Tatizo lenu wana ccm mmesahau kuwa ukicheka na nyani unavuna mabua.Ikiwa nitajibiwa kwa facts nitaridhika na kuona kuwa sasa JF inao washiriki ambao ni great thinkers haswa sio wale wa matusi na posho. JF hii inapaswa kuwa bora kuliko ilivyo sasa, na inaweza kuwa hivyo tu ikiwa watu wake wanafanya na kusema yale ambayo great thinkers wanatakiwa kuyasema na kuyafanya.
Mkuu unachosema ni kweli haya ni mandalizi ya kitambo yenye malengo maalumu,watu walishasema nchi isitawalike vitu kama hivi tuvitarajie tu kwa watu wapumbavu wenye nia mbaya na taifa letu ila kamwe hawatafanikiwa na mwisho wao waja.
Ikiwa nitajibiwa kwa facts nitaridhika na kuona kuwa sasa JF inao washiriki ambao ni great thinkers haswa sio wale wa matusi na posho. JF hii inapaswa kuwa bora kuliko ilivyo sasa, na inaweza kuwa hivyo tu ikiwa watu wake wanafanya na kusema yale ambayo great thinkers wanatakiwa kuyasema na kuyafanya.
Leo asubuhi ya saa mbili na dakika 56 (08:56:16am) nimepokea ujumbe wa simu kutoka kwa mmoja wa Viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi CCM, ambae kwa cheo ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC). Ujumbe wenyewe ni huu ufuatao:
Ujumbe huu uliniongezea simanzi na majonzi niliyonayo juu ya maafa mbalimbali yaliyojitokeza katika vurugu za Mtwara jana. Simanzi hii ilitokana na kuona hali ya unyonge, woga na wasiwasi mkubwa walionao viongozi wenzangu wa Chama, wasiwasi huo hautokani na woga wa kitoto bali kutokana na hatari wanayoiona mbele yao ya kuwindwa, kushambuliwa na kufanyiwa hujuma na matendo mengine ya kudhuru mwili.
Swali la msingi na lenye kufikirisha ni kwanini wahaini hao wanawalenga wanaCCM..? je inaweza kuwa watu hao wanamlengwa mwingine wa kisiasa ambao unakinzana na CCM hivyo kuifanyia CCM na Viongozi wake mambo haya..? Sitaki kuamini kuwa vurugu hizi zina unasaba wa aina yeyote na Siasa zetu hapa nchini bali najilazimisha kuamini kuwa vurugu hizi ni hujuma na uhaini unaofanywa na wahuni, wahaini ambao hawaitakii mema nchi yetu. Najilazimisha kuamini hivyo kutokana na maana halisi ya Siasa, ama harakati za siasa kuwa hazihafikiani na kinachofanyika mtwara, bali vitendo hivyo vinashabihiana na maana ya hujuma na uhaini kama ifuatavyo.
Maana ya maneno mawili ya mwanzo ya yaani hujuma na uhaini yanafuatana kwa maana hujuma inaweza kutumika kama mkakati wa uhaini. Uhaini ni tendo la kusaliti nchi, serikali au mfadhili; uasi. Hujuma ni shambulio ama vamio: fisidi, kuvuruga ama kuharibu.
Maana ya kipengele cha tatu ambacho kimebeba maneno mawili harakati na siasa, ama siasa ina maana ni mfumo wa mawazo yaongozayo utawala wa serikali ya nchi tafsir nyingine ni utaratibu wa utekelezaji au uendeshaji wa jambo kwa kutumia busara na hekima ili kufikia lengo linalotarajiwa.,na maana ya neno la mwisho yaani harakati ni juhudi zinazoafanywa na watu kwa ajili ya kufikia lengo fulani, bidii, jitihada.
Katika tafsir hizo tatu, kinachoendelea mtwara hivi sasa tunakitoa kabisa katika maana halisi ya harakati za kisiasa, kwa kuwa maana ya harakati za kisiasa ni juhudi za kupanga utaratibu wa mfumo wa mawazo yaongozayo (ama yanayolenga kuongoza) utawala wa serikali ya nchi.
Kwa maana ya Hujuma kuwa ni shambulio, kuvuruga ama kuharibu ni sahihi kwa upande mmoja kuwa hiki ndicho kinachoendelea mtwara lakini kwa tafsir ya uhaini ndiyo hasa inayoelezea kinachoendelea Mtwara.
Ndio ni uhaini uliopangwa na kutekelezwa na watu wenye nia mbaya na nchi hii, wasio wazalendo na waliokosa utaifa. Wanaoendesha mkakati wa nchi kutotawalika, kwa kuibua hujuma mbalimbali dhidi ya serikali na chama kiendeshacho serikali hiyo yaani CCM.
Sio ajenda na hoja ya gesi, bali hoja hii imetumika kimbinu kuendesha mkakati huu wa kihaini ambao unawawinda wanaCCM, ofisi zao, mali zao pamoja na serikali yao. CCM ni chama cha siasa kinafanya siasa ya kuendesha nchi hii, vipo vyama vya upinzani navyo vinalenga kuelekea katika mlengwa huu wa kisiasa, lakini wakati mwingine vinapotoka na kuacha Siasa ama harakati za kisiasa na kujikuta wakifanya hujuma na vitendo vingine vya kihaini. Kwani kama hoja ni gesi vipi vurugu zilenge katika mali, ofisi na uhai wa wanaCCM..?
Watanzania tumeze moto tu hata kama moto ...ukweli kwa hali iliyokuwa inaonekana na kilichotokea jana hapa Mtwara ukweli ulio wazi jambo hili lilipangwa na wako wanaoliongoza ila walikuwa wanangoja sababu ya kuanzia kutekeleza uhaini wao... Cha kushangaza kwa vurugu zinazolipuka wakati huo huo ni nadra kuyapata mabomu ya samaki na magobore, mapanga... Hili jambo tukatae tukubali lilipangwa na wako wanaofanya mipango hiyo.. Na walipanga wafanye hiki na hiki...
Binafsi nawapongeza jeshi la polisi kwa jitihada zao walizozitumi kunusuru hali isiendele kuwa mbaya ukweli hata mkiwabeza lakini ukweli uko wazi wamesaidia kwa kiwango kikubwa..Tukumbuke pia si wananchi wote wanapenda kinachoendelea hapa Mtwara. Naomba JWTZ endelee kuangalia hali inavyoendele ili amani iwepo msiingie kazi kutekeleza sheria za kijeshi mana khali itakuwa mbaya zaidi kwa wananchi mana jeshi 99% mafunzo yao ni kuua..
Shime watz turudi nyuma tuache ushabiki wa kisiasa tuliangalie hili jambo kiiundani zaidi na nyuma kuna nini tusiingizwe kichwa kichwa .
Tatizo lenu wana ccm mmesahau kuwa ukicheka na nyani unavuna mabua.
Wenzenu wanacheza rafu zote ili kuweza kuwatoa madarakani nyie bado mnakenua meno,watu kama kina lema,mwisiga etc wanachochea vurugu serikali inawakamata kwa mda na kuwaacha huku wakipelekwa mahakamani kama geresha tu,mnategemea nini wakati serikali inawakamata wachochezi leo,kesho wanatolewa hukt wakibebwa jujuu na vijana kama mashujaa.ITAKULA KWENU NAWAMBIENI.
Wewe unawasema ccm nyie chadema mmetekeleza lipi au haya ya ugaidi na masndamano.WHEN THE RICH AND CCM ROB THE POOR IT'S CALLED BUSINESS,
WHEN THE POOR FIGHT BACK IT'S CALLED VIOLENCE & UHAINI??
FACE IT...!
Pia nenda kamwambie na boss wako nape sisi tunaskia furaha sana kuwaona mnalia na kusaga meno kias hiki,mambo haya ambayo mmeshindwa kuyatekeleza yalikuwa kwenye ilani yenu wakati mnaomba kura,sasa mmebakiza mwaka mmoja muondoke madarakani bado mnaendelea kuja na kutupa maneno ya kwenye vitabu na ahadi za kusadikika,hilo hatutalivumilia na tumeghair moja kwa moja,na kazi ndio kwanza imeanza....
Makubaliano ya Pinda na wanamtwara yapo bayana tena yakiwa na viongozi wa kaya, viongozi wa kisiasa na hata wa kidini wa mtwara. Makubaliano hayo yanabainisha faida na mafanikio ambayo mtwara kama mkoa utanufaika nayo kutokana na miradi ya gesi, lakini hmakubaliano hayo hayakuwa yakikataza gesi kutoka mtwara na hata neno lenyewe kutoka linatrumika vibaya kwa maana kiasi cha gesi ambacho kitaendesha shughuli zakiuchumi za mtwara ni kubwa na inayokidhi haja kuliko hata itakayosafirishwa kwa ajili ya kufua umeme kwa ajili ya gridi ya Taifa.
Ni upotoshaji wenye nia ile ile ya kuvuruga nchi ndio hasa unapelekea matukio na kadhia hizi zenye kuchafua taswira ya Taifa. Wananchi wa mtwara wanao wawakilishi wanaowaridhia, lakini si tu kuwa kuna wawakilishi, serikali na chama kimefanya juhudi kubwa ya kukutana na kujadili na wananchi wa kawaida kabisa juu ya manufaa yatakayopatikana mtwara. Hivyo hakuna usahihi wa aina yeyote kudai kuwa hawakuandaliwa kisaikolojia.
Wewe KIBE! ishu ya kugoma gesi kugomewa na wanamtwara haikuanza jana ni muda wabunge wa upinzani kwa muda mrefu walipigia kelele bungeni kuhusu mgawanyo wa mapato, mwaka jana wananchi wa mtwara waliandamana sana kupinga, hadi baadhi wakaja ikulu ya dar, na kama utakumbuka vizuri kuna BIBI alilaani kwamba wakichimba tu bomba litatowa maji na sio gesi........., akatumwa mn'goa kucha mmoja kwa bibi wananchi wakamshtukia nusura auwawe akakimbia gari lake likachomwa moto. wananchi wa mtwara wakaendelea kuwa na msimamo kwamba gesi haitoki..kwa hiyo yanayofanyika ni ya wanamtwara wenyewe na sio msukumo toka nje.
1. Silaha za wananchi ni mabomu ya uvuvi,mishale na mapanga ambayo yapo kila siku,miaka yote hayajaagizwa kutoka nje ya nchi.
2. Hivi wewe unataka kuniambia mwananchi akidai haki zake eti "katumwa na wachochezi'' kana kwamba yeye hana akili timamu.......unataka kutuambia hata wazee wetu wapigania uhuru waliambiwa na watu wa nje kwamba nchi zetu zilikuwa zinanyonywa na wakoloni.
3. Hata kama makosa yalifanyika nyuma kwa mikoa ya tabora,shy,mza,mara (migodi ya dhahabu na almasi) sio lazima turudie mtwara.
4. Ingekuwa Mza,A-town,Dar,Moshi serikali ya CCM ingekuja na jibu rahisi kwamba CDM inachochea, ingekuwa Zenj CUF wangetuhumiwa, Sasa mtwara tunadanganya ''mkono wa nje"
5. Wewe kama Mtz em pita vijiwe vya watu wa kawaida Kariakoo,manzese,tandale,Tmk,Kndoni,Mza,Arusha,Musoma,Bk jaribu kuuliza au kusikiliza maoni ya wananchi ndio uende kuwaambia wakuu wako pale lumumba.
6. Tunataka masahihisho yaanzie mtwara, mji ufanane kama miji maarufu ya uchimbaji wa madini kule africa kusini tusirudie makosa ya mwanza,Shy,Tbr,Mara nk.
7. Unaposema mtwara ni mbali, unamaanisha mbali na wapi? kwasababu wanaihitaji gesi watalipia gharama za usafiri kuifuata sababu ni adimu.
8. Eti Mtwara hamna wataalamu ni uongo, Nchi yetu haina wataalamu ndio kwanza wameenda shule.......kama hiyo ni sababu bomba lingejengwa kumwaga gesi urusi ndio kuna wataalam.
9. Wasomi wote wako Dar sababu ya ajira na asilimia zaidi ya 90% si wazawa wa Dar, ni matumaini yangu kwamba hata bomba lingekuwa mtwara bado wasomi wangelifuata mtwara kupata ajira nzuri, mbona migodi ya dhahabu haijahamishwa Tbr,Shy nk lakini vijana wasomi kibao wanakimbilia huko kupata ajira nono.
Kwahiyo ni vema kukaa chini na kuja na suluhisho la juu juu, kwa sasa serikali ya CCM haiwezi kudanganya watu, sababu watu wamekufa kahama,mererani,tarime kwa manufaa ya viongozi walafi pasipo hata manufaa kwa mwananchi. Pia wananchi wakipinga usiuite uhaini, tatizo lako na CCM hamjui kwamba hata Polisi na JWTZ ni watanzania na hawafurahishwi dhuluma kwa wananchi...................
Ninachosikitika ni kuwa wakati tumekubaliana na TandaleOne kwamba tujadili mjadala huu kwa hoja ili kupata kiini hasa cha tatizo; mpasa sasa keshaukimbia mjadala wake aliouanzisha na sijui kama atarudi tena.Akirudi atarudi kama guest.
.Tatizo lenu wana ccm mmesahau kuwa ukicheka na nyani unavuna mabua.
Wenzenu wanacheza rafu zote ili kuweza kuwatoa madarakani nyie bado mnakenua meno,watu kama kina lema,mwisiga etc wanachochea vurugu serikali inawakamata kwa mda na kuwaacha huku wakipelekwa mahakamani kama geresha tu,mnategemea nini wakati serikali inawakamata wachochezi leo,kesho wanatolewa hukt wakibebwa jujuu na vijana kama mashujaa.ITAKULA KWENU NAWAMBIENI.
Na huu utaratibu wa CCM kukimbia mijadala na kuogopa hata hoja wanazoanzisha wao wenyewe; kwa kiasi kikubwa ndio huleta matatizo nchini.Sasa kwa stahili hii ya kukimbia kimbia halafu wanalalamika oooh! sijui nini na nini! any way mimi sina la ziada.mkuu mimi mwenyewe nilishaanza kuvutiwa na huu mjadala, baada ya TandaleOne kuja na hoja badala ya vioja kama siku zote.
Lakini ndio hivyo tena ameingia mitini.!!
Ikiwa nitajibiwa kwa facts nitaridhika na kuona kuwa sasa JF inao washiriki ambao ni great thinkers haswa sio wale wa matusi na posho. JF hii inapaswa kuwa bora kuliko ilivyo sasa, na inaweza kuwa hivyo tu ikiwa watu wake wanafanya na kusema yale ambayo great thinkers wanatakiwa kuyasema na kuyafanya.