Mimi nilianzisha thread ya kuonyesha doubts zangu kuhusu hii issue ya Rubella, ule uzi ukafungwa. Cha kushangaza Pdidy ambaye nina shaka sana na uelewa wake wa magonjwa anaanzisha uzi unaosema Rubella ni hatari kuliko Ebola lakini unaachwa?
Kweli ugonjwa ambao ukimpata mtoto ni mild na huwa unapotea wenyewe ni hatari kuliko EBOLA. JF inakua inazidi vituko kila kukicha.
Mimi binafsi sijapata sababu za kutosha za kumchoma mwanangu hio chanjo. Nimefanya research yangu online na ofisi na WHO sijaona uthibitisho wowote wa utafiti uliofanywa nchini kwetu kuonyesha Rubella ni tatizo.
Huu ni mradi tu watu wametengeneza kupiga hela. HAYO NI MAONI YANGU!
Huu ni mradi wa GAVI Alliance ambao umetengewa zaidi ya USD million 16 na tayari zaidi ya USD mil 1 zimeshatolewa. Nenda google, type rubella in tanzania utaiona document ya huu mradi.
Sasa nyie niambieni kama kweli nia ni kufikia watoto wote, kweli itawezekana ndani ya siku 5/6 kufanya hivyo kwa Tanzania yetu. i.e. tarehe 18 mpaka 24?
Njaa na tamaa itatuponza sana waAfrika kwa kweli. Hapo watu washatengeneza project yao na tayari washavuta hela. Sisi wataalamu wetu wanafanya nini? Kwanini tupokee tu vya kuambiwa nje? Wasomi wetu wamekuja na utafiti wowote au sababu kasema mzungu basi sawa.
Nafikiri na hii post itafutwa kutokana na akili ndogo na uelewa mdogo wa mods. Nishazoea!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.