert Member
Aug 14, 2013
1,708
1,026
Upo ukweli kwamba kuna wafanyakazi wengi wa serikali wana kumbukumbu za uongo juu ya umri wao, wamedanganya wakionyesha umri wao ni mdogo ili wachelewe kustaafu.

Lakini tunasahau kwamba kwa kufanya hivyo wazee hao huziba nafasi za wahitimu kutoka vyuo mbalimbali nchini na inawezekana tatizo la ajira rasmi nchini linaweza likawa sivyo lilivyo sasa.

Wahitimu hawa wapya watapataje ajira huku nafasi zinaendelea kushikiliwa na wanaopaswa kustaafu, wengine hata miaka mitano hadi kumi nyuma?

Rais Magufuli, kama alivyofanya uhakiki katika maeneo mengine hili alipitie atagundua madudu mengi ya vyeti feki vya kuzaliwa kutoka RITA wakati huo ikiitwa Vizazi na Vifo.
 
Kumbuka malimbikizo ya watumishi yaliyohakikiwa tayari , walisema soon watalipa . Months passed, nothing happen.
A madness system.
 
Kumbuka malimbikizo ya watumishi yaliyohakikiwa tayari , walisema soon watalipa . Months passed, nothing happen.
A madness system.
Wanajifanya kusubiri uhakiki wa vyeti ili wapate sababu ya kuchelewesha malipo ya wafanyakazi kwa hoja kwamba ripoti ya vyeti feki haijamfikia mkuu

Hela ya kuwapa wazungu wanaouza reli na ndege zipo,za kumpa mlalahoi inazungushwa kweli kweli
 
Kumbuka malimbikizo ya watumishi yaliyohakikiwa tayari , walisema soon watalipa . Months passed, nothing happen.
A madness system.
Lakini mbona kama ni kujiongezea mzigo uje kuubeba kwa pamoja? Kustaafu kunaendelea,hakusubiri wanyuma walipwe kwanza!
 
Watanzania kweli tunaongea maana kuna mada ukizisoma sana hata uelewi njia yake ni nini.

Mfanyakazi wakati anaajiriwa alijaza taarifa zake yaani personal particulars, na kumbuka taarifa hizo zote zipo.Sasa uhakiki wa umri unatoka wapi?

Na watu hata vyeti vya kuzaliwa hawana kama Rais alipokuwa anatoa tamko la kufuta agizo la Dr Mwakyembe kuhusu kufunga ndoa kwa kuwakilisha kwanza cheti cha kuzaliwa.
 
Upo ukweli kwamba kuna wafanyakazi wengi wa serikali wana kumbukumbu za uongo juu ya umri wao, wamedanganya wakionyesha umri wao ni mdogo ili wachelewe kustaafu.Lakini tunasahau kwamba kwa kufanya hivyo wazee hao huziba nafasi za wahitimu kutoka vyuo mbalimbali nchini na inawezekana tatizo la ajira rasmi nchini linaweza likawa sivyo lilivyo sasa. Wahitimu hawa wapya watapataje ajira huku nafasi zinaendelea kushikiliwa na wanaopaswa kustaafu, wengine hata miaka mitano hadi kumi nyuma????Rais Magufuli, kama alivyofanya uhakiki katika maeneo mengine hili alipitie atagundua madudu mengi ya vyeti feki vya kuzaliwa kutoka RITA wakati huo ikiitwa Vizazi na Vifo.
Stress za kukosa ajira mbaya sana, mtafukua mashimo yote na hamta pata panya wala panya buku.
 
Upo ukweli kwamba kuna wafanyakazi wengi wa serikali wana kumbukumbu za uongo juu ya umri wao, wamedanganya wakionyesha umri wao ni mdogo ili wachelewe kustaafu.

Lakini tunasahau kwamba kwa kufanya hivyo wazee hao huziba nafasi za wahitimu kutoka vyuo mbalimbali nchini na inawezekana tatizo la ajira rasmi nchini linaweza likawa sivyo lilivyo sasa.

Wahitimu hawa wapya watapataje ajira huku nafasi zinaendelea kushikiliwa na wanaopaswa kustaafu, wengine hata miaka mitano hadi kumi nyuma?

Rais Magufuli, kama alivyofanya uhakiki katika maeneo mengine hili alipitie atagundua madudu mengi ya vyeti feki vya kuzaliwa kutoka RITA wakati huo ikiitwa Vizazi na Vifo.
Acha wivu ww,riziki anatoa Mungu
 
Yote hayo yalifanyika wakati wa uhakiki wa wafanyakazi hewa na wengi wetu hasa walimu cheti cha kuzaliwa na baeua za mikataba ya ajira ilikuwa lazima uwakilishe.
Sioni maana tena ya kuja na uhakiki mpya badala yake huyo aliyekuwa na kazi ya uhakiki ampelekee taarifa ya alichogundua ili hatua stahili zichukuliwe.
Na bado siamini kama taarifa za uhakiki wa wafanyakazi hazijamfikia rais kwani ni zaidi ya miezi 6 imepita. Nashauri mhusika nae atumbuliwe kwa kudelay kupeleka taarifa kwani atakuwa anaichakachua kwa maslahi yake!
Baada ya taarifa hiyo kumfikia basi, awalipe wafanyakazi halali haki zao zikiwa ni pamoja na areas za malimbikizo ya madaraja yao mapya. Vinginevyo nitaamini naye anaucheza mdundo wa mhakiki!
 
Upo ukweli kwamba kuna wafanyakazi wengi wa serikali wana kumbukumbu za uongo juu ya umri wao, wamedanganya wakionyesha umri wao ni mdogo ili wachelewe kustaafu.

Lakini tunasahau kwamba kwa kufanya hivyo wazee hao huziba nafasi za wahitimu kutoka vyuo mbalimbali nchini
na inawezekana tatizo la ajira
rasmi nchini linaweza likawa sivyo lilivyo sasa.

Wahitimu hawa wapya watapataje ajira huku nafasi zinaendelea kushikiliwa na
wanaopaswa kustaafu, wengine hata miaka mitano hadi kumi nyuma?

Rais Magufuli, kama alivyofanya uhakiki katika maeneo mengine
hili alipitie atagundua madudu mengi ya vyeti feki vya kuzaliwa kutoka RITA wakati huo ikiitwa Vizazi na Vifo.

Hovyooo hoja dhaifu sana, wakati wa uhakiki wa vyeti watumishi wa umma walidaiwa mpaka vya kuzaliwa sasa sijui unaongea uharo gani
 
Mwanangu kkarumekenge endelea kusugua benchi tu nyoko wewe kama unasubiri ajira za serikali! Hivi unategemea serikali iwe na uwezo wa kutoa ajira zaidi ya laki 8 kila mwaka kutokana na idadi hiyo kuingia sokoni kila mwaka. Namwomba Rais astishe ajira kwa muda wa miaka mi-3 ili ajipange vizuri, fungu la ajira alipeleke kwenye miundo mbinu ya umwagiliaji!!!
 
Duh mi niliongeza umri ili walau nikistaafu kwa lazma nistaafu na miaka 55 ila kwa hiari basi 50 maana sipendi kuwa mtumwa kwa miaka yote 60
 
Back
Top Bottom