Ukweli ni kwamba wanaume wanaokataa kutoa talaka hata pale ambapo wanajua kabisa kwamba, hakuna upendo kati yao na wake zao hufanya hivyo kwa sababu mbalimbali. Kwanza ni kuhofia kwamba, talaka itawagharimu kimali, kwa sababu watatakiwa kugawana mali na hao wake zao.
Pili ni kutaka kuwakomoa wake zao kwa sababu, huenda wao (wanaume) ndio wameshika kwenye mpini katika vurugu hizo. Lakini pia inawezekana ni mfujaji, na kama inavyofahamika kwamba mwanaume mfujaji hana mdhamana. Mwanaume anayefuja, hupenda kuona mwanmke akiteseka kwa vitendo na kauli zake, na mwanamke kutaka kujitoa kwenye kifungo chake ni fadhaa kubwa kwa mfujaji, hawezi kukubali.
Tatu ni kutokujiamini kwa wanaume, ambao huwa wanachukulia kutoa talaka kama jambo lenye kuwadhalilisha sana. lakini pia ni ile dhana kuwa kuwaacha wake hao na kwenda kwenye mikono ya wanaume wengine, itakuwa ni kujishusha sana. Wanaume wa aina hii wanakuwa na wivu wa mbwa kwa majani ya ng'ombe.
Lakini ipo hatari kubwa kwa jambo hili, kwani tumeshuhudia au kusikia kupitia vyombo vya habari juu ya wanawake ambao wamewahi kujiuwa au kuuwa waume zao, kwa sababu ya vurugu za waume zao, kukataa katakata kutoa talaka. Kama hakutaki si umwache…………….!!!!!!!
Mtambuzi
NAomba nisicomment kwenye hii mada yako leo. Ninawezajikuta nakula ban toka kwa kila mod!!
Ni mada nzuri sana aksante.
Mtambuzi naomba kutofautiana nawe kidogo... ndugu yangu talaka hata MUNGU haitaki isipokuwa kwa habari ya uzinzi...kwanini kushangilia talaka na isiwe kutafuta suluhu lau itachukua muda mrefu...kuachana kuna gharama kubwa especially watoto na kuendeleza zinaa(ukimwi je?)...ktk ujane(kujitakia?) kuna sononi hatimaye kifo...ndoa nyingi zimepata afya baada ya suluhu ya muda(kutenganishwa kwa muda)...ni mchango tu.
Mimi sio mhafidhina, huwa nakubali kutofautiana................nimeipokea changamoto yako
Umegundua eeeh!...tulipendana sana mwanzo...nikakuanzishia(ulikopa thru' kibanda chetu) biashara waenda hongkong umependeza,umenawiri...afu waja na hadithi za talaka...akafaidi nani au ndo majaribu?Kuna wengine hawataki kutoa talaka kwa sababu ya mapenzi. Bado wao wanapenda japo kuwa wao hawapendwi. Wako radhi kukaa na wanwake wasiowapenda kwa vile wao wanawapenda.
Mtambuzi naomba kutofautiana nawe kidogo... ndugu yangu talaka hata MUNGU haitaki isipokuwa kwa habari ya uzinzi...kwanini kushangilia talaka na isiwe kutafuta suluhu lau itachukua muda mrefu...kuachana kuna gharama kubwa especially watoto na kuendeleza zinaa(ukimwi je?)...ktk ujane(kujitakia?) kuna sononi hatimaye kifo...ndoa nyingi zimepata afya baada ya suluhu ya muda(kutenganishwa kwa muda)...ni mchango tu.
Mtambuzi,
Hii imekaa kiupande upande, yaani wewe unaamini kuwa vurugu katika ndoa husababishwa na wanaume, na kuwa wanaume ndo wanatakiwa watoe taraka kwa wake zao. Huo ni msimamo ambao umeshapitwa na wakati na hali halisi haiko hivyo. Hakuna utafiti unaothibitisha kuwa panapokuwa na vurugu kwenye ndoa basi wanaume ndo wako responsible!!
Mwanamke akiona anafanyiwa vurugu naye hapendi hizo vurugu na wala hashiriki kwenye hizo vurugu, huwa ana uhuru wa kuondoka na kwenda kutafuta taraka yake mahakamani. Ukiona vurugu zinaendelea na wote wapo, ujue wote ni wabia katika vurugu hizo na wote kila mmoja ana makosa ya kwake!!
Ni rahisi sana kufanya mjumuisho eti wanaume wanaleta vurugu kwenye ndoa bila kufanya utafiti wa kujua kinachosababisha hizo vurugu. Wewe kwa kuwa kwa maoni yako tu unaona kuwa wanawake ni victim wa vurugu (Mambo yakienda physical mara nyingi mwanamke atalia kunyanyaswa) basi umejumuisha kuwa wanaume ndo wenye makosa. Jiulize mara mbili, pengine huna ndoa, ndoa unaiona tu kutokea nje!!
Fanya utafiti ndugu, iko siku unaweza kuyameza maneno yako uliyoandika hapa. Ulichokiandika, hukijui!! Pengine umeangalia case moja au mbili zinazokuzunguka; hujaangalia upana wote wa suala hili! Si rahisi kama unavyofikiria.