Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,806
- 15,379
Kuna wanaume wengi sana ambao ni wagumu kutoa talaka, hata pale ambapo kile kinachoitwa ndoa, sio ndoa bali ni aina ya vurugu iliyokomaa kiasi kwamba mtu kutoka roho ndio hatua pekee iliyobaki. Wanaume hao wanakataa kutoa talaka kwa sababu ambazo haziko wazi.
Ukweli ni kwamba wanaume wanaokataa kutoa talaka hata pale ambapo wanajua kabisa kwamba, hakuna upendo kati yao na wake zao hufanya hivyo kwa sababu mbalimbali. Kwanza ni kuhofia kwamba, talaka itawagharimu kimali, kwa sababu watatakiwa kugawana mali na hao wake zao.
Pili ni kutaka kuwakomoa wake zao kwa sababu, huenda wao (wanaume) ndio wameshika kwenye mpini katika vurugu hizo. Lakini pia inawezekana ni mfujaji, na kama inavyofahamika kwamba mwanaume mfujaji hana mdhamana. Mwanaume anayefuja, hupenda kuona mwanmke akiteseka kwa vitendo na kauli zake, na mwanamke kutaka kujitoa kwenye kifungo chake ni fadhaa kubwa kwa mfujaji, hawezi kukubali.
Tatu ni kutokujiamini kwa wanaume, ambao huwa wanachukulia kutoa talaka kama jambo lenye kuwadhalilisha sana. lakini pia ni ile dhana kuwa kuwaacha wake hao na kwenda kwenye mikono ya wanaume wengine, itakuwa ni kujishusha sana. Wanaume wa aina hii wanakuwa na wivu wa mbwa kwa majani ya ng'ombe.
Lakini ipo hatari kubwa kwa jambo hili, kwani tumeshuhudia au kusikia kupitia vyombo vya habari juu ya wanawake ambao wamewahi kujiuwa au kuuwa waume zao, kwa sababu ya vurugu za waume zao, kukataa katakata kutoa talaka. Kama hakutaki si umwache…………….!!!!!!!
Ukweli ni kwamba wanaume wanaokataa kutoa talaka hata pale ambapo wanajua kabisa kwamba, hakuna upendo kati yao na wake zao hufanya hivyo kwa sababu mbalimbali. Kwanza ni kuhofia kwamba, talaka itawagharimu kimali, kwa sababu watatakiwa kugawana mali na hao wake zao.
Pili ni kutaka kuwakomoa wake zao kwa sababu, huenda wao (wanaume) ndio wameshika kwenye mpini katika vurugu hizo. Lakini pia inawezekana ni mfujaji, na kama inavyofahamika kwamba mwanaume mfujaji hana mdhamana. Mwanaume anayefuja, hupenda kuona mwanmke akiteseka kwa vitendo na kauli zake, na mwanamke kutaka kujitoa kwenye kifungo chake ni fadhaa kubwa kwa mfujaji, hawezi kukubali.
Tatu ni kutokujiamini kwa wanaume, ambao huwa wanachukulia kutoa talaka kama jambo lenye kuwadhalilisha sana. lakini pia ni ile dhana kuwa kuwaacha wake hao na kwenda kwenye mikono ya wanaume wengine, itakuwa ni kujishusha sana. Wanaume wa aina hii wanakuwa na wivu wa mbwa kwa majani ya ng'ombe.
Lakini ipo hatari kubwa kwa jambo hili, kwani tumeshuhudia au kusikia kupitia vyombo vya habari juu ya wanawake ambao wamewahi kujiuwa au kuuwa waume zao, kwa sababu ya vurugu za waume zao, kukataa katakata kutoa talaka. Kama hakutaki si umwache…………….!!!!!!!