Void ab initio
JF-Expert Member
- Mar 1, 2015
- 5,713
- 5,643
Avatar sio tatizo wengi wana picha za ajab kama unataka kumsaidia mtu sio lazima uangalie avatar kwani walionishauli wametumia kigezo gani kama hujui kaa kimya usitafute sababu ya watu kutokunisaidiaIla kwa heshima tu na taadhima naomba hiyo avatar uitoe, unaweza usipate matokeo mazuri kwa ndugu yako kwa sababu ya mambo kama hayo.
I am a spiritual man, I know what I am talking about
Avatar sio tatizo wengi wana picha za ajab kama unataka kumsaidia mtu sio lazima uangalie avatar kwani walionishauli wametumia kigezo gani kama hujui kaa kimya usitafute sababu ya watu kutokunisaidia
Pole sana ndugu, kifafa ni tatizo linalotokana na sababu kuu kubwa mbili;
1. Kurithi
Hapa mtu hulilirithi toka kwa wazazi/ukoo. Familia yenye kifafa ina uwezekano wa muendelezo wa vizazi vya wenye kifafa.
2. Kuumia ubongo.
Ubongo unaendeshwa na mfumo wa umeme ambao ukiwa disturbed mfano kupitia kujeruhiwa kichwani kunakopelekea brain injury, kiharusi au birth injury huweza kusababisha kifafa.
Hii kitu haitibiki, ila kikubwa ni kuwa karb na muathirika, pia ondoa vitu vya hatari jirani na alipoangukia. Zipo pia dawa za kutuliza hospitali.
Pole kwa changamoto hiyo, ila mtunze nduguyo kwa upendo. Inaonekana alipokatwa jembe alipata brain injury iliyopelekea kifafa!
Eclat are you a pharmacist??Hata hizi dawa apate pia ushauri wa pharmacist
Sio uongo wataalamu wanaongea kwa mujibu wa uwanda wa taaluma yao, kinachofanyika hata katika watu wanaotumia dawa za kisasa za kifafa kwa usahihi inawezekana mtu akakaa muda mrefu pasina kuwa au kuonyesha dalili za kifafa, nilishawahi kukutana na mtoto ana miaka 12 anatumia hizo dawa lakini hajawahi kupata kifafa wala hajui mtu wa kifafa anakuaje, kilichotokea ni kwamba shida aliipata na kugundulika alivokua bado mdogo sana akawa kwenye matibabu mpaka leo na yuko poa.Wataalamu wa afya wa kisasa wanadai kifafa (epilepsy) hakina tiba.
Huu ni uongo mkubwa,kuna watu waliwahi kuugua lakini baada ya kupata tiba mbadala mpaka leo wana zaidi ya miaka 30 hawajawahi kusiki hata dalili.
Mzungu kawapotosha.